Skip to main content

LULU: Nilidanganya umri kuipa hadhi filamu



MAMA mzazi wa msanii wa filamu Elizabeth Michael 'Lulu', Lucresia Kalugila, amedai kitendo cha mwanawe kutamka mbele ya umma kwamba ana umri wa zaidi ya miaka 18, kililenga kuipa hadhi filamu yake.
Alidai pia kwamba mtoto huyo, alifanya hivyo ili kuepuka unyanyapaa ambao ulikuwa ukifanywa dhidi yake na wasanii wenzake katika sanaa ya filamu wakimwelezea kuwa ni mtoto.
Lucresia alidai hayo kupitia hati ya kiapo majibu aliyoiwasilisha Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, akikana mwanae kuwa na umri wa zaidi ya miaka 18.
Hati hiyo ya majibu iliwasilishwa jana mahakamani hapo, mbele ya Jaji Dk. Fauz Twaib na mawakili Kenneth Fungamtama, Peter Kibatala na Flugence Massawe, wanaomwakilisha Lulu.
Mawakili hao waliwasilisha hati hiyo ya majibu baada ya Jamhuri kuwasilisha ushahidi wa CD ya mahojiano ya Lulu na mtangazaji Zamaradi Mketema, maelezo yake aliyoyatoa polisi, maombi ya hati ya kusafiria na leseni ya udereva.
Katika ushahidi huo wa Jamhuri inaonekana muombaji (Lulu) wa kufanyiwa uchunguzi kuhusu utata wa umri wake akisema ana miaka zaidi ya 18.
Kwa mujibu wa hati ya majibu ya mzazi wake Lulu, ameapa kwamba mwanae majina yake ni Elizabeth Michael Kimemeta na Diana Elizabeth Michael Kimemeta na siyo Diana Michael Kimemeta.
Mama huyo, pia amedai kuwa alimuliza Lulu sababu za kusema ana umri zaidi ya miaka 18 wakati si kweli ambapo alimjibu alifanya hivyo ili kuweza kuipa hadhi filamu yake.
Akifafanua, alidai Lucresia anaamini kwamba kama mwanawe angepewa msaada wa kisheria pamoja na wa wawazi kuwepo wakati akihojiwa polisi akiwa katika wakati mgumu na mwenye msongo wa mawazo, angeweza kusema umri wake sahihi ambao ni miaka 17.
Mama huyo amedai kwamba anaamini kuwa Lulu kutokana utoto wake, alitoa matamko ya uongo ili aweze kupata hati ya kusafiria la leseni ya udereva na kwamba si kweli amezaliwa Aprili 17, mwaka 1991 kama alivyoeleza. Amedai angekuwa kazaliwa tarehe hiyo angekuwa na miaka 21 kitu ambacho si kweli.
Lulu anayekabiliwa na kesi hiyo, iliyopo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, aliwasilisha maombi katika Mahakama Kuu ya kufanywa uchunguzi wa umri wake.
Jaji Dk. Twaib amepanga kusikiliza maombi hayo baada ya pande zote kuwasilisha ushahidi wao, Jumatatu wiki ijayo. Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.