Skip to main content

KANGEZI: LENGO LETU NI KUUZA WACHEZAJI NJE


WAKATI baadhi ya timu zikihaha kusajili wachezaji wapya kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu, klabu ya African Lyon imeweka wazi kuwa, haina malengo ya kutwaa taji hilo kwa sababu halina thamani kwao. Hayo yameelezwa na mmoja wa wamiliki wa klabu , Rahim Kangezi
SWALI: Wewe ni mmoja kati ya wamiliki wa klabu ya African Lyon inayoshiriki michuano ya ligi kuu ya Tanzania na hivi karibuni mliwahi kumpeleka mshambuliaji Mrisho Ngasa kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa Marekani, hebu tueleze matokeo ya majaribio hayo?
JIBU: Ni kweli tulimpeleka Ngasa kufanya majaribio Marekani na alipata nafasi ya kucheza mechi ya kirafiki katika timu ya Seattle Sounders dhidi ya Manchester United, lakini viongozi wa timu ile ya Canada walishauri arudi nchini kwanza ili ajiweke sawa kiafya na kuwa fiti zaidi.
Japokuwa kwa sasa Ngasa amehama Azam na kujiunga na Simba, bado mipango hiyo ipo pale pale na muda wowote anaweza kuitwa tena Marekani, hilo halina mjadala.
Lengo letu ni kuona wachezaji wengi wa Tanzania wanapata nafasi ya kufanya majaribio nje ya nchi ili wapate nafasi ya kucheza soka ya kulipwa na kuingiza mapato mengi zaidi kutokana na soka. Hilo ndilo lengo hasa la African Lyon.
SWALI: Hivi karibuni mmemleta kocha mpya kutoka Argentina badala ya Jumanne Chale. Kwa nini mmeamua kufanya mabadiliko hayo katika benchi lenu la ufundi?
JIBU: Ni kweli tumeamua kumleta kocha mpya, Pablo Ignacio Velez kuchukua nafasi ya Jumanne Chale. Lengo letu kubwa ni kuongeza nguvu kwenye benchi letu la ufundi baada ya kubaini kuwepo kwa mapungufu mengi katika misimu miwili iliyopita.
Pamoja na kufanya mabadiliko hayo, tunamshukuru sana kocha wetu Jumanne kwa sababu amefanyakazi kubwa na nzuri katika kuinoa timu yetu ikiwa ni pamoja na kuiwezesha kubaki kwenye ligi kuu. Tuna hakika chini ya kocha wetu mpya, tutafanya vizuri zaidi msimu huu kwa sababu tunao wachezaji wengi wazuri na wenye vipaji.
Unajua lengo la timu yetu sio kutwaa ubingwa wa ligi kuu. Lengo letu ni kuibua vipaji vya vijana na kuwaendeleza kwa kuwatafutia timu za kwenda kucheza soka ya kulipwa nje ya nchi.
SWALI: Unadhani kwa kipindi cha mwaka mmoja, ambacho kocha huyo mpya atakuwa na timu, mtaweza kupata wachezaji wengi wa kuuza nje?
JIBU: Ninachoweza kusema ni kwamba tayari kazi hiyo imeshaanza kwa kuivunja timu yetu ya kikosi cha pili na kuiunda upya. Kazi hiyo itafanywa na kocha mpya kwa sababu moja ya majukumu yake ni kuibua vipaji vya vijana.
SWALI: Kwa muda mrefu umekuwa ukiupinga mkataba wa udhamini wa ligi kuu kati ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom kwa madai kuwa, zawadi wanazotoa kwa timu ni ndogo. Unadhani nini kifanyike ili kuuboresha mkataba huo?
JIBU: Hata wewe ukiutazama mkataba huo, utagundua kwamba una kasoro. Haiwezekani timu itumie gharama kubwa kusajili wachezaji kila mwaka, kuwalipa mishahara na posho muda wote wa ligi kisha timu bingwa inapata shilingi milioni 40.
Gharama ambazo klabu zinatumia kusajili wachezaji wapya ni kati ya sh. milioni 120 hadi 150. Haiingii akilini ni kwa nini TFF imekubali kuingia mkataba huu na Vodacom wakati fedha za zawadi ni ndogo. Ni vyema mkataba huo utazamwe upya.
Nashukuru kuona kuwa baadhi ya viongozi wenzangu wa timu za ligi kuu wameshaibaini kasoro hiyo na kuniunga mkono, hivyo tunatarajia kuundwa kwa kampuni ya ligi kutasaidia kufanyika kwa mabadiliko hayo.
SWALI: Kwa maana hiyo unataka kusema kwamba, uchache huu wa zawadi zinazotolewa na Vodacom ndio umewafanya msiwe na malengo ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu?
JIBU: Sera ya klabu yangu ni kuibua na kukuza vipaji vya vijana na kuwauza nje ndio sababu tumeingia mkataba na kocha huyu mpya, ambaye tunamlipa pesa nyingi kwa ajili ya kazi hiyo. Tukisema tusubiri pesa za Vodacom, ambazo hadi kuzipata kwake inachukua muda mrefu, hatuwezi kufika mbali.
Tuna hakika kwamba ujio wa kocha huyu utafungua ukurasa mpya kwa African Lyon kwa sababu tayari vijana wengi wameshaanza kujitokeza kwa ajili ya kufanyiwa majaribio na baada ya muda si mrefu tutakuwa na kikosi kikali cha timu ya pili.
SWALI: Usajili wenu unaonekana kufanyika kimya kimya. Je, tangu kuwasali kwa kocha huyu mpya, ameshawafanyia majaribio wachezaji wangapi na kupendekeza wasajiliwe?
JIBU: Amewahi kuwajaribu baadhi ya wachezaji nyota kama vile Chacha Marwa kutoka Yanga, lakini hakuvutiwa naye na anadhani wachezaji waliopo ni wazuri zaidi.
Wapo wachezaji wengine kadhaa, ambao tunatarajia kuwafanyia majaribio mwishoni mwa wiki hii wakati African Lyon itakapocheza na Yanga katika mechi ya kirafiki kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
SWALI: Kitu gani kingine kipya kilichojitokeza kwenye timu yenu?
JIBU: Tunatarajia kumtangaza mkurugenzi wetu mpya hivi karibuni. Mkurugenzi huyu ni mwanamke na tutamtangaza rasmi wakati wa mechi yetu dhidi ya Yanga.
SWALI: Katika kikosi chenu cha sasa, kuna wachezaji wa kigeni kutoka nje?
JIBU: Wapo wachezaji watatu, ambao bado mwalimu wetu anawafanyia majaribio. Nadhani kati ya leo na kesho atakuwa amemaliza kuwafanyia majaribio na kutoa ushauri kwetu kama wanafaa kusajiliwa au la.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...