Skip to main content

Helikopta za Uganda zapotea


Ndege ya kijeshiHelikopta tatu za Uganda zikiwa njiani kuelekea Somalia zimepotea katika ardhi ya Kenya. Maafisa wa jeshi la Kenya wamesema leo kwamba helikopta nne ziliondoka Uganda na moja ikatuwa mjini Garissa.

Kwa mujibu wa msemaji wa jeshi la Kenya Bogita Ongeri, helikopta hizo zilipotea karibu na eneo la mlima Kenya, lakini rubani mmoja aliweza kuwasiliana nao, akiomba msaada.

Kwa mujibu wa msemaji huyo, mvua na hali mbaya ya hewa zilihujumu juhudi za uokozi na Ongeri akaongeza kwamba kundi la waokowaji limepelekwa sehemu hiyo ya ajali. 

Hata hivyo alisema hawafahamu kwa uhakika ni wapi hasa ajali hiyo ilitokea kwa sababu bado hali ya hewa ni mbaya. Helikopta hizo aina ya Mi-24 zinauwezo wa kubeba hadi abiria wanane.

Comments