Skip to main content

Wananchi Aina Ya Maoni


Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Mstaafu Joseph Warioba akiongea na waandishi wa habari ofisi za Tume leo (Alhamisi, Agosti 9, 2012) kuhusu tathmini ya kazi ya Tume ya kukusanya maoni ya wananchi kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Katibu wa Tume Bw. Assaa Rashid.
 

Mwandishi wa Habari wa Radio Deutchelle Welle Bi. Hawra Shamte akiuliza swali katika mkutano kati ya waandishi wa habari na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Mstaafu Joseph Warioba. Mkutano huo ulifanyika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Mstaafu Joseph Warioba avitaka vyama vya siasa, asasi za kidini na wanaharakati kuacha kuwaelekeza wananchi aina ya maoni wanayopaswa kutoa kuhusu Katiba Mpya.

Jaji Warioba ameyasema hayo leo (Alhamisi, Agosti 9, 2012) katika mkutano wake na waandishi wa habari kuzungumzia tathmini ya mikutano ya awamu ya kwanza ya ukusanyaji wa maoni ya wananchi kuhusu Katiba Mpya katika mikoa minane ya Pwani, Dodoma, Manyara, Kagera, Shinyanga, Tanga, Kusini Unguja na Kusini Pemba.

“Sio wanasiasa tu, watu wote wakiwemo viongozi wa kidini, wanaharakati na taasisi zisizo za kiserikali ziache kuwalazimisha wananchi watoe maoni wanayotaka wao. Wananchi wawe huru kutoa maoni yao,” alisema na kuongeza kuwa vyama vya siasa, asasi zisizo za kiserikali ziatapata muda wa kuwasilisha maoni yao Tume.

“Mwananchi akitoa maoni yake binafsi, anakuwa ‘very articulate’ (anajieleza kwa ufasaha), lakini akielekezwa cha kusema, na ukamuomba ufafanuzi, anashindwa hata kueleza,” alisema Jaji Warioba katika mkutano huo uliohudhuriwa na pia na Katibu wa Tume hiyo, Bw. Assaa Rashid na Naibu Katibu Bw. Casmir Kyuki.

Kuhusu idadi ya mikutano iliyofanyika katika awamu ya kwanza, Mwenyekiti huyo amesema Tume yake imefanya mikutano 386 katika mikoa minane ya awamu ya kwanza kwa muda wa mwezi mmoja.

“Wastani wa wananchi 188,679 walihudhuria mikutano hiyo ya Tume. Hii ikiwa ni wastani wa watu 489 walifika kwenye kila Mkutano,” alisema na kuongeza kuwa Tume inaridhika na idadi hii na inaonesha wananchi wana mwamko wa kutoa maoni yao.

Kati ya waliohudhuria, Jaji Warioba alisema, wananchi 17,440 walitoa maoni yao kwa njia ya kuzungumza kwenye mikutano hiyo na jumla ya wananchi 29,180 walitoa maoni yao kwa njia ya maandishi na kuyawasilisha kwenye Mikutano ya Tume.

Jaji Warioba aliongeza kuwa Tume ilipokea maombi na kufanya mikutano nane na makundi maalum yakiwemo Taasisi za Dini na Vyombo vya Ulinzi na Usalama katika awamu ya kwanza. 

“Kimsingi, Tume imeridhika na kazi ya ukusanyaji wa maoni katika awamu ya kwanza kwani mikutano yote iliyopangwa na Tume imefanyika na imefanyika kwa amani na utulivu na wananchi walivumiliana katika kutoa maoni yao,” alisema.

Akizungumzia changamoto, Mwenyekiti huyo alisema katika mikutano ya Tume, wanawake bado hawajitokezi kwa wingi kutoa maoni yao mbele ya Tume ingawa wanahudhuria mikutano hiyo na kusisitiza kuwa Tume itaendelea kuwahamasisha kutoa maoni yao kwa uhuru na uwazi.

Kuhusu kuanza kwa awamu ya pili ya mikutano ya kukusanya maoni, Jaji Warioba alisema kazi ya kukusanya maoni kwa awamu ya pili inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 27 Agosti, 2012 na ratiba ya mikutano hiyo itatolewa na Tume hivi karibuni.

Akiongea katika mkutano huo, Naibu Katibu wa Tume hiyo, Bw. Kyuki alisema kuwa awamu ya pili ya kazi ya ukusanyaji maoni ya wananchi kuhusu Katiba Mpya itafanyika katika mikoa saba ambayo ni Mbeya, Morogoro, Lindi, Ruvuma, Kigoma, Katavi na Mwanza.Inatoka kwa Mjengwa.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...