Skip to main content

CUF Haitakufa: Asema Maalim Seif


Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad akihutubia katika mkutano wa hadhara kata ya Msambweni Tanga.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad akionesha tunzo maalum aliyokabidhiwa na Wazee wa Tanga kutoka na mchango wake kwa amani ya Zanzibar.Picha na Salmin Said-Ofisi ya Makamu Wa Kwanza Wa Rais Zanzibar
-----
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad amewataka wanachama na wapenzi wa Chama hicho katika Mkoa wa Tanga kuacha kuyumbishwa kwa mambo yasiyokuwa na msingi, na badala yake waungane katika kikiimarisha Chama hicho.

Amesema Chama hicho kiko imara na kitaendelea kuimarika kutokana na uwezo wa viongozi wake ambao wamepata sifa kubwa duniani kutokana na umahiri wao wa masuala ya uchumi na siasa.

Maalim Seif ametoa changamoto hiyo katika eneo la Msambweni Tanga wakati akiwahutubia maelfu ya wanachana na wapenzi wa Chama hicho waliojitokeza kwa ajili ya kumsikiliza na kujua mwelekeo wa Chama hicho baada ya kupata misukosuko ya kuwatimua baadhi ya viongozi wake.

Amesema Chama hicho siku zote kimekuwa mstari wa mbele katika kusimamia misingi ya haki na usawa kwa wananchi wote, na kwamba hakitosita kufanya hivyo kwa kuangalia maslahi ya mtu binafsi.

Maalim Seif amewapongeza wananchi wa Tanga kwa kumpa mapokezi makubwa wakati akipowasili katika uwanja wa ndege wa Tanga, hali inayodhirisha uhai wa chama hicho katika mkoa huo na maeneo mbali mbali Tanzania bara na Visiwani.

Amesema mapokezi yake ambayo yanathibitisha kuwa Tanga ni ngome ya CUF ambayo haiwezi kubomoka, na yale ya Prof. Lipumba yaliyofanyika Dar es Salaam tarehe 11/03/2012 yatakuwa dira ya kukiimarisha zaidi chama hicho na kasi hiyo itaendelezwa hadi uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Maalim Seif amekebehi kwa wale wanaodai kuwa CUF ni CCM ‘B’ kwamba “wana wivu wa kisiasa”, na wanaumwa na maendeleo ya chama hicho, na kuweka wazi kuwa CCM na CUF havijaungana na wala havitoungana ikizingatiwa kuwa kila chama kina sera zake.

Akiwasilisha salamu za mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba kwa wakaazi wa Mkoa wa Tanga amewataka kusimama imara na kujipanga katika kutoa maoni ya katiba mpya, ili kuhakikisha kuwa katiba inaweka wazi suala la maliasili kuwa rasilimali za Watanzania.

Amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na maliasili nyingi zikiwemo dhahabu, almasi, Tanzanite, copper na madini mengine kadhaa, lakini bado rasilimali hizo hazijawanufaisha wananchi kutokana na kutokuwepo utaratibu unaoeleweka juu ya mgawano wa rasilimali hizo.

Amesema Watanzania wanaweza kunufaika moja kwa moja na mgawano wa rasilimali hizo, hali ambayo itapunguza utegemezi wa chakula, mfumko wa bei na kupunguza umaskini kwa wananchi.

Katika salamu hizo Maalim Seif amesema Tanzania inahitaji uongozi wenye dira ya kuikomboa Tanzania kiuchumi, kwa kuweka mipango imara ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu na kuvutia wawekezaji wa sekta mbali mbali, jambo ambalo limekosekana kwa kipindi kirefu.

Katika mkutano huo Maalim Seif alikabidhiwa tunzo maalum kutoka kwa wazee wa Tanga kutokana na ujasiri wake wa kurejesha Amani Zanzibar.

Mkutano huo ulikwenda sambamba na kumtambulisha na kumnadi mgombea wa udiwani wa chama hicho kata ya msambweni Bw. Abrahman Hassan Omar, ambapo amewataka wanachama kumchagua mgombea huyo ili aweze kusaidia kuwatatulia kero zao.

Nae Mgombea udiwani wa CUF kata ya Msambweni Bw. Abrahman Hassan Omar amesema haombi uongozi ili apate kuwa bwana mkubwa bali kuwatumikia wananchi wakati wote.

Naibu Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chama hicho bw. Sheweji Mketo amewatahadharisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya tarehe 01/04/2012, huku akiwataka wananchi wasishawishike kwa chochote na waelewe kuwa siku hiyo itakuwa “April fool”.
 Na
 Hassan Hamad 
Ofisi ya Makamu Wa Kwanza Wa Rais Zanzibar

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.