Skip to main content

CUF Haitakufa: Asema Maalim Seif


Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad akihutubia katika mkutano wa hadhara kata ya Msambweni Tanga.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad akionesha tunzo maalum aliyokabidhiwa na Wazee wa Tanga kutoka na mchango wake kwa amani ya Zanzibar.Picha na Salmin Said-Ofisi ya Makamu Wa Kwanza Wa Rais Zanzibar
-----
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad amewataka wanachama na wapenzi wa Chama hicho katika Mkoa wa Tanga kuacha kuyumbishwa kwa mambo yasiyokuwa na msingi, na badala yake waungane katika kikiimarisha Chama hicho.

Amesema Chama hicho kiko imara na kitaendelea kuimarika kutokana na uwezo wa viongozi wake ambao wamepata sifa kubwa duniani kutokana na umahiri wao wa masuala ya uchumi na siasa.

Maalim Seif ametoa changamoto hiyo katika eneo la Msambweni Tanga wakati akiwahutubia maelfu ya wanachana na wapenzi wa Chama hicho waliojitokeza kwa ajili ya kumsikiliza na kujua mwelekeo wa Chama hicho baada ya kupata misukosuko ya kuwatimua baadhi ya viongozi wake.

Amesema Chama hicho siku zote kimekuwa mstari wa mbele katika kusimamia misingi ya haki na usawa kwa wananchi wote, na kwamba hakitosita kufanya hivyo kwa kuangalia maslahi ya mtu binafsi.

Maalim Seif amewapongeza wananchi wa Tanga kwa kumpa mapokezi makubwa wakati akipowasili katika uwanja wa ndege wa Tanga, hali inayodhirisha uhai wa chama hicho katika mkoa huo na maeneo mbali mbali Tanzania bara na Visiwani.

Amesema mapokezi yake ambayo yanathibitisha kuwa Tanga ni ngome ya CUF ambayo haiwezi kubomoka, na yale ya Prof. Lipumba yaliyofanyika Dar es Salaam tarehe 11/03/2012 yatakuwa dira ya kukiimarisha zaidi chama hicho na kasi hiyo itaendelezwa hadi uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Maalim Seif amekebehi kwa wale wanaodai kuwa CUF ni CCM ‘B’ kwamba “wana wivu wa kisiasa”, na wanaumwa na maendeleo ya chama hicho, na kuweka wazi kuwa CCM na CUF havijaungana na wala havitoungana ikizingatiwa kuwa kila chama kina sera zake.

Akiwasilisha salamu za mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba kwa wakaazi wa Mkoa wa Tanga amewataka kusimama imara na kujipanga katika kutoa maoni ya katiba mpya, ili kuhakikisha kuwa katiba inaweka wazi suala la maliasili kuwa rasilimali za Watanzania.

Amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na maliasili nyingi zikiwemo dhahabu, almasi, Tanzanite, copper na madini mengine kadhaa, lakini bado rasilimali hizo hazijawanufaisha wananchi kutokana na kutokuwepo utaratibu unaoeleweka juu ya mgawano wa rasilimali hizo.

Amesema Watanzania wanaweza kunufaika moja kwa moja na mgawano wa rasilimali hizo, hali ambayo itapunguza utegemezi wa chakula, mfumko wa bei na kupunguza umaskini kwa wananchi.

Katika salamu hizo Maalim Seif amesema Tanzania inahitaji uongozi wenye dira ya kuikomboa Tanzania kiuchumi, kwa kuweka mipango imara ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu na kuvutia wawekezaji wa sekta mbali mbali, jambo ambalo limekosekana kwa kipindi kirefu.

Katika mkutano huo Maalim Seif alikabidhiwa tunzo maalum kutoka kwa wazee wa Tanga kutokana na ujasiri wake wa kurejesha Amani Zanzibar.

Mkutano huo ulikwenda sambamba na kumtambulisha na kumnadi mgombea wa udiwani wa chama hicho kata ya msambweni Bw. Abrahman Hassan Omar, ambapo amewataka wanachama kumchagua mgombea huyo ili aweze kusaidia kuwatatulia kero zao.

Nae Mgombea udiwani wa CUF kata ya Msambweni Bw. Abrahman Hassan Omar amesema haombi uongozi ili apate kuwa bwana mkubwa bali kuwatumikia wananchi wakati wote.

Naibu Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chama hicho bw. Sheweji Mketo amewatahadharisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya tarehe 01/04/2012, huku akiwataka wananchi wasishawishike kwa chochote na waelewe kuwa siku hiyo itakuwa “April fool”.
 Na
 Hassan Hamad 
Ofisi ya Makamu Wa Kwanza Wa Rais Zanzibar

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...