Skip to main content

Maamuzi Ya Kamati Ya Nidhamu Dhidi Ya Mh. Aden Rage Na Louis Sendeu




Kikao cha Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF, iliyoketi kusikikiza
mashitaka dhidi ya Alhaj Ismail Aden Rage na Louis Sendeu kilifanyika
leo tarehe 24 Machi, 2012 kilisikiliza tuhuma zilizowasilishwa na TFF.
Mashitaka hayo yalihusiana na matamko yaliyotolewa na watuhumiwa hao
kabla ya mchezo wa Ngao ya Hisani kati ya Simba na Yanga, uliochezwa
tarehe 17 Agosti, 2011.

Katika mashitaka hayo, watuhumiwa hao walituhumiwa kukiuka Kanuni ya
30 (1) (f) na Kanuni ya 53 (1) (2) cha Kanuni za Adhabu za FIFA.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili na kutafakari maelezo hayo,
pamoja na kuchambua sheria na kanuni mbalimbali, Kamati imeamua
yafuatayo:

Hasara kwa Mdhamini

Kuhusiana na suala hasara, Kamati inaona kwamba suala hili halikuwa
na uzito wowote wala hakukuwa na hoja ya msingi, wala ushahidi wa
kuthibitisha kwamba tishio au matamko hayo yalikuwa na uhusiano na
hasara inayodaiwa kwamba mdhamini huyo aliipata. Hakuna malalamiko
yoyote yaliyotolewa kuhusiana na kinachodaiwa kuwa ni hasara
inayotokana na matamko ya viongozi hawa. Kamati imeitupilia mbali hoja
hii.

Tuhuma za matamko ya watuhumiwa

Kamati imebaini kwamba matamko hayo yalikuwa ni uvunjaji wa kanuni
na yalilenga kuchochea hisia mbaya na kuleta vurugu. Kamati ina maoni
ya kwamba viongozi wa vilabu hivi walistahili kufuata taratibu za kawaida
katika kudai haki zao, badala ya kutoa matamko ambayo yangeweza
kuchochea hisia mbaya. Kitendo hicho si cha kiungwana na kinaendana
kinyume na taratibu za uongozi wa mpira.

Wao kama viongozi, walistahili kutumia utashi na kupima athari za
matamko yao, ili kuepuka uwezekano wa kuleta msuguano usio wa lazima
na kuungiza mchezo wa mpira katika kashfa au kukosa heshima. Matamko
haya yanaweza kuwa ni kichocheo kwa viongozi wengine wenye tabia ya
namna hiyo kutumia mwanya huu kufanya vitendo hivyo.

Kwa msingi huo, Kamati inawaona wote wawili kuwa wana hatia na
matamko hayo yanayohusiana na mchezo huo. Kwa kuzingatia hilo,
Kamati inatoa onyo kali dhidi ya watuhumiwa hao wawili na inaonya
kwamba adhabu kali zaidi zitachukuliwa kama watuhumiwa watalirudia
kosa kama hili au linalofanana na hilo.

Kamati imebaini pia kwamba Mheshimiwa Aden Rage amehusika pia na
kutoa maneno ya uchochezi dhidi ya Bwana Saad Kawemba wa TFF,
akidaiwa kwamba alikuwa anazuia usajili wa mchezaji Gervais Kago na
kwamba Bwana Kawemba alifanya hivyo kwa vile ana mapenzi na klabu ya
pinzani ya Yanga.

Pamoja na kwamba hakukuwa na athari za moja kwa moja dhidi ya Bwana
Kawemba, ukweli ni kwamba kitendo hicho kilikuwa ni kosa ambalo
halistahili kufanywa na kiongozi mwenye uzoefu mkubwa wa uongozi kama
Mheshimiwa Rage, na kilikuwa kina dalili za kuchochea chuki zisizo na
msingi dhidi ya Bwana Kawemba. Kitendo hicho kilikuwa kinakiuka kifungu
cha 53 (1) (2) cha Kanuni za Adhabu za FIFA.

Kamati inatoa onyo kali dhidi ya Mheshimiwa Aden Rage kwa kupatikana
na hatia yake hiyo.

Imetolewa na Kamati ya Nidhamu na usuluhishi leo tarehe 24 Machi, 2012.

..................................................
Kamishna Alfred Tibaigana
Mwenyekiti wa Kamati

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...