Naibu
Katibu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bw. Selestine Gesimba
(katikati) akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu makubaliano
baina ya Serikali na Viongozi wa Taasisi za Kiislamu kuhusu mgogoro wa
shule ya Sekondari Ndanda iliyoko Masasi mkoa wa Mtwara leo jijini Dar
es salaam ambapo pamoja na mambo mengine serikali
itawarudisha shuleni mwaka huu wanafunzi wote 62 waliohusika na mgogoro
wa shule hiyo. Wengine kutoka kushoto ni Sheikh Musa Kundecha, Amir wa
Baraza kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania na Bw. Samweli
Kusaga kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi, Idara ya Sekondari.
(PICHA NA ARON MSIGWA WA MAELEZO- DAR ES SALAAM)
Viongozi
wa Taasisi za Kiislamu Tanzania wakiongozwa na Sheikh Musa Kundecha
(pili kutoka kulia) ambaye ni Amir wa Baraza kuu la Jumuiya na Taasisi
za Kiislamu Tanzania wakijadili jambo na Rais wa Jumuiya ya wanafunzi
wa Kiislamu Tanzania (TAMSYA) Jaafar Mneke (katikati) leo jijini Dar es
salaam mara baada ya kumalizika kwa mkutano uliojadili makubaliano
baina ya Serikali na Viongozi wa Taasisi za kiislamu kuhusu mgogoro wa
shule ya sekondari Ndanda.
Rais
wa Jumuiya ya wanafunzi wa Kiislamu Tanzania (TAMSYA) Jaafar Mneke
(kulia) akitoa taarifa kwa waandishi wa habari ya kusitishwa kwa
maandano yaliyokuwa yamepangwa kufanyika kesho nchini nzima kufuatia
makubaliano yaliyofikiwa kuhusu mgogoro wa shule ya sekondari Ndanda.
Baadhi
ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Ndanda waliosimamishwa masomo
kufuatia mgogoro wa shule hiyo wakifuatilia tamko la makubaliano ya
viongozi wa dini ya kiislamu na Serikali lililotolewa leo jijini Dar es
salaam na Naibu Katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bw.
Selestine Gesimba kufuatia mkutano wa pamoja uliofanyika tarehe 7 mwezi
huu.
Wanafunzi
wa shule ya Sekondari Ndanda waliosimamishwa masomo yao kufuatia vurugu
zilizotokea katika shule hiyo wakitoka ndani ya jengo la Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa
kusoma makubaliano uliowahusisha viongozi wa dini ya Kiislamu, Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na waandishi wa habari ambapo makubaliano
hayo yameeleza kuwa serikali itawarudisha shuleni wanafunzi wote 62
waliosimamishwa,kuhakikisha kuwa shule ya sekondari Ndanda ina
mazingira mazuri kwa wanafunzi wa dini zote kitaaluma na kuwawezesha
kufanya ibada zao, shule zote zilizotaifishwa ni miliki ya serikali
kiuendeshaji, ardhi na majengo vyote ni mali ya serikali na serikali
kufanya utaratibu wa kuwepo vikao na viongozi wa asasi za dini zote.
Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.
Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.
Comments