Skip to main content

Darasa La Tano Na Sita Watumia Darasa Moja Huko Kisarawe



Wanafunzi wakiwa wa darasa la Tano na la Sita wakiwa  darasani kwa pamoja
WAKATI Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi nchini ikijipanga kuanza kufundisha kwa kutumia teknolojia ya kompyuta katika shule mbalimbali, wanafunzi wa darasa la tano na sita wa Shule ya Msingi Mengwa bado wanatumia darasa moja kwa wakati mmoja. 
Hali hiyo imejulikana juzi baada ya mwandishi wa habari hizi kutembelea shule hiyo, iliyopo Kata ya Maneromango, Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mengwa, Peter Gadie alisema kitendo cha wanafunzi hao kutumia darasa moja kimefanya wapunguziwe muda wa vipindi wa kawaida ili kupishana kwa zamu kutumia darasa hilo.
Alisema badala ya kila kipindi kufundishwa kwa dakika harobaini walimu wameamua kufundisha kwa dakika ishirini kila kipindi ili kupeana zamu kuwafundisha wanafunzi hao.

Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia darasa hilo likiwa na wanafunzi wote yaani wa darasa la tano ambao wapo 24, na darasa la sita wakiwa 29 wakiendelea na masomo kwa pamoja huku wakitenganishwa kwa mistari ya madawati.
Akizungumzia staili ya ufundishaji wa walimu kwa kutumia darasa moja, Gadie alisema mwalimu wa darasa la tano anapoingia darasani huendelea na kipindi kwa dakika 20 huku akiwataka wanafunzi wa darasa la sita kujiinamia na kujisomea ama kuendelea na kazi walizoachiwa na mwalimu aliyetoka punde.
"Anapoingia mwalimu kufundisha darasa moja uwaamuru wanafunzi wa darasa lingine wajisomee
 ama kuendelea kufanya kazi ambazo wameachiwa na mwalimu aliyetoka...kweli wanapata usumbufu lakini haina namna maana tunaupungufu wa madarasa shuleni kwetu," alisema Gadie akizungumza na mwandishi wa habari hizi.
Aidha alisema tatizo hilo halipo kwa wanafunzi wa darasa la sita na la tano pekee, kwani wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili nao usomea darasa moja kwa kupokezana saa; ambapo darasa la kwanza huingia saa mbili hadi saa sita na baadaye kuwapisha darasa la pili ambao huingia saa sita na kuendelea hadi mchana.
Alisema upungufu wa vyumba vya madarasa umeifanya shule hiyo kukodisha ukumbi wa kuoneshea video kijijini Mengwa na kulifanya darasa la awali kwa wanafunzi wa shule hiyo wanaosoma darasa la awali kabla ya kujiunga na darasa la kwanza.
Habari hii imeandaliwa na Mtandao wa Thehabari.com (www.thehabari.com) kwa kushirikiana na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP).

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...