Skip to main content

Chadema Wamkaanga Mzee Mkapa Arumeru

WADAI ALIUZA NCHI AKIWA IKULU, CCM WAHAHA KUVUNJA MAKUNDI, NASSARI AAHIDI KUREJESHA ARDHI ILIYOPORWA

Waandishi Wetu, Arumeru, JOTO la kuwania ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki, mkoani Arusha linazidi kupanda. Jana Chadema kilimgeukia Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa ambaye aliongoza uzinduzi wa kampeni za CCM juzi kikidai kwamba kiongozi huyo hana uadilifu wa kushiriki kampeni za uchaguzi huo mdogo.

Madai hayo ya Chadema kwa Mkapa yalitolewa katika mikutano iliyofanyika katika Kata za Legaruki, Poli, Selunani na Sing’isi, siku moja baada ya Mwenyekiti huyo mstaafu wa CCM kusema chama hicho cha upinzani hakina sera zinazoweza kuwakomboa wana Arumeru na kuwataka wasimchague mgombea wake, Joshua Nassari.
Kadhalika, Mkapa katika mkutano huo ulifanyika kwenye Uwanja wa Ngaresero, Usa River, alimshambulia Mbunge wa Musoma Mjini (Chadema), Vicent Nyerere akisema katika kuishi na kufanya kazi na Hayati Mwalimu Julius Nyerere hakuwahi kusikia jina la Vicent likitajwa katika ukoo huo wa Baba wa Taifa.

Jana, mbunge huyo ambaye ni Meneja Mwenza wa kampeni za Chadema katika uchaguzi huo alimjia juu Mkapa akisema kiongozi huyo si mwadilifu akidai kwamba ndiye chanzo cha matatizo mengi yanayolikabili taifa kwa sasa.
 “Tuliwahi kusema kuhusu Mzee Mkapa na tukapata wito kwamba tumwache apumzike baada ya kustaafu lakini inavyoonekana hapendi kupumzika na badala yake amekuja hapa (Arumeru) na kuanza kutuchokonoa.
Mimi nasema huyu mzee siyo mwadilifu kwani alifanya madudu mengi alipokuwa Ikulu,” alisema Nyerere na kuongeza::
“Eti jana (juzi) aliwaahidi kwamba atashughulikia matatizo ya ardhi, kwani aliyesababisha matatizo haya yote ni nani?…. ni yeye. Halafu yeye sasa siyo Rais, siyo diwani wala mbunge, kwa hiyo hana uwezo wowote wa kutatua matatizo yenu, wala msidanganyike.”
Nyerere alidai kwamba utawala wa Mkapa ni mbaya kuliko mwingine uliowahi kutokea nchini kwani ulisababisha mauaji Kisiwani Pemba kiasi cha Watanzania wengine kugeuka wakimbizi baada ya kukimbilia eneo la Shimoni, Mombasa, Kenya.
Mbunge huyo wa Musoma Mjini alisema matatizo ya ajira nchini ni matokeo ya ubinafsishwaji wa viwanda vyote uliofanywa na Serikali ya Mkapa... “leo hii ukiwa mijini huwezi kujua nani ni kichaa na nani mzima, vijana wengi wanaokota makopo. Ni bingwa wa kuuza kila kitu, aliuza benki zote na aliuza viwanda vyote na sasa hivi tunavyozungumza viwanda vingi vimegeuzwa magodauni (maghala) ya kuhifadhia bidhaa za Wachina badala ya kuwa vitovu vya ajira kwa vijana wetu.”
Nyerere alidai pia kwamba Mkapa ni kiongozi pekee ambaye baada ya kukaa madarakani miaka 10, kisha kupata fursa ya kulipwa pensheni ambazo ataendelea kuzipata maisha yake yote, aliingiwa na tamaa ya mali, hivyo kujiuzia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira.
“Kama tusingetumia nguvu ya umma kuudai mgodi huo asingeurudisha, sasa mtu wa aina hiyo ana kitu gani cha kutuambia hapa Arumeru?... Kama kweli ana uadilifu, basi aje hapa kesho atujibu ili tumwambie madudu yake mengine aliyofanya akiwa Rais,” alidai Nyerere.
Kuhusu uhusiano wake na Baba wa Taifa, Nyerere alisema kimsingi yeye ni mwanafamilia kwani Baba yake, Mzee Kiboko Nyerere alikuwa ndugu wa damu wa Julius Nyerere na kwamba Mkapa si mwanafamilia hiyo hivyo hawezi kufahamu masuala ya familia yao.
Soma zaidi:http://www.mwananchi.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...