Skip to main content

Mazishi Ya Mwakilishi Wa Bububu Zanzibar


 Wananchi mbalimbali wakiwa wamebeba Jeneza la aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Marehemu Salum Amour Mtondoo katika Msikiti kwa ajili ya Kumsalia.Marehemu alifariki hapo jana katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohd Shein wakatikati akijitayarisha pamoja na viongozi mbalimbali kwa ajili ya Kumsalia marehemu Salum Amour Mtondoo,kulia kwake ni Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamadi na kushoto yake anaejitengeneza kanzu yake ni Mufti mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Kabi.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Sheikh Ali Mohd Shein wakatikati akiwa pamoja na waislamu wengine katika dua ya kumuombea aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Marehemu Salum Amour Mtondoo katika msikiti wa Bububu.Kulia kwake ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamadi na kushoto yake ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Kabi na wambele alieshika maiki ni Msomji wa Dua hio Sheikh Halfan.
 
 Waheshimiwa mbalimbali pamoja na Wananchi waliohudhuria katika kumuambea Dua aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Marehemu Salum Amour Mtondoo hapo katika Msikiti Mkuu wa Bububu Mjini Zanzibar.
Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar Kabi  mwenye Maik akiomba Dua kwa ajili ya kumuambea aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Marehemu Salum Amour Mtondoo hapo katika Msikiti Mkuu wa Bububu Mjini Zanzibar.kulia kwake ni Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein na mwengine ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamadi.na kushoto ya sheikh ni Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi na mwengine ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Amer Kificho.
 Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhili Soraga akitoa Mawaidha katika mazishi ya aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Zanzibar Marehemu Salum Amour Mtondoo huko Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohd Shein akiongoza wanananchi mbalimbali katika mazishi ya  aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Zanzibar.Mazishi hayo yaliofanyika huko kijijini kwao Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja.
 Spikawa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho akitoa hotuba ya Shukrani kwa Viongozi na Wananchi mbalimbali waliohudhuria katika Mazishi ya aliyekua Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Marehemu Salum Amour Mtondoo aliezikwa huko kijijini kwao Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja.
PICHA ZOTE NA YUSSUF SIMAI MAELEZO ZANZIBAR.16/03/2012.
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar 16/03/2012

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed
Shein leo ameongoza mamia ya wananchi wa Zanzibar katika mazishi ya
aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Bububu (CCM) Salum Amour Mtondoo
yaliyofanyika katika kijiji cha Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Katika Mazishi hayo ambayo pia yalihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa kitaifa
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akiwamo Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim
Seif Shariff Hamad, Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd na Spika wa
Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho pamoja na Rais mstaafu Ali Hassan
Mwinyi yalitanguliwa na sala iliyofanyika katika Msikiti wa Bumbwini Misufini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mohammed
kwa niaba ya Serikali ilitoa hisia zake za kuguswa na msiba huo na kuwaomba
wananchi wa Jimbo la Bububu na wanafamilia kwa ujumla kuwa wastahamilivu
katika kipindi hiki kigumu.

Aidha Waziri Aboud amesema kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano na
wanafamilia katika kipindi hiki sambamba na kutoa ubani kwa ajili ya wanafamilia
hao ikiwa ni njia ya kuwafariji.

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai amesema kifo cha Mwakilishi
huyo ni pigo kwa wananchi wa Zanzibar,Jimbo la Bububu na Baraza la
Wawakilishi kutokana na utendaji kazi alioukuwa nao.

Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameri Kificho kwa upande wake ametoa
shukrani kwa Viongozi na wananchi ambao walishirikiana nao tokea kipindi cha
kuumwa marehemu hadi kifo chake.

Spika Kificho amesema marehemu Mtondoo alikuwa ni mtu mtulivu na mwenye
mashirikiano makubwa kwa wenziwe na kuwataka wananchi wa Jimbo la
Bububu kumuomba Mungu ili wapate kiongozi bora kama marehemu.

Marehemu Salum Mtondoo ambaye amefariki dunia jana katika Hospitali Kuu ya
Mnazi Mmoja alikuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Jimbo la Bububu ,
kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar
uliofanyika Octoba, 2010.

Marehemu Mtondoo alizaliwa tarehe 14/ 12/ 1962 huko Bububu, Wilaya ya
Magharibi , Zanzibar ambapo alipata elimu yake ya msingi na Sekondari katika
Skuli ya Bububu kuanzia mwaka 1969 hadi mwaka 1979.

Aidha katika katika shughuli za kisiasa, Marehemu amewahi kushika nyadhifa
mbali mbali katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikiwemo Mjumbe wa Kamati ya
siasa ya Tawi na nafasi za ujumbe katika jumuiya ya wazazi Wilaya hadi Mkoa.

Marehemu Mtondoo nje ya siasa katika uhai wake aliwahi kufanya kazi ya
Usimamizi wa Kiwanda cha COTEX mnano mwaka 1983 hadi mwaka 1985 na
Baadae kufanyakazi za Ujenzi katika ushirika wa BBB 1986 hadi mwaka 1992.
Mbali ya kazi hizo, Marehemu aliwahi kufanyakazi za biashara kuazia mwaka
1992 hadi mwaka 2010.

Marehemu ambaye amefariki dunia kutokana na ugonjwa wa shindikizo la damu
ameacha wake watatu (Vizuka) na watoto 10.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Dk.Jakaya
Kikwete kufuatia msiba huo ametuma salamu za rambi rambi kupitia Naibu
Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai pamoja na viongozi mbali mbali wa
Bara na Visiwani.

Huyu ni Mwakilishi wa pili kufariki dunia kupitia Chama cha Mapinduzi ambapo
Mwakilishi wa kwanza kufariki alikuwa Marehemu Mussa Khamis Silima wa
Jimbo la Uzini kwa ajali ya gari ambaye pia alikuwa Mbunge wa kuchaguliwa
kupitia Baraza la Wawakilishi

Mwenyezi Mungu aiweke roho ya Marehemu mahali pema peponi. Amin.

Imetolewa na Maelezo Zanzibar 16/03/2012

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.