Skip to main content

TANZIA YA MAREHEMU WILLY EDWAR



Bodi ya Wakurugenzi na wafanyakazi wa Jambo Concepts Ltd inayochapisha gazeti la Jambo Leo na Jarida la Jambo Brand wanapenda kuwajulisha Watanzania na wanahabari wote nchini kwamba Mhariri Mkuu wa gazeti hilo, Willy Edward Ogunde amefariki dunia mjini Morogoro.
Tunasikitika mno kuondokewa na mfanyakazi wetu ambaye alikuwa mchapakazi na mwenye ueledi mkubwa katika tasnia ya uandishi wa habari. Kwa wanaomfahamu Willy watakuwa mashahidi wa hilo tunalosema.
Hadi sasa hatujapata taarifa rasmi za kidaktari kuhusu kifo chake, lakini taarifa zilizopatikana kutoka kwa ndugu wa marehemu zinasema alikuwa anasumbuliwa na tatizo la moyo. Mwili wa marehemu utawasili leo, Juni 17, 2012 na maandilizi ya mazishi yanaendelea.

Wasifu

Willy Edward Daniel Ogunde ambaye alikuwa Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo alizaliwa Machi 7, 1974 katika Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.
Alisoma shule ya msingi Mapinduzi mwaka 1983 hadi 1989 kisha elimu ya Sekondari katika shule ya Serengeti mwaka 1990 hadi 1993.Baadaye alijiunga na shule ya Sekondari Musoma kidato cha tano na sita mwaka 1994 na 1995.
Mwaka 1996 alijiunga na Kampuni ya uchapishaji wa magazeti ya BTL akiwa mwandishi wa gazeti wakati huo likiitwa Majira Jioni.
Akiwa na kampuni hiyo alipata mafunzo mafupi ya kikazi yakiwemo ya kompyuta na ya uandishi wa habari.
Mwaka 1998 alihamishwa kitengo kutoka kwenye gazeti la Majira Jioni kwenda kwenye gazeti jipya la Dar Leo na kuwa mwandishi wa habari wa gazeti hilo lakini pia akishikilia nafasi ambazo alikuwa akizitumikia kwenye gazeti la Majira Jioni.
Alifanikiwa kuaminika na kutokana na uwezo wake kazini alipanda daraja na kuwa Mhariri wa gazeti la Dar Leo kuanzia mwaka 2002 hadi 2005.
Kipindi cha mwaka 2006 hadi 2007 alikuwa akitumikia nafasi ya Mhariri Msaidizi wa Michezo gazeti la Majira na baadaye 2006 hadi 2007 akawa Mhariri wa Michezo wa gazeti hilo .
Mwaka 2006 hadi 2007 alipata cheti cha elimu ya uandishi wa habari katika Chuo cha Ceylon (CSJ).
Amesafiri nchi mbalimbali duniani katika kuripoti habari za michezo na burudani ikiwemo Afrika Kusini mwaka 2003 hadi 2006 kwenye mashindano ya Big Brother Africa.
Pia mwaka 2007, 2008 na 2009 Kenya, Senegal na Uingereza kuripoti habari za michezo kupitia Super Sport.

Mei mwaka huu alisafiri kwenda nchini Uturuki kwenye kongamano la wadau wa masuala ya mawasiliano ambako alikuwa kiongozi wa wahariri waliotoka Tanzania na kutoa mada iliyohusu mwenendo wa vyombo vya habari nchini Tanzania.
Nje ya kazi ya uandishi wa habari mwaka 2008 na 2009 alifanya kazi katika kampuni ya matangazo ya ZK akiwa Ofisa Habari na Uhusiano.
Miongoni mwa vyombo vya habari ambavyo aliwahi kufanya kazi enzi za uhai wake ni pamoja na Kampuni ya New Habari ambayo aliitumikia mwaka 2007 na 2008 akiwa Mhariri Msaidizi wa gazeti la Bingwa.
Hatimaye mwaka 2008 alikuwa Mhariri Mkuu wa gazeti la Bingwa kabla hajaacha kazi katika kampuni hiyo na kujiunga na Kampuni ya ZK.
Alijiunga na gazeti la Jambo Leo mwaka 2010 akiwa Mhariri wa Habari na kuanzia mwaka jana hadi mauti ilipomkuta alikuwa Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo.
Taarifa hii imetolewa na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concepts Ltd,
Ramadhan Kibanike

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.