Skip to main content

Jezi No 17 Yanga ndio hii Hapaaaa..

 


Sendeu akimkabidhi jezi Kavumbangu leo Jangwani

Na Prince Akbar
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Burundi, Didier Kavumbangu ametambulishwa rasmi leo katika klabu yake ya Yanga, makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam na kukabidhiwa jezi namba 21.
Akimtambulisha mchezaji huyo, Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema kwamba mchezaji huyo kutoka Atletico Olympique ya Burundi, amesaini mkataba wa miaka miwili.
Kavumbangu amefanya mazoezi leo na wenzake Uwanja wa Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Akizungumza baada ya kutambulishwa kwenye mkutano huo, Didier alisema anashukuru kutua Yanga, kwa sababu ni timu ambayo amekuwa akiisikia muda mrefu tangu akiwa mdogo na atajitahidi kufanya vizuri, kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.
“Nimefurahi kuja Yanga, nimefurahia mapokezi mazuri, na mimi naahidi nitafanya vizuri kuwafurahisha mashabiki,”alisema Kavumbangu.
Katika kikao hicho pia, mshambuliaji wa Yanga, Said Bahanuzi alikanusha uvumi kwamba amesaini Simba. “Nina mkataba wa miaka miwili na Yanga, hizo habari ni uzushi, mimi mchezaji wa Yanga,”alisema.
Yanga, ambao ni mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, walianza maandalizi yao ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana na Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Mbelgiji Tom Saintefiet aliwataja wachezaji ambao hawajaanza mazoezi ni Hamisi Kiiza, ambaye ameitwa timu ya taifa ya Uganda, The Cranes, Ibrahim Job na David Luhende ambao bado wapo kwao Mwanza, wakati Juma Abdul bado ni majeruhi.
Tom alisema wachezaji wengine waliokosekana mazoezini jana ni wale ambao wapo timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes, Frank Damayo, Omega Seme na Simon Msuva.
Yanga ilitwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Jumamosi kwa kuifunga Azam FC mabao 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wafungaji Hamisi Kiiza ‘Diego Milito’ na Said Bahanuzi ‘Spider Man’.
Hilo lilikuwa taji la tano la michuano hiyo kwa Yanga kihistoria, baada ya awali kutwaa mataji ya Kombe hilo katika miaka ya 1975 Zanzibar, 1993, 1999 Uganda na 2011 Dar es Salaam na mara zote hizo, ikiwa chini ya makocha wa kigeni.
Mwaka 1975 Yanga ilibeba Kombe hilo, ikiwa chini ya kocha kutoka Jamhuri ya Kodemokrasia ya Kongo (DRC), Tambwe Leya (sasa marehemu), 1993 chini ya kocha kutoka Burundi, Nzoyisaba Tauzany pia marehemu, 1999 chini ya Raoul Shungu kutoka DRC na mwaka jana chini ya Mganda Sam Timbe.
Wiki hii ziliibuka habari kwamba, baada ya kuipa Yanga Kombe la Kagame,Tom ameomba kazi ya kufundisha timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, lakini mwenyewe alisema baadaye akizungumza na BIN ZUBEIRY kwamba tangu amejiunga na klabu hiyo mwezi uliopita hajawahi kuomba kazi sehemu nyingine yoyote.
Mtakatifu Tom alisema anashangazwa mno na habari hizo za kizushi, za kizandiki zenye kulenga kumchonganisha yeye na mwajiri wake, Yanga SC.
“Nakumbuka niliwahi kuomba kazi Chama cha Soka Kenya (KFF) kufundisha timu yao ya taifa (Harambee Strars), lakini ilikuwa ni muda mrefu sana hata kabla sijaomba kazi Yanga,”alisema.
Blog moja iliyowahi kuandika Iddi Kipingu anagombea Uenyekiti Yanga, wiki hii iliandika habari yenye kichwa kisemacho; “WIKI MOJA BAADA YA KUIPA UBINGWA: KOCHA WA YANGA TOM SAINTFIET ATUMA MAOMBI YA KUIFUNDISHA HARAMBEE STARS,”.
Akiizungumzia habari hiyo, Mtakatifu alisema; “Ni uongo, tangu nimesaini mkataba na Yanga, sijawahi kuomba kazi pengine popote,”alisema.
Sendeu katikati, kulia Kavumbagu kulia na Bahanuzi kushoto leo asubuhi .

Didier Kavumbangu


Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...