MWANAMUZIKI, mwigizaji na mtunzi wa nyimbo, Tevin Campbell, alizaliwa Novemba 12, 1976 katika mji wa Waxahachie, Texas, Marekani, na alikuwa akipenda muziki tangu akiwa mdogo.
Campbell alianza kwa kuimba nyimbo za kwaya kanisani, kwanza kama mwanachama wa kwaya, na kisha mpiga solo katika Kanisa dogo la Jacob katika nji mdogo wa kusini mwa Dallas, Texas.
mwaka 1988, rafiki wa mama yake alimtaharisha Campbell kuimba na mwanamuziki wa jazi, Bobbie Humphrey, njini New York ili wamwimbie. Humphrey alimpenda Campbell na kuikabidhi kanda ya muziki aliyoimba naye kwa Warner Bros.
Hii ilipelekea kufanyika mkutano na Benny Medina, makamu wa rais wa Warner na maneja mkuu wa mauzo ya muziki wa watu weusi.
Campbell alitambulishwa kampuni ya R&B World na Quincy Jones mwaka 1989. Nyimbo ya kwanza singo ya Campbell inaitwa "Tomorrow (A Better You Better Me)" ambayo ilishika nafasi na.1 katika chati za Billboard za muziki singo za R&B/Hip hop mwaka 1990.
Baada ya kufanya kazi na Jones na watunzi na maprodyuza akiwemo Siedah Garrett,Campbell alifanya kazi pia na maprodyuza kama Narada Michael Walden, Al B. Sure, Babyface, na wengineo kurekodi muziki wa ziada.
Nyimbo ya Campbell akiwa peke yake inaitwa "Round and Round", ambayo ilishika nafasi ya tatu katika chati za R&B mwaka 1990. Mwaka 1991 Campbell alitoa albamu kwa jina T.E.V.I.N, ikiwa ya kwanza baada ya mafanikio ya singo zake mbili, "Tell Me What You Want Me To Do," "Alone with You", ikifuatiwa na "Goodbye".
Albam yake ya pili iliitoa 1993 ikibeba jina la 'I'm Ready', maprodyuza wakiwa Jones na Medina. "Nilitaka kutoa albamu yangu ya pili kuonesha ukomavu wangu wa akili kwa sasa," Campbell alimweleza J. R. Reynolds katika gazeti la Billboard.
"Albamu yangu ya 'I'm Ready' inazungumzia mimi kwa sababu ya mambo mengi yaliyonisibu miaka minne iliyopita au zaidi. Natumaini watu watatambua mimi si mtoto tena kama ilivyokuwa kwenye albamu yangu ya kwanza."
Mwaka 1994, Campbell alitoa singo nyingine, "U Will Know," akiwa na kundi la muziki wa R&B la Black Men United, kundi ambalo pia lilimjumuisha mwimbaji Usher. Mwaka 1995 alitoa nyimbo mbili "Eye to Eye" na "Stand Out.



Comments