Skip to main content

Dk Shein asisitiza wananchi kushiriki Sensa ya watu na makaazi


Na Rajab Mkasasba, Ikulu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, ameeleza kuwa matokeo ya sensa ndio yanayoipa Serikali taarifa halisi na ya kitaalamu juu ya idadi ya watu na taarifa nyengine muhimu katika kutayarisha mipango ya maendeleo.

Matokeo yake hutumika kutayarisha mipango ya maendeleo

Dk. Shein aliyasema hayo katika taarifa yake aliyoitoa kupitia vyombo vya habari kwa wananchi kuhusu umuhimu wa wananchi katika kushiriki kikamilifu katika zoezi la sensa ya watu na makaazi itakayofanyika tarehe 26 Agosti, mwaka huu.

Kwa matiki hiyo, Dk. Shein alieleza kuwa kujua idadi ya watu katika eneo fulani kunaiwezesha Serikali kukadiria mahitaji ya huduma kwa wakaazi wake ambapo kinyume chake ni kutoa huduma pungufu kwa vile hakuna takwimu sahihi ya wakaazi hao.

Dk. Shein alisema kuwa si jambo la kufurahisha kusikia kuwa baadhi ya watu ambao wanawashawishi watu wengie wasishiriki katika zoezi hilo muhimu na kusisitiza kuwa wananchi wa Zanzibar sio wageni katika zoezi hilo kwani wameshashiriki kwa vipindi kadhaa na kupata mafanikio ambapo sensa ya mwanzo iliyowajumuisha watu wote ilifanyika mwaka 1948.

Comments