Skip to main content

Wanafunzi Walemavu Mafinga Waipigia Magoti Serikali






Na Joachim Mushi, Thehabari.com- Mafinga

WANAFUNZI wenye ulemavu anuai katika Shule ya Msingi Makalala wameiomba
Serikali na wadau wengine kuwasaidia kuwajengea mazingira bora ya
kujifunzia kwa watoto wenye ulemavu ili waweze kupata elimu bora kama
ilivyo kwa watoto wengine.

Kauli hiyo imetolewa katika risala ya wanafunzi hao iliyosomwa jana
Wilayani Mafinga kwenye maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika iliyofanyika
kiwilaya kwenye Shule ya Msingi Makalala nje kidogo ya Mjini wa Mafinga.

Katika maelezo yao watoto hao wameiomba Serikali na wadau wengine
kuwatizama kundi la watoto wenye ulemavu anuai kwa jicho la karibu, hasa
katika uboreshaji wa mazingira jumuishi ya kujifunzia katika shule zenye
watoto wenye ulemavu.

Pamoja na hayo wanafunzi hao walemavu wameomba kuboreshewa mazingira ya
lijifunzia katika Shule yao ya Makalala, ikiwa ni pamoja na kuwajengea
chumba maalumu kwa ajili ya kujifunzia kitakachokidhi mahitaji ya kundi
hilo maalumu.

Akizungumza katika maadhimisho hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Mafinga, Bi. Farida Mwasumilwe alisema licha ya Serikali
kujitahidi kuboresha huduma mbalimbali kwa watu wenye ulemavu bado kuna
changamoto nyingi hivyo kuomba wadau kushirikiana kwa pamoja kuwasaidia
watu wenye ulemavu hasa watoto.

Bi. Mwasumilwe aliwataka wadau mbalimbali kusaidiana kutoa elimu kwa baadhi
ya wazazi ambao bado wamekuwa na kasumba ya kuwaficha watoto wenye ulemavu
ndani hivyo kukosa haki za msingi ikiwemo elimu, ambayo ndio mkombozi pekee
kwa kundi hilo.

"Naomba tusaidiane kuwafichua watoto wote walemavu ambao baadhi ya wazazi
wamekuwa wakiwaficha ndani hivyo kukosa haki yao ya msingi. Pia jamii haina
budi kusaidia malezi ya watoto kwani mzigo huu sio waserikali pekee,"
alisema Mwasumilwe ambaye ni Ofisa wa Elimu Shule za Msingi Wilaya ya
Mafinga.

Katika maadhimisho hayo yalioambatana na michezo mbalimbali kwa makundi ya
watu wenye ulemavu, Shirika la Sightsavers limeahidi kumalizia ujenzi darasa la kisasa pamoja na baadhi ya vifaa vya kujifunzia litakalokuwa na uwezo wa kufundishia wanafunzi wenye ulemavu shuleni hapo.

Shirika hilo mbali na kukabidhi fimbo 35 maalumu za kutembelea kwa wanafunzi wasioona pia limeahidi kutoa gari la kisasa kwa shule ya Makalala ili kuwasaidia wanafunzi walemavu hasa wasioona kupata huduma zao nje ya kituo hicho pale inapohitajika. (kila fimbo moja ina thamani ya sh 50,000 za kitanzania).

Maadhimisho hayo yaliandaliwa na taasisi anuai zinazofanya kazi na watu wenye ulemavu, zikiwemo Chama cha wasioona Tanzania (TLB), Kituo cha Habari Kuhusu Walemavu nchini (ICD), Sightsavers, CCBRT, INUKA, SHIVYAWATA kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania. Kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka huu inasema, "Haki za Watoto wenye Ulemavu; Ni Jukumu letu Kuzilinda, Kuziheshimu, Kuziendeleza na Kuzitimiza".

*Habari hii imeandaliwa na Mtandao wa Thehabari.com (www.thehabari.com) kwa kushirikiana na Kituo cha Habari Kuhusu Walemavu Tanzania (ICD)

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AFANYA MAHOJIANO NA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Moh amed Shein,alipokuwa akifanya mahojiano na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kupitia ZBC TV na kutoa wito kwa Watanzania hasa wa Zanzibar kushiriki kikamilifu katika zoezi la uandikishaji vitambulisho hivyo,ambapo zoezi hilo  linatarajia kuwanza Oktoba 15 mwaka. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu mjini Zanzibar leo,(kulia) Mtangazji wa ZBC TV Nasra Nassor. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...