Skip to main content

KIHAMA CHA STESHENI ZA RADIO NA TV DESEMBA 31 SAA 6 USIKU


vituo vya radio nchini vingi kujifunga vyenyewe kwa kuingia kwa teknolojia ya Dijitali

Nchi yetu itasitisha rasmi matumizi ya teknolojia ya utangazaji ya analojia na kuhamia teknolojia ya dijitali ifikapo tarehe 31 Desemba, 2012 saa sita usiku.
Lengo la kufanya hivyo ni kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano duniani kote,Miongoni mwa faida za kutumia teknolojia ya dijitali ni kuongezeka kwa ubora wa matangazo ya televisheni, ongezeko la chaneli za televisheni litakalotokana na matumizi bora ya masafa, kuwepo kwa masafa ya ziada yatakayopatikana baada ya kuzimwa kwa mitambo ya analojia inayotumia masafa mengi, kuongezeka kwa watoa huduma wa mawasiliano ya simu, matangazo ya televisheni kupatikana katika vifaa vingi zaidi vya mawasiliano kama vile simu za mkononi na kompyuta kupitia mtandao wa intaneti.
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano inakua kwa kasi sana na hivyo kuwa kichocheo katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Kufuatia kasi ya ukuaji wa teknolojia, sekta ya utangazaji ipo katika mabadiliko kutoka mfumo wa teknolojia ya analojia kwenda mfumo wa wa digitali duniani kote. Hii inatokana na changamoto zinazoikabili teknolojia ya analojia ikiwemo uhafifu wa picha na sauti, matumizi makubwa ya masafa na nishati, pamoja na teknolojia inayopitwa na wakati ya kurushia matangazo ya aina hiyo.Ndi

Comments