.
MCHEZAJI mpya wa Simba, Mrisho Ngassa, leo
amekabidhiwa jezi namba 16 atakayokuwa akiitumia
kwenye klabu yake msimu huu.
Ngassa alikabidhiwa jezi yake hiyo katika makao makuu ya
Simba Mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam na Makamu
Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange Kaburu.
Kaburu alisema Simba inamkaribisha Ngassa kwa moyo
mmoja na kwamba wapenzi wote wa Wekundu wa
Msimbazi wana imani kubwa naye kwani uwezo wake
mkubwa wa soka unafahamika ndani na nje ya nchi.
"Tunashukuru kwamba tumekidhi vigezo vyote
vilivyohitajika kwa ajili ya usajili wa mchezaji huyu.
Tumeingia naye mkataba wa mwaka mmoja baada ya
kumaliza muda wa mkopo wake kutoka Azam na ni imani
yetu kwamba ujio wa Ngasa utaimarisha zaidi timu kwani
yeye ni miongoni mwa wachezaji ambao Kocha Mkuu wa
Simba, Milovan Cirkovic, anawapenda," alisema.
Akizungumza katika tukio hilo, Ngassa alisema amefurahi
kusajiliwa na Simba kwani ni sawa na historia kujirudia,
akikumbusha kwamba baba yake mzazi, Khlfan Ngassa,
aliwahi kuwa mchezaji wa klabu katika miaka ya 1990.
Kabla ya mkutano huo na waandishi wa habari, Ngassa
alifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa Simba katika
ufukwe wa Coco, jijini Dar es Salaam ambako Simba
inaendelea na mazoezi yake chini ya makocha Amatre
Inatoka kwa mdau.
amekabidhiwa jezi namba 16 atakayokuwa akiitumia
kwenye klabu yake msimu huu.
Ngassa alikabidhiwa jezi yake hiyo katika makao makuu ya
Simba Mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam na Makamu
Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange Kaburu.
Kaburu alisema Simba inamkaribisha Ngassa kwa moyo
mmoja na kwamba wapenzi wote wa Wekundu wa
Msimbazi wana imani kubwa naye kwani uwezo wake
mkubwa wa soka unafahamika ndani na nje ya nchi.
"Tunashukuru kwamba tumekidhi vigezo vyote
vilivyohitajika kwa ajili ya usajili wa mchezaji huyu.
Tumeingia naye mkataba wa mwaka mmoja baada ya
kumaliza muda wa mkopo wake kutoka Azam na ni imani
yetu kwamba ujio wa Ngasa utaimarisha zaidi timu kwani
yeye ni miongoni mwa wachezaji ambao Kocha Mkuu wa
Simba, Milovan Cirkovic, anawapenda," alisema.
Akizungumza katika tukio hilo, Ngassa alisema amefurahi
kusajiliwa na Simba kwani ni sawa na historia kujirudia,
akikumbusha kwamba baba yake mzazi, Khlfan Ngassa,
aliwahi kuwa mchezaji wa klabu katika miaka ya 1990.
Kabla ya mkutano huo na waandishi wa habari, Ngassa
alifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa Simba katika
ufukwe wa Coco, jijini Dar es Salaam ambako Simba
inaendelea na mazoezi yake chini ya makocha Amatre
Inatoka kwa mdau.
Comments