Skip to main content

Balozi Seif Akutana na Ujumbe wa Kampuni ya Ujenzi wa Reli Nchini China {CRCG}


Na Othman Khamis Ame
Jamuhuri ya Watu wa China itaendelea kuwa Mshirika mkubwa wa Zanzibar katika harakati za Uimarishaji wa Maendeleo ya Kiuchumi Kibiashara, Miundombinu na Ustawi wa jamii.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema hayo hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar wakati alipofanya mazungumzo na Ujumbe wa Kampuni ya Ujenzi wa Reli Nchini China
{CRCG} ukiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni hiyo Bwana Liu Rongyao.

Balozi Seif alisema jamii imeshuhudia juhudi za China zinavyozidi kuongezeka katika kuona Zanzibar inajikwamua katika wimbi la umasikini kupitia kasi za uimarishaji miundo mbinu.

Aliyapongeza Makampuni mbali mbali ya China yanayotowa huduma zake hapa Zanzibar hasa yale ya Ujenzi ambayo kwa kiasi kikubwa yanaendelea kuchangia mabadiliko ya haiba ya Mji wa Zanzibar katika kipindi kifupi.

Alisisitiza kwamba ukamini wao katika kutoa huduma hizo ndio unaopelekea kuchaguliwa baada ya kushinda tenda dhidi ya Makampuni mengine Duniani na zaidi Barani Afrika.

“ Ujenzi wa baadhi ya Majengo ya Taasisi za Serikali , Mashirika ya Umma na hata miradi ya Jamii ni ushahidi uliowazi wa juhudi za Makampuni hayo”. Alisisitiza Balozi Seif.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyahakikishia Makampuni yote yanayotowa huduma hapa Zanzibar kwamba Serikali itashirikiana nayo kwa lengo la kuhakikisha yanakamilisha miradi yao kwa wakati uliopangwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni hiyo ya Ujenzi wa Reli Nchini China Bwa Liu Rongyao alisema kwamba Ujumbe wao upo Nchini kukagua Miradi ya Ujenzi inayosimamiwa na Kampuni hiyo ikiwemo ile ya Makaazi ya Nyumba za Viongozi na Ofisi za Serikali .

Ujenzi huo unafanywa kwa njia ya Mkopo kutoka Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China.
Mapema asubuhi Balozi Seif alikutana na Ujumbe wa Jumuiya inayojishughulisha na Miradi ya Maendeleo ya Kijamii kutoka Nchini Marekani ya Rosenthall Group.

Mwakilishi wa Jumuiya hiyo Bwana Robert Rosenthall alimueleza Balozi Seif kwamba Taasisi yao inaangalia taratibu za namna gani wanaweza kuelekeza nguvu zao katika Miradi ya Kijamii ndani ya Bara la Afrika.

Bw. Robert alisema mbali ya ujenzi wa nyumba katika kipindi kifupi unaofanywa na Taasisi yao lakini pia hutoa Taaluma ya huduma ya kwanza na Biashara mafunzo ambayo huchukua takriban Wanafunzi 150.

Naye Balozi Seif aliuomba Ujumbe huo kuangalia zaidi maeneo ambayo wanaweza kuwekeza hapa Zanzibar kwa nia ya kusaidia Uchumi wa Taifa.

Balozi Seif alisema yapo maeneo mengi yaliyopewa kipau mbele katika kuongeza kasi ya maendeleo akiyataja kuwa ni pamoja na Utalii, Kilimo, Huduma za Umme na Miundo mbinu.

Wakati huo huo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikuwa na Maungumzo na Balozi wa Shirikisho la Ujerumani Nchini Tanzania Bwana Klaus Peter Brandes.

Bwana Peter alifika Ofisini kwa Balozi Seif Vuga Mjini Zanzibar kumtambulisha rasmi Balozi Mdogo wa Shirikisho la Ujerumani atakayefanya kazi hapa Zanzibar Bwana Hans Dieter Allgaier.

Balozi Seif amemuahidi Bwana Allgaier kwamba Serikali itajitahidi kumpa mashirikiano zaidi ili kuona jukumu alilokabidhiwa na Nchi yake linafikiwa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Jumuiya inayojishughulisha na Miradi ya Maendeleo ya Kijamii kutoka Nchini Marekani ya Rosenthall Group pamoja na Washirika wao hapa Tanzania

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...