Skip to main content

Dk Kitine,Butiku Wakitabiria Kifo CCM




YUMO PIA KADUMA, WASEMA WANAMTANDAO NI CHANZO CHA UFISADI
Elias Msuya
MAKADA watatu wakongwe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ibrahim Kaduma, Dk Hassy Kitine na Joseph Butiku, wameibuka na kukitabiri anguko chama hicho tawala kwa kile walichosema, kwenda kinyume na misingi ya kuasisiwa kwake.

Kauli za makada hao maarufu, zinakuja kipindi ambacho upepo wa kisiasa umekuwa ukivuma vibaya ndani ya chama hicho kikongwe nchini na barani Afrika, kutokana na vita ya makundi kati ya watuhumiwa wa ufisadi na wale wanaojipambanua kwamba ni wazalendo na wapinga ufisadi.

Wakizungumza juzi usiku katika kipindi cha "Je, tutafika?" Kilichorushwa na kituo cha luninga cha Channel ten, makada hao walitoa kauli hizo nzito huku wakishambulia kundi la wanamtandao ndani ya chama hicho, vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi na vitendo vya ufisadi vinavyolitikisa taifa.

Kaduma
Kaduma ambaye aliwahi kuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Mwalimu Julius Nyerere, alisema hali ndani ya CCM sasa ni mbaya na imefika hapo kwa sababu ya kuacha misingi ya TANU iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere.

“Kwa hali ilivyo, CCM kinaweza kusambaratika wakati wowote. Sisi tuliingia kwenye TANU kutokana na misingi ambayo Mwalimu Nyerere aliiweka,” alionya Kaduma.

Kaduma aliitaja misingi hiyo kuwa ni pamoja na imani kuwa binadamu wote ni ndugu, kuwatumikia watu kwa moyo wote, kujitolea nafsi kuondoa umasikini ujinga na maradhi, rushwa ni adui wa haki hivyo ni kosa kutoa au kupokea rushwa, kutotumia cheo cha umma kwa maslahi binafsi, kusema kweli daima na kuacha fitina, kujielimisha kadiri ya uwezo na kutumia elimu hiyo kwa manufaa ya umma.

Alisisitiza, “Mwalimu hakuwa akiongea nadharia, ndiyo maana mwaka 1955 aliacha kazi aliyokuwa nayo ya ualimu iliyokuwa na mshahara mzuri na kwenda kuimarisha chama cha TANU ilikuwa ni ku-risk (kujiweka kwenye hatari).’’

Dk Kitine
Dk Kitine akizungumzia barua zilizowahi kuandikwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku kwa wenyeviti wa CCM (Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete), na kutojibiwa na viongozi hao, alisema hata angekuwa yeye asingezijibu kwa sababu ndiyo mfumo wa chama hicho kutotatua na kuficha matatizo.

“Barua ya Butiku kwenda kwa Mwenyekiti wa zamani na wa sasa haikujibiwa..., hata ningekuwa mimi nimeandikiwa barua na mambo ninayofanya ni wazi, nisingeijibu. Mimi siwalaumu. Hiyo ni moja ya matatizo na utamaduni wa chama tawala kutokuwa na utamaduni wa kutatua matatizo,” alisema Dk Kitine.

Akizungumzia chanzo cha kuporomoka kwa maadili ndani ya CCM, Dk Kitine ambaye pia aliwahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, alisema yalitokana na kuanzishwa kwa makundi na mitandao ya kusaka madaraka kwenye chama.

“Mitandao na makundi ndani ya CCM, hakikuandikishwa mahali popote. Mtandao ulianzishwa mwaka 1995 na ulikuwa wa vijana. Mwaka huo mtandao huo ulifanya mgomo mbele ya Mwenyekiti Ali Hassan Mwinyi na mbele ya Mwalimu Nyerere wakati huo tunatafuta viongozi,” alisema Dk Kitine na kuongeza:

“Wakati Mzee Mwinyi anatuongoza kama mwenyekiti na amekuja kutueleza maazimio ya Kamati Kuu kwamba kwanini baadhi ya wagombea hawakuwa na sifa, wanamtandao wakasema jambo hilo halikubaliki.”

Aliongeza kwamba, mtandao huo ndiyo umekuwa chanzo cha ufisadi ndani ya chama na kufafanua; “Kundi hilo ndilo sasa linaendesha rushwa, linafanya wanachama wa CCM kuwa hawana maana, linakusanya kadi. Kama wanabisha waje kwenye kikao kama hiki wajieleze.”

Dk Kitine alitaja kashfa za ufisadi zilizovuma kuwa ni pamoja na Deep Green, Kagoda, Meremeta, EPA na kubainisha kwamba zote zina mkono wa kundi hilo la mtandao.

“Lakini yote yanatokana na kuficha matatizo, kwa mfano unapowakataza watu kujadili suala la Muungano, unaficha nini? Sasa haya ya kuficha pia masuala ya Kagoda na mengineyo, ipo siku watu watataka majibu yao tu hata miaka 100 ijayo. Matokeo yake watakichukia chama,” alisema.

Kauli ya Butiku
Katika mjadala huo, Butiku ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, alisema CCM kimebadilika kutoka kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi na kuwa chama cha wafanyabiashara na maslahi binafsi.

“Mnapofanya kazi katika Serikali au chama, wajibu wenu siyo kukiua chama mlichokianzisha kama ni chama chochote au CCM kinachojiita kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi. Kwa bahati mbaya sana wafanyabiashara wengi waliojiingiza katika Chama Cha Mapinduzi, wamegeuka, kazi yao na madhumuni ndiyo yamekuwa malengo mbadala ya chama,” alisema Butiku na kuongeza:

“Mimi naamini biashara ni kazi, lakini kama unachukua malengo ya biashara na kuyafanya kuwa malengo mbadala ya Chama Cha Mapinduzi, chama hicho bado kipo?,” Alihoji.

Butiku ambaye aliwahi kuwaandikia barua Mwenyekiti mstaafu wa CCM Mkapa na Mwenyekiti wa sasa Rais Kikwete akitoa angalizo kuhusu mweleko wa chama hicho, alisema hali ya sasa chama ni mbaya.

“Kwa hiyo wakati ule nilisema chama kimeanza safari ya kifo. Leo ukitazama, ukisikiliza viongozi wanavyosema, ukisiliza matendo yao, uwepo wao wote ni wa kibiashara na si kuimarisha chama hicho, ni kuimarisha malengo yao ya kibiashara na kibinafsi,” alisema Butiku.

Aliongeza kuwa chama hicho kimepoteza maadili kiasi kwamba imekuwa kawaida kwa viongozi kununua kura na kwamba siku hizi, uongozi wa chama unanunuliwa.

"Nani anabisha kwamba CCM hatununui uongozi? CCM viongozi wote wa ngazi mbalimbali, mmoja mmoja anieleze kama siyo kweli kwamba CCM kimekuwa chama cha kukumbatia rushwa na kununua uongozi?,” Alihoji na kuongeza:,Soma zaidi www.mwananchi.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.