Skip to main content

BARAZA LA MJI MPANDA LARIDHIA BIL 14.6 YA BAJETI YA HALMASHAURI



BARAZA la madiwani la halmashauri ya mji Mpanda katika mkoa wa Katavi limepitisha mapendekezo ya bajeti ya hamashauri hiyo kwa kipindi cha mwaka 2012/2013 kwa ajili ya shughuli za maendeleo
Mwandishi wa mtandao huu kutoka Mpanda mkoani Katavi Willy Sumia anaripoti kuwa baraza hilo lilioketi leo Machi 9, 2012 limekubali kuyapitisha makadirio na makisio ya bajeti ya halmashauri hiyo ambapo mweka hazina wa Halmashauri hiyo Tatu Kisori amesema katika kipindi cha 2012/13 halmashauri imepanga kukusanya kiasi cha shilingi 606,847,000 kutoka katika vyanzo vya ndani ambapo pia halmashauri yake inatarajia kupokea ruzuku toka serikali kuu kiasi cha shilingi 6,441,517,240.
Amesema katika ruzuku ya serikali kiasi cha shilingi 5,338,014,240/= ni malipo ya mishahara kwa watumishi wa kada mbali mbali na shilingi 1,103,503,000/= ni za matumizi ya kawaida na kufafanua kuwa katika bajeti hiyo mishahara ni ongezeko la asilimia 20 kutoka shilingi 4,265,057,000/= hadi 5,338,014,240/=
Akizungumzia miradi ya maendeleo mweka hazina huyo alisema katika bajeti ya maendeleo halmashauri yake inatarajia kutumia shilingi 3,870,010,627/= kutoka serikali kuu, katika fedha hizo miradi ya maji imepewa kipaumbele kikubwa kwa kutengewa asilimia 34 ambayo ni shilingi 1,300,288,600/= ikifuatiwa na idara ya utawala kwa asilimia 26 sawa na shilingi 1,027,733,000/= pamoja na elimu ya sekondari iliyopewa shilingi 614,474,000/= sawa na asilimia 16.
Tatu Kisori pia amewasilisha bajeti ndogo ya maombi maalum ya nje ya ukomo wa bajeti kutokana na baadhi ya shughuli muhimu kushindwa kuingia katika bajeti kutokana na viwango vidogo vya bajeti vilivyowekwa na TAMISEMI na hivyo kuathiri bajeti kushindwa kuingizwa vitu muhimu ili kufikia malengo na kuondoa kero zilizoko katika jamii
Kisori amesema kutokana na hali hiyo halmashauri imelazimika kuomba fedha nje ya bajeti ya kawaida kiasi cha shilingi 3,558,000,000/= kwa ajili ya kununulia gari la kuzoa taka ngumu mjini Mpanda, kununulia gari la kunyonya maji machafu mjini, matengenezo ya gari la zimamoto na ujenzi wa sekondari ya Kata ya Kakese pamoja na kuweka miundombinu ya umeme katika shule za sekondari zote.
Aidha baraza la madiwani la halmashauri ya mji Mpanda limeridhia na kupitisha makisio ya bajeti ya hamashauri hiyo katika kipindi cha Julai 2012 hadi juni 2013 kiasi cha shilingi 14,688,051,240/= ikiwa ni mapato ya ndani na ruzuku ya serikali kwa ajili ya maendeleo ya halmashauri ya Mji Mpanda
Awali akiwasilisha mapitio ya bajeti ya 2011/2012 Kisori amesema halmashauri yake ilipanga kukusanya kiasi cha shilingi 823,164,000/= kutoka katika vyanzo vya ndani na kuweza kukusanya kiasi cha shilingi 241,873,480/= katika kipindi cha Julai 2012 hadi januari 2012 sawa na asilimia 29.38 ya makisio ambapo kiasi hicho kimefikiwa kwa kutumia mawakala wa ukusanyaji wa ushuru.
Amesema katika kipindi cha bajeti 2011/12 halmashauri ilipanga kuingiza mapato ya shilingi 70,350,000/= kutokana na vyanzo vya mapato vilivyofutwa na kuweza kukusanya shilingi 42,028,500/= sawa na asilimia 60 ya makisio.
Katika hatua nyingine baraza hilo limetoa Baraka zote kwa shirika la nyumba la Taifa kuenza ujenzi wa majengo katika mji wa Mpanda baada ya kuridhia malipo ya shilingi milioni 100 ikiwa ni kwa ajili ya eneo la jingo la starehe maarufu kwa jina la jengo la Paradise eneo litakalojengwa gorofa nne kwa ajili ya matumizi ya kibenki, ofisi na maduka ya biashara
Aidha baraza hilo limepokea na kuridhia maombi ya mamlaka ya viwanja vya ndege nchini juu ya kuomba upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mpanda utakaopelekea kuhamishwa kwa baadhi ya wakazi wa eneo la Nsemulwa Uwanja wa ndege ili kupisha upanuzi huo.
Imeelezwa katika baraza hilo kuwa upanuzi huo taathiri baadhi ya wananchi watakaotakiwa kipisha upanuzi huo baada ya kulipwa fidia na mamlaka husika katika kipindi kifupi kijacho kwani ujenzi unatarajia kuanza katika kipindi kifupi kijacho.Source Francis Godwin.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...