Mwandishi Manyerere aliyefanya mahojiano haya akiwa na wanauamsho
Haya ndiyo madai ya Uamsho kuuvunja Muungano
*Wasema bayana kwamba wanataka Zanzibar iwe 'Sovereign State', ijitawale yenyewe
*Wasema Dar es Salaam ilikuwa ya Zanzibar, maili kumi kuingia ndani, mikataba ipo
*Kiongozi ahoji: Kilomita chache zinakushughulisheni wakati mna mapori tele
Jumuiya
ya Uamsho ya Visiwani Zanzibar hivi karibuni ilijikuta matatani, baada
ya Jeshi la Polisi kutumia mabomu ya kutoa machozi kutawanya wafuasi
wake. Mwandishi wa gazeti la JAMHURI, Manyerere Jackton, amefanya
mahojiano ya ana kwa ana na Amiri Mkuu wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar,
Sheikh Farid Hadi Ahmed, aliyeeleza lengo kuu la Jumuiya hiyo ya
Kiislamu.
JAMHURI: Ni nini chanzo cha vurugu za Mei 26?
Sheikh
Farid: Kilichotokea hapa kwa muda mrefu, japo inasikika Jumuiya ya
Uamsho ndiyo inayofanya mihadhara, lakini ni Umoja na Jumuiya za
Kiislamu ambazo zimekuwa zinaendesha mihadhara. Tumefanya mihadhara
zaidi ya mia moja hadi sasa - mikutano zaidi ya mia pamoja na
makongamano tofauti. Na lengo zaidi hapo awali lilikuwa ni kuwaelimisha
watu kujua Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na kuona ni jinsi gani
inawabana Wanzibari na haijawapa ile haki yao ya kuujadili Muungano.
Na baada ya hapo kilichokuwa kinazungumzwa zaidi ni kuwaelimisha wananchi kujua haki yao, kujua.... Soma zaidi.. http://www.kwanzajamii.com
Comments