Skip to main content

Chadema Wamkaanga Mzee Mkapa Arumeru

WADAI ALIUZA NCHI AKIWA IKULU, CCM WAHAHA KUVUNJA MAKUNDI, NASSARI AAHIDI KUREJESHA ARDHI ILIYOPORWA

Waandishi Wetu, Arumeru, JOTO la kuwania ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki, mkoani Arusha linazidi kupanda. Jana Chadema kilimgeukia Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa ambaye aliongoza uzinduzi wa kampeni za CCM juzi kikidai kwamba kiongozi huyo hana uadilifu wa kushiriki kampeni za uchaguzi huo mdogo.

Madai hayo ya Chadema kwa Mkapa yalitolewa katika mikutano iliyofanyika katika Kata za Legaruki, Poli, Selunani na Sing’isi, siku moja baada ya Mwenyekiti huyo mstaafu wa CCM kusema chama hicho cha upinzani hakina sera zinazoweza kuwakomboa wana Arumeru na kuwataka wasimchague mgombea wake, Joshua Nassari.
Kadhalika, Mkapa katika mkutano huo ulifanyika kwenye Uwanja wa Ngaresero, Usa River, alimshambulia Mbunge wa Musoma Mjini (Chadema), Vicent Nyerere akisema katika kuishi na kufanya kazi na Hayati Mwalimu Julius Nyerere hakuwahi kusikia jina la Vicent likitajwa katika ukoo huo wa Baba wa Taifa.

Jana, mbunge huyo ambaye ni Meneja Mwenza wa kampeni za Chadema katika uchaguzi huo alimjia juu Mkapa akisema kiongozi huyo si mwadilifu akidai kwamba ndiye chanzo cha matatizo mengi yanayolikabili taifa kwa sasa.
 “Tuliwahi kusema kuhusu Mzee Mkapa na tukapata wito kwamba tumwache apumzike baada ya kustaafu lakini inavyoonekana hapendi kupumzika na badala yake amekuja hapa (Arumeru) na kuanza kutuchokonoa.
Mimi nasema huyu mzee siyo mwadilifu kwani alifanya madudu mengi alipokuwa Ikulu,” alisema Nyerere na kuongeza::
“Eti jana (juzi) aliwaahidi kwamba atashughulikia matatizo ya ardhi, kwani aliyesababisha matatizo haya yote ni nani?…. ni yeye. Halafu yeye sasa siyo Rais, siyo diwani wala mbunge, kwa hiyo hana uwezo wowote wa kutatua matatizo yenu, wala msidanganyike.”
Nyerere alidai kwamba utawala wa Mkapa ni mbaya kuliko mwingine uliowahi kutokea nchini kwani ulisababisha mauaji Kisiwani Pemba kiasi cha Watanzania wengine kugeuka wakimbizi baada ya kukimbilia eneo la Shimoni, Mombasa, Kenya.
Mbunge huyo wa Musoma Mjini alisema matatizo ya ajira nchini ni matokeo ya ubinafsishwaji wa viwanda vyote uliofanywa na Serikali ya Mkapa... “leo hii ukiwa mijini huwezi kujua nani ni kichaa na nani mzima, vijana wengi wanaokota makopo. Ni bingwa wa kuuza kila kitu, aliuza benki zote na aliuza viwanda vyote na sasa hivi tunavyozungumza viwanda vingi vimegeuzwa magodauni (maghala) ya kuhifadhia bidhaa za Wachina badala ya kuwa vitovu vya ajira kwa vijana wetu.”
Nyerere alidai pia kwamba Mkapa ni kiongozi pekee ambaye baada ya kukaa madarakani miaka 10, kisha kupata fursa ya kulipwa pensheni ambazo ataendelea kuzipata maisha yake yote, aliingiwa na tamaa ya mali, hivyo kujiuzia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira.
“Kama tusingetumia nguvu ya umma kuudai mgodi huo asingeurudisha, sasa mtu wa aina hiyo ana kitu gani cha kutuambia hapa Arumeru?... Kama kweli ana uadilifu, basi aje hapa kesho atujibu ili tumwambie madudu yake mengine aliyofanya akiwa Rais,” alidai Nyerere.
Kuhusu uhusiano wake na Baba wa Taifa, Nyerere alisema kimsingi yeye ni mwanafamilia kwani Baba yake, Mzee Kiboko Nyerere alikuwa ndugu wa damu wa Julius Nyerere na kwamba Mkapa si mwanafamilia hiyo hivyo hawezi kufahamu masuala ya familia yao.
Soma zaidi:http://www.mwananchi.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.