Skip to main content

Maiti ya Meles yarudishwa nyumbani


Hayati Meles Zenawi aliyekuwa Waziri Mkuu wa EthiopiaMaelfu ya raia wa Ethiopia walikusanyika katikati mwa mji mkuu Addis Ababa jana, kuipokea maiti ya waziri mkuu wao, Meles Zenawi, ambaye alifariki katika hospital moja mjini Brussels, Ubelgiji.

Kulikuwa na msongamano mkubwa wa magari na watu kwenye barabara inayotoka uwanja wa ndege wa mjini Addis Ababa kuelekea nyumbani kwa marahemu Meles Zenawi, ambako maiti yake imewekwa ili wananchi waweze kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi wao.

Jeneza lenye mwili wa marehemu ambalo lilifunikwa na bendera ya taifa lilisindikizwa na bendi ya jeshi, huku wakiwepo pia wanasiasa, maafisa wakuu wa jeshi, wanadiplomasia na viongozi wa kidini. Mke wake Azeb Mesfin ambaye alijitandia kwa mavazi meusi ya msiba, aliisindikiza maiti ya mumewe ambayo kutoka Brussels ilisafirishwa na shirika la ndege la Ethiopia. Baadhi ya waombolezaji walibeba picha za Meles.

Mwisho wa minong'ono

Kifo cha waziri mkuu huyo ambacho kilitangazwa usiku wa kuamkia jana, kilimaliza uvumi wa miezi kadhaa kwamba kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 57 alikuwa na matatizo makubwa kiafya. Ethiopia imetangaza kuwa taifa liko katika kipindi cha maombolezo, lakini tarehe ya mazishi bado haijatangazwa.

Comments