Skip to main content

Maelfu Wamzika Atta Mills


Maelfu ya wananchi wa Ghana jijini Accra wamehudhuria mazishi ya kitaifa ya rais John Atta Mills aliyefariki ghafla mwezi Julai mwaka huu.

Baadhi ya wakuu wa nchi za Afrika wapatao kumi na wanane na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani Hillary Clinton walihudhuria mazishi hayo katika uwanja wa historia ya uhuru mjini Accra.

Mills aliyeugua saratani ya koo kwa muda mrefu amefariki ikiwa imebaki miezi mitano tu kabla ya kufanyika uchaguzi wa urais ambao angegombea tena nafasi hiyo.Mwandishi wa BBC mjini Accra anasema kifo chake kimewaunganisha Waghana katika majonzi. Anasema kifo hicho kilionekana kama jaribio kwa demokrasia changa ya nchi hiyo.

Mills aliyeanza kipindi cha miaka minne ya urais mwezi Januari mwaka 2009, amerithiwa na makamu wake rais John Dramani Mahama.

Ghana imepongezwa na jumuiya ya kimataifa kwa namna ambavyo imeshughulikia kipindi cha mpito katika taifa hilo linalofahamika kwa siasa zake za mgawanyiko.
Mazishi

''Leo giza nene limetanda katika anga ya Ghana, Afrika na kwa kweli ulimwengu mzima,'' Bwana Mahama aliuambia umati wa waombolezaji waliokuwa wakifuatilia mazishi hayo kupitia televisheni kubwa zilizowekwa uwanjani hapo.

''Rais Mills alikuwa muhimu sana katika yale ambayo tumekuwa hatuna katika siasa zetu, uzalendo, uvumilivu katika uongozi, uaminifu,'' alisema.

Mwandishi wa BBC Vera Kwakofi anasema watu walianza kukusanyika mapema alfajiri katika uwanja huo wakiwa wamevalia mavazi maalum ya maombolezo rangi nyeusi na nyekundu.Machifu wengi wa kimila walihudhuria wakiwa na ngoma zao wakipiga midundo ya ujumbe wa kuomboleza.Mbele ya wapiga ngoma wachezaji walichezesha mikono yao kwa namna ya ishara yenye maana maalum.

Wakati bendi ya jeshi ilipoingia na mwili wa marehemu uwanjani, ngoma, nyimbo za kusifu na za kishujaa zilisimama, mwandishi wetu anasema.

Filimbi za kuomboleza zilichezwa wakati rais Mahama alipowasha moto wa ishara ya kumbukumbu kwa marehemu, ambaye daima alitambulika kama ''Profesa au Mwalimu'', ikiashiria taaluma yake ya muda mrefu ya ualimu, na ''Asumdwoehene'', ikimaanisha mfalme wa amani katika lugha ya Twi.
Misururu ya foleni

Kwa muda wa siku mbili kabla maelfu ya wananchi wa Ghana walisafiri kuelekea Accra kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Mills.Baadhi walipanga foleni kwa saa kadhaa, wengi wao wakilia kwa uchungu, katika mistari ya urefu wa kama kilometa kumi nje ya jengo la Ikulu mjini Accra.

''Nimekuwa hapa kwa saa tatu, ili kumuona, lakini tutamkumbuka sana hapa,'' mwanamke mmoja aliiambia BBC.Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani Hillary Clinton aliwasili Ghana akitokea Nigeria siku ya Alhamisi kuhudhuria mazishi hayo, akikamilisha ziara yake ya siku kumi na moja ya nchi saba za Afrika.

Ikionekana kama mfano bora wa demokrasia katika eneo hilo la Afrika, ghana ilichaguliwa na rais wa Marekani Barack Obama katika ziara yake ya nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara mwaka 2009.

Mills aliyefariki akiwa na umri wa miaka 68 alikuwa ni mwanasiasa wa ngazi ya juu kwa miaka mingi.Kati ya mwaka 1997-2001 alikuwa makamu wa rais kwa aliyekuwa mtawala wa kijeshi Jerry Rawlings, lakini alijiweka mbali na kiongozi huyo.

Reactions::

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...