Skip to main content

Maalim Seif Atembelea Vyombo Vya Habari




Khadija Khamis-Maelezo Zanzibar 12/03/2012
Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad amesema changamoto zinazotokea katika utendaji kazi katika Taasisi mbali mbali ni chachu katika kuleta maendeleo na kujikwamua pale tulipofika.
Amesema bila ya kuwa na changamoto maendeleo yataendelea kusuasua kwani kutakuwa hakuna hatua itakayopigwa mbele katika kuleta mafanikio.
Maalim Seif aliyaeleza hayo leo wakati akizungumza na uongozi wa Vyombo vya Habari vya Serikali ikiwemo Idara ya Habari Maelezo,Shirika la Utangazaji Zanzibar ZBC na Gazeti la Zanzibar ikiwa ni mfululizo wa kutembelea Idara za Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo.
Amesema vyombo vya habari ndio kiungo kikubwa kati ya wananchi na Serikali hivyo ni vyema kufanya kazi kwa uadilifu na kuweza kukabiliana na vikwazo ambavyo vinaweza kurudisha nyuma juhudi mbali mbali zinazochukuliwa na wananchi na hata Serikali.
Akizungumzia juu ya mafunzo kwa wanahabari, Maalim Seif alizitaka taasisi hizo kuwa na mpango mzuri wa kuwapeleka waandishi wa habari masomoni na katika mafunzo mengine ili waweze kukabiliana na kasi ya maendeleo ya teknolojia ambayo kwa sasa inakwenda kwa kasi kubwa.
Amesema masomo humjengea uwezo mwana habari wa kuweza kutumia kifaa chochote na kuweza kuibua mambo kadha ikiwemo uwezo wa kumkabili mtu yeyote bila ya woga au wasi wasi.
Amewataka waandishi wa habari katika Idara hiyo kuendelea kuwa wabunifu katika uandishi na kuandika habari zilizofanyiwa utafiti wa kina bila ya woga wowote
Maalim Seif alisisitiza haja ya kuwa na vifaa vya kisasa vinavyokwenda na wakati ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi , haraka na kwa wepesi zaidi.
Mapema Makamu wa Kwanza wa Rais aliipongeza Idara ya Habari kwa utendaji wake hasa kwa vile inatoa huduma ndani na nje ya nchi na kuishauri kuanza kupeleka taarifa zake katika vituo vyengine vya kigeni kama BBC,AFP CNN na REUTERS ili kuweza kutumia taarifa hizo na kuitangaza Zanzibar.
Akizungumzia suala la mishahara alisema kuwa viwango vya mshahara kwa wafanyakazi wa Vyombo vya habari ni vidogo kulingana na hali halisi na kupendekeza viwango hivyo kubadilishwa kulingana na wakati uliopo.
“Binadamu ni binadamu anaangalia maslahi yake tukisema uzalendo tu wengi watashindwa”alisema Maalim Seif
Katika Ziara hiyo Maalim Seif alitembelea Idara ya Habari Maelezo,Shirika la Magazeti ya Serikali,Shirika la Utangazaji la Zanzibar ZBC pamoja na maeneo ya Mitambo ya kurushia matangazo ya Shirika hilo.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...