Skip to main content

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad Ajionea Uvamizi Unaofanywa Nje ya Uzio Wa Uwanja wa Amaan Zanzibar


 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Habari, Wizara na Ardhi, na Vikosi vya SMZ baada ya kukagua uchafuzi wa mazingira katika eneo la uwanja wa Amaan.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiangalia uchafuzi wa mazingira nje ya uzio wa uwanja wa Amaan wakati alipofanya ziara ya kutembelea maeneo yaliyovamiwa. Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na MBM Dr. Mwinyihaji Makame, na katikati (mwenye suti) ni Waziri wa Maji, Makaazi, Maji na Nishati Mhe. Ali Juma Shamhuna.
 Meneja wa Uwanja wa Amaan Khamis Ali Mzee, akitoa maelezo kuhusiana na uvamizi wa eneo hilo, wakati Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad alipofanya ziara ya kutembelea eneo hilo.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiwa katika ziara ya kutembelea maeneo yaliyovamiwa nje ya uzio wa uwanja wa Amaan. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib Mhe. Abdallah Mwinyi Khamis na kushoto ni Meneja wa Uwanja wa Amaan Khamis Ali Mzee.
Baadhi ya watendaji wa Wizara ya Habari, Wizara na Ardhi, na Vikosi vya SMZ wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad baada ya kukagua uchafuzi wa mazingira katika eneo la uwanja wa Amaan.Picha zote na Salmin Said -Ofisi Ya Makamu wa Kwanza wa Rais Wa Zanzibar
--

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad ameutaka uongozi wa Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati kulipima upya eneo la uwanja wa Amaan ili likabidhiwe uongozi wa uwanja huo kwa ajili ya kuliendeleza.

Hatua hiyo imekuja kufuatia uvamizi unaofanywa nje ya uzio wa eneo hilo ambao pia husababisha uharibifu wa mazingira kwa kuchimbwa mchanga pamoja na kutupwa taka kiholela.

Maalim Seif ametoa agizo hilo baada ya kutembelea maeneo yaliyofanyiwa uvamizi huo na kutaka hatua za haraka zichukuliwe ili kudhiti uharibifu usiendelee.

Ameitaka Wizara hiyo kulipima tena eneo la nje ya uwanja huo lililobakia na kulimikisha kwa Wizara ya Habari, utamaduni, utalii na michezo, ili liweze kutumika kwa shughuli za maendeleo kama ilivyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kujenga viwanja vya michezo ya ndani (Indoor games).

Ameusisitiza uongozi wa uwanja wa Amaan kuliwekea udhibiti eneo hilo mara wanakapokabidhiwa nyaraka za umiliki, ili kuepusha uvamizi mwengine usije kujitokeza.

Makamu wa Kwanza wa Rais pia amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi kukaa pamoja na watu wanaojishughulisha na upasuaji wa magogo katika eneo hilo, ili kusaidia ulinzi wa eneo linalochimbwa mchanga, sambamba na kuangalia uwezekano wa kubadilisha mfumo wa usafirishaji wa magogo na bidhaa zitokanazo na magogo hayo kwa kutumia usafiri wa magari badala ya ule wa magari ya punda na ng’ombe uliozeleka.

Amesema hatua hiyo itasaidia kudhibiti uchimbaji wa mchanga katika eneo hilo pamoja na kusimamia marufuku ya uingiaji wa wanyama katika eneo la mji.

Katika hatua nyengine Maalim Seif ameutaka uongozi wa uwanja wa Amaan kukaa pamoja na Wizara ya Habari pamoja na ile inayohusiana na vikosi vya SMZ ili kujadiliana juu ya namna ya kutatua tatizo la ulinzi katika uwanja huo, baada ya kubainika kutokuweko maelewano mazuri kati ya taasisi hizo, hali iliyopelekea walinzi wa JKU kuondoka katika eneo hilo.

Awali meneja wa Uwanja wa Amaan bw. Khamis Ali Mzee amebainisha kuwa walinzi wa JKU waliondoka baada ya kuwalalamikia kwa kutotekeleza majukumu yao ipasavyo.

Nae Mkuu wa Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) Kanal Sudi Haji Khatib amesema walilazimika kuwaondosha askari wao katika eneo hilo baada ya kukosa mashirikiano mazuri kutoka kwa uongozi wa Uwanja wa Amaan.

Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati Mhe. Ali Juma Shamhuna kwa upande wake ameahidi kulishughulikia suala la upimaji wa eneo hilo ndani ya kipindi cha mwezi mmoja na kuchukua hatua zinazostahiki.

Meneja wa Uwanja wa Amaan Bw. Khamis Ali Mzee alidai kuwa sehemu ya eneo linalolalamikiwa aliwahi kupewa mtu kwa ajili ya kuliendeleza lakini ameshindwa kufanya hivyo na kusababisha kuwa sehemu ya kutupia taka (jaa).

Amesema kwa vile uongozi wa uwanja umeshapata muwekezaji atakayeiendeleza hoteli ya uwanjani kuwa na hadhi ya “nyota nne hadi tano”, ni vyema eneo hilo likabidhiwe kwa uongozi wa uwanja huo ili liweze kuwekwa katika hali nzuri, sambamba na kulinda hadhi ya hoteli hiyo.
 
Na 
  Hassan Hamad 
Ofisi Ya Makamu Wa Kwanza Wa Rais Zanzibar

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.