Pagan Amun ni mjumbe wa kutoka serikali ya Sudan Kusini aliyepo Addis Ababa, na hapa anazungumzia madhumuni la mkutano huo. " Mkutano wetu unatupia jicho kuwepo utaratibu wa kuweka mikakati ya usimamizi wa mipaka baina ya nchi zetu mbili, pia kuunda kamati ya kupokea malalamiko ya pande zote mbili kama kukiwa na upande mmoja umekiuka makubalino ya mipaka yaliyofikiwa."
Mkutano huu, ukibarikiwa na Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika, AU, umeanza jana, huku wajumbe kutoka pande zote na viongozi wakuu wakikutana ili kuepusha kutokea kwa mapigano ya mpakani kwenye maeneo yanayogombaniwa, ambapo utata juu ya mipaka ya sasa na ile ya zamani likiwa tatizo kubwa.
Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika wamezipa Sudan muda wa miezi miwili, hadi Agosti 2, ziwe zimeshapata suluhu juu ya mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na kuainisha mpaka wa kila moja, usafirishaji wa mafuta na masuala ya uraia.
Comments