Skip to main content

RAIS JAKAYA KIKWETE ASEMA ANATAKA KULIACHA TAIFA LIKIWA NA WATU WENYE AFYA NJEMA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua mkutano wa kujadili jinsi ya kuyaweka masuala ya kinywa na meno katika hatua ya awali ya kupata huduma. Jumla wa wajumbe kutoka nchi 18 wanahudhuria mkutano huo wa siku tatu unaofanyika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.
(PICHA NA IKULU)
NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
RAIS Jakaya Kikwete amesema kwamba serikali itafanya kila iwezavyo katika kupanua na kuendesha huduma za afya zilizobora na kisasa ili kuhakikisha taifa linakuwa la watu wenye afya njema kwa kuzuia na kutibu magonjwa mbalimbali katika kipindi cha uongozi wake.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Rais Kikwete mara baada ya kukabidhiwa kadi ,katiba na tuzo ya kukubali kuwa mwanachama wa Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania na Rais wa chama hicho, Rachel Mhaville katika hoteli ya Court yard jijini DaresSalaam.
“Sikutegemea kutokea kwa kitendo hiki. Ninachoweza kusema ninaomba mniamini nitakuwa mwanachama mzuri. Tutafanyakazi kwa pamoja ili kutimiza ndoto zenu hususan kuhakikisha mradi wa kituo cha Kigamboni cha magonjwa hayo unaanzishwa.
“Hili ni jukumu kwangu , kwani lengo langu ni kuliacha taifa likiwa lenye watu wenye afya njema,” alisema Rais Kikwete.
Aliongeza kuwa serikali yake inafanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha ujenzi wa Chuo Kikuu kipya cha Sayansi za Afya na Tiba eneo la Mlongazila unafanikiwa ili kiweze kufanya kazi kabla ya mwaka 2015.
Rais Kikwete alisema chuo hicho kitakuwa na shule mbalimbali za afya na tiba.
Akifungua mkutano wa mafunzo ya siku tatu ya kuweka hatua za awali za kupata huduma za kuzuia na kutibu magonjwa hayo, Rais Kikwete alisema bado kuna safari ndefu ya kuiwezesha sekta ya huduma hiyo kuwa na rasimali watu wa kutosha wakiwemo madaktari, wauuguzi na watumishi wengine wa eneo hilo.
Rais Kikwete aliongeza kuwa sekta hiyo ina upungufu wa madakatari ukilinganisha na idadi ya watu nchini wapatao milioni 43 .
Alizitaja takwimu za madaktari wa sekta hiyo nchini kuwa wapo 518 ambapo uwiano unaonesha kuwa 1: 120,000 (yaani daktari mmoja kwa wagonjwa 120,000) wakati kwa sheria za Shirika la Afya la Dunia(WHO) 1:7500 (yaani daktari mmoja anatakiwa kutibu wagonjwa 7500).
“Serikali itaendelea kujenga uwezo kwenye hospitali na kituo cha afya, lazima ziwe na vitengo vya huduma za kinywa na meno,” alisisitiza huku akiongeza kwamba itasaidia kuanzisha na kupanunua vilivyopo na itangalia ili iweze kuanzisha hata katika Chuo Kikuu cha Dodoma.
Alitoa changamoto kwa wadau wa sekta hiyo kuhakikisha kuwa huduma za magonjwa hayo zinapatiakana, kutolewa katika hatua za awali na kwa gharama nafuu.
Naye Rais wa chama hicho, Mhaville alisema aliitaka jamii kuacha kutembea na magonjwa hayo badala yake wafike hospitali ili kupata ushauri na tiba kwa kuwa magonjwa hayo yanazuilika.
Alisema changamoto iliyopo kwao ni kutoa elimu kwa jamii hususan kwenye maeneo ya vijijini.
Mhaville alisema mkutano huo utatengeneza mwongozo wa mamna ya kuyashughulikia magonjwa ya afya ya kinywa na meno, ambapo Rais alisema serikali inausubiri kwa hamu.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.