Skip to main content

Simba Wamkatia Tamaa Yondani




WAKATI mwenyekiti wa Simba, Ismail aden Rage akijigamba kulijumuisha jina la mchezaji Kelvin Yondani katika usajili, habari ambazo Mwananchi imezipata, ni kwamba klabu hiyo imeamua kuachana na mchezaji huyo.

Simba ilikuwa ikihaha kumnusuru beki huyo ambaye amekwishajichomoza Yanga na hata kuanza mazoezi wakitaka kumrejeshea fedha zake apeleke Yanga na arudi kundini.

Hatua hiyo ilifikiwa baada ya Yondan kuanza mazoezi Yanga, na viongozi na wadau wakubwa wa Simba walikuwa katika hekaheka za kumrudisha kundini.

Awali Habari ambazo Mwananchi ilizipata zilidai kuwa mdau mmoja wa Simba alikutana na wadau na viongozi wa Simba pamoja na Yondani mwenyewe wakimshawisi wampatie fedha, kiasi alichochukua ili azirejeshe Yanga.

Chanzo cha habari kinasema kuwa wadau na wapenzi wa Simba hawakuridhishwa na hatua ya beki huyo kwenda Yanga na kwamba anahitajika kwa kiasi kikubwa Simba.

Baada ya Yondani kuonyesha kuanza mapenzi mapya na Yanga, watu wa karibu wa Simba wamepitisha azimia la kuachana na beki huyo huku wakiamini kuwa wachezaji waliopo wanaweza kuvaa viatu vyake.

"Tumeamua kuachana na Yondani baada ya kumuona Lino Musonda, anacheza vizuri beki wa kati na tunaamini atatusaidia," kilipasha chanzo hicho.

Kiliendelea kudai chanzo hicho kuwa, wasiwasi mkubwa ulikuwa beki wa kati lakini baada ya kupatikana Musonda, kwa pamoja waliridhia beki huyo aende akacheze soka Yanga.

Wakati hayo yakijiri jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage alikaririwa na Mwananchi Jumapili akikazia kusema Yondani amekwenda Yanga kutia mashamsham ya mazoezi lakini bado ni mchezaji wao halali.

"Yanga wanajifurahisha wenyewe na kelele zao kamwe hazinitishi...mimi nasema mbivu na mbichi vitajulikana Juni 30 tutakapoweka hadharani kikosi chetu kitakashiriki Ligi Kuu msimu ujao," alisema Rage.

Katika hatua nyingine, kocha wa Simba, Milovan Cirkovic aliyewasili jijini Dar es Salaam juzi usiku akitokea Serbia alikokuwa kwa mapuziko, anatarajia kuanza mikakati yake leo ya kuinoa Simba kwa Michuano ya Kagame iliyopangwa kuanza kutimua vumbi Julai 14 mwaka huu.

Kocha huyo pia ataitumia nafasi hiyo kuangalia uwezo wa wachezaji wapya wa kikosi hicho ambao walisajiliwa na hivi karibuni bila ya yeye kuwepo licha ya uongozi wa kilabu hiyo kudai kuwa ulikuwa umepata baraka zake zote.

Kikosi cha mabingwa hao wa Ligi Kuu ambacho kilikuwa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Michuano ya Kagame.

Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema kuwa timu hiyo haina muda wa kupoteza kwa sasa na leo jioni itaendelea na mzoezi yake kwenye Viwanja vya Klabu ya Sigara, TCC, Chang’ombe, Dar es Salaam.

               Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/sport

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.