Pichani chini ni Hoteli ya kitalii ya Nashera alipokuwa Mhe. Malima. picha ya juu kwa hisani ya John Nditi.
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Adamu Kighoma Malima ameibiwa vitu vyake
alivyokuwa navyo vianavyokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya sh.
milioni 15 katika hoteli ya kitalii ya Nashera ya mjini Morogoro.
Taarifa za kipolisi zilizopatikana kutoka mjini hapo zimethibitisha kutokea wizi huo zikisema ulitokea usiku wa kuamkia leo ndani ya hoteli hiyo aliyokuwa amefikia katika ziara yake mkoani Morogoro.
Taarifa za kipolisi zilizopatikana kutoka mjini hapo zimethibitisha kutokea wizi huo zikisema ulitokea usiku wa kuamkia leo ndani ya hoteli hiyo aliyokuwa amefikia katika ziara yake mkoani Morogoro.
SITA UWANJANI LIGI KUU YA VODACOM WIKIENDI HII
Michuano
ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara
inaendelea wikiendi hii kwa mechi tatu zitakazokutanisha timu sita
kwenye viwanja tofauti.
Yanga
itakuwa mwenyeji wa Azam katika mechi itakayochezwa kesho (Machi 10
mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Machi 11 mwaka huu kutakuwa
na mechi kati ya Simba na Toto Africans ya Mwanza itakayochezwa kwenye
uwanja huo huo.
Viingilio
katika mechi hizo vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya rangi ya bluu na
kijani, sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa viti
vya VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 15,000.
Mechi
nyingine itakayochezwa Machi 11 mwaka itakuwa kati ya Polisi Dodoma na
Kagera Sugar. Mechi hiyo itachezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini
Dodoma.
Jumatano
ya Machi 14 mwaka huu kutakuwa na mechi mbili. Simba watakuwa wageni wa
Polisi Dodoma kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma wakati Yanga
watakuwa wenyeji wa African Lyon kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Chanzo;Full Shangwe
Chanzo;Full Shangwe


Comments