Kwa sababu hiyo, amepinga maoni ya baadhi ya wabunge wanaotaka ivunjwe na badala yake akasema kama kuna ushahidi wa kutosha dhidi ya vitendo vya rushwa, basi awajibike yeye.Kusoma zaidi bofya
Akizungumza na waandishi wa habari jumanne, Zitto alisema licha ya mkakati huo, katu hatarudi nyuma katika kutetea masilahi ya taifa kwa kuwa anaamini siku zote uongo hujitenga na ukweli.
“Mchango wa POAC katika Bunge na ustawi wa mashirika ya umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali na fedha za umma kutokana na umakini wake,” alisema Zitto na kuongeza:
“Tumefanya hivyo CHC, Kiwira na kwenye mashirika mengi. Kote huku uadilifu wa kamati hii haujawahi kuhojiwa. Zipo hoja pandikizi za kutaka POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi.”
“Kwa maoni yangu, POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi (Zitto) na siyo kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu.”
Comments