Skip to main content

"Nitakuwa Wa Mwisho Kuishabikia Katiba Mpya" Manyerere




Nimejitahidi kutafakari ni kwa namna gani Katiba mpya itatuletea mabadiliko ya kweli tunayoyataka, nimekosa majibu - na sidhani kama nitayapata.
Fikra zangu zinanirejesha enzi za kudai Uhuru. Wapo walioamini kuwa kwa kupata Uhuru, taifa letu lingepiga hatua kubwa kimaendeleo. Wapo waliojiaminisha kuwa kwa kupata Uhuru, maana yake umasikini ungetoweka.Wengine wakauona Uhuru kama mwanga wa kutufikisha kwenye nchi ya kimaendeleo mithili ya Marekani na Ulaya. Bila shaka walikuwapo walioamini kuwa kwa kupata Uhuru, basi kila kitu kinachomfaa binadamu kingepatikana katika taifa letu.

Hizo zilikuwa njozi. Miaka 50 baada ya Uhuru, tuna makabwela wengi kupindukia. Idadi yao inaongezeka. Ile ahueni ya kuwapa Watanzania elimu ya bure, maji bure, huduma za afya bure, imetoweka. Mambo yanazidi kuwa magumu.
Ugumu huu umewafanya wengi waamini kuwa kwa kupata Katiba mpya, basi kila kitu kitakuwa kwenye mstari. Tunarejea tena kwenye njozi za Uhuru. Wanaamini kwa kupata Katiba mpya, watapata milo mitatu kwa siku, watasomesha watoto, watajenga nyumba, watanunua magari, watafanya kila linalomfaa mwanadamu ili aweze kuishi kwa sifa zitakazomtofautisha na wanyama wengine; na kwa kifupi ni kwamba Katiba mpya, mafisadi wote watayeyuka kama theluji.
Kwa nadharia hizi, naapa kwa dhati kabisa kwamba hata kama tutapata Katiba mpya, itakuwa kazi bure. Wakati fulani aliyekuwa Rais wa Ghana, Jerry Rawlings, alipata kuuliuzwa ni kwa namna gani ameweza kuifikisha nchi yake kwenye maendeleo ya kupigiwa mfano.
Rais Rawlings, akajibu kwa kujiamini kabisa kwamba ametumia sera za Tanzania na maandiko ya aliyekuwa Rais wa Tanzania, Julius Nyerere, kuifikisha Ghana hapo ilipofika. Akasifu maandiko na sera za Tanzania akisema zilikuwa zimebeba mafunzo maridhawa kwa taifa lolote la Afrika kuweza kuzitumia kwa mazingira yake na kujipatia maendeleo.
Huyo alikuwa Rawlings. Yupo mwingine. Huyu ni Rais Paul Kagame wa Rwanda. Kwa Kagame, Tanzania ni darasa tosha. Amekuwa muwazi kueleza mbinu alizozitumia kuifikisha Rwanda hapo ilipo; nyingi akiwa amezinakili kutoka kwetu. Nidhamu, utendaji kazi na kuyashusha maendeleo kwa wananchi, ni mambo aliyoyazingatia. Haishangazi kuiona Rwanda ikiitumia Oktoba 14 kama siku rasmi ya kumkumbuka Mwalimu Nyerere.
Si hao tu, bali yupo Rais Hugo Chavez wa Venezuela, ambaye kama ukiisema vibaya Tanzania kwa sera zake, anaweza kukuadhibu! Nimepata kuhudhuria Mkutano wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) katika jiji la Havana, Cuba. Rais Chavez alitumia muda mrefu kumsifu Mwalimu Nyerere na sera za Tanzania kwamba kama vikifuatwa, mataifa ya Kusini yatapiga hatua kubwa kimaendeleo. Chavez ni mmoja wa wafuasi mahiri wa siasa ya Ujamaa. Amehakikisha mali za umma zinabaki kuwa za umma. Zinawanufaisha wananchi wote. Anatumia fedha za umma kusambaza huduma za kijamii kwa wananchi wote bila ubaguzi. Ni mfuasi mkuu wa Mwalimu.
Waliofaidika kwa sera za Tanzania ni wengi mno. Siwezi kuwataja wote. Ninachojaribu kukisema hapa ni kwamba hata kabla ya Katiba mpya, Tanzania tumekuwa na sheria na sera nzuri sana. Tumepata bahati ya kuwa na maandiko mazuri na viongozi walioona mbali, lakini vyote tumevipuuza. Tumeviweka kando. Sasa tunalilia Katiba mpya kana kwamba itakuja na kitu cha ajabu sana.

Kama hatutabadilika na kuwa watu wa vitendo, hiyo Katiba mpya hata ikipambwa kwa maandishi ya dhahabu na almasi, na ikafukizwa maradhi ya karafuu; itakuwa kazi bure.
Katiba ya sasa ukiisoma hutaona kama ina dosari nyingi za kuwafanya wengine waisigine. Haina udhaifu huo. Katiba yetu imeeleza vema kabisa namna ya kulinda rasilimali za nchi yetu. Imeeleza dhima ya kila Mtanzania katika kulinda na kuhifadhi rasilimali asilia. Imeainisha haki ya kila Mtanzania kutendewa haki mbele ya vyombo vya utoaji haki. Imesema wananchi wote wako sawa mbele ya sheria.
Kutoka na Katiba, tuna sheria nyingi. Tuna sheria hadi za kuzuia uvutaji sigara katika hadhira-sheria ambayo haipo katika mataifa mengi duniani. Tuna sheria za kulinda na kuhifadhi mazingira. Sheria hizo zikatungiwa sheria ndogo ndogo zinazozuia kukata miti hovyo, kujisaidia maeneo yasiyoruhusiwa, kutotupa taka ovyo, na kadhalika.
Pamoja na utitiri wa sheria zote hizo, tujiulize, kitu gani kimetukwamisha hata tusiweze kusitekeleza? Juzi, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ametoa ripoti inayoonyesha namna Tanzania inavyotafunwa. Sheria za kuwabana wezi zipo, tena zipo sheria kali kama ile ya Uhujumu Uchumi. Kila mwaka CAG anatoa ripoti akiainisha majizi wanaolimaliza taifa. Anafichua njama zinazofanywa na viongozi na wafanyabiashara kuhakikisha Tanzania inasalia mifupa. Hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wahusika. Hawachukuliwi hatua si kwa sababu Katiba ni mbaya, au sheria hazipo, bali kwa sababu ya wanaopaswa kuifanya kazi hiyo kuwa nao ni sehemu ya tatizo.
Ndiyo maana najiuliza, hiyo Katiba mpya itakuja na upako gani utakaowafanya Watanzania hawa hawa, wa tabia hizi hizi, na wa uporaji rasilimali huu huu, wabadilike na kuwa watu tofauti? Silioni hilo.

Katiba yetu hakuna mahali inasema wageni ndiyo wawe wa kwanza kufaidi rasilimali za nchi. Haisemi wao ndiyo wafaidi samaki wetu maziwani na baharini, lakini leo yote haya yanafanyika huku umasikini ukiongezeka kwa wananchi. Kwenye sheria za nchi yetu ipo inayompa mamlaka rais kuidhinisha mtu anyongwe. Hii ndiyo adhabu kali kabisa katika nchi yetu. Wapo wanaoipiga vita kwa maelezo kwamba haisaidii kumaliza matatizo. Wanasema inakinzana na haki ya msingi ya binadamu ya kuishi.
Sasa kama hivyo ndivyo- kwamba sheria ya kuua ipo, lakini inatakiwa ifutwe- sheria dhidi ya wahujumu uchumi ipo, sheria ya kufilisi mali za mafisadi zipo, hiyo Katiba itakuja na jipya gani?
Ndiyo maana nasema Katiba ya kweli ya Watanzania inapaswa kuandikwa katika mioyo na utashi wao, na wala si ya kuandikwa kama hii tunayoililia sasa.
Tunapaswa kubadilika kifikra. Tunapaswa kuwajibika-kila mmoja kwa nafasi yake-tunapaswa kuwa watu wa vitendo zaidi badala ya blabla na porojo zisizokoma, tunapaswa kusimamia sheria na kanuni tunazojiwekea.

Tunaweza kuwa na Katiba nzuri sana, lakini bila kuwa na wasimamizi wa kweli wa Katiba hiyo, tutabaki kuwa kichekesho.
Katiba mpya na nzuri haitoshi kutufanya tushibe, haiwezi kuwasomesha bure watoto wetu, haiwezi kupunguza ajali za barabarani kama madereva wataendelea kubebwa, haiwezi kumaliza umasikini kama kila siku kazi yetu ni kuamkia vilabuni na kushinda kwenye michezo ya “pool”. Katiba mpya haiwezi kutufaa jambo kama wengi wetu tutakuwa tukisubiri kulishwa chakula na mtu mmoja katika familia ya watu 15.
Wala Katiba mpya haiwezi kutufaa lolote kama maono ya viongozi wetu ni kuwahamasisha vijana kukopeshwa bodaboda badala ya kuwapa matrekta na zana nyingine za kuwawezesha kuzalisha mali kwa njia za kisasa.

Katiba mpya haiwezi kutufaa kitu kama tutaendelea kuabudu ushirikiana na kuamini kuwa maendeleo ya mtu yanaletwa kwa imani za kijinga za kuwaua ndugu zetu albino na kuchukua viungo vyao. Hatuwezi kubadilika kimaendeleo kama tutabaki kuwa taifa la watu wanaoamini tunguli na matangazo ya waganga matapeli eti wanaosafisha nyota na kutufanya tupande vyeo kazini. Kama ingelikuwa kweli mtu akipata dawa hizo anapanda cheo, basi kampuni ingekuwa na mawaziri 50 au 100 kwa wakati mmoja!

Tuna rasilimali ya mabonde, wanyamapori, madini, maziwa, bahari, mito, ardhi isiyo na mfano; na ukwasi wa kila aina. Tunachohitaji si Katiba pekee, bali viongozi makini wa kuwafanya wananchi wafaidike na ukwasi huu. Kwangu mimi, suala la kuwabadili kwanza Watanzania kifikra ili waipende nchi yao, wapende kuwajibika ndiyo yangekuwa mambo la maana zaidi kwangu.

Tukiwa na Katiba mpya, lakini tukawa na kiongozi anayemzuia Waziri kupanua barabara eti kwa sababu kwa kufanya hivyo anawaudhi wapigakura, haki ya Mungu tutaendelea kuonekana kama taifa ya washirikina tu.

Mwisho, niseme kwamba Katiba “nzuri na tamu” haina maana kama uwajibikaji wa viongozi wetu na wananchi vitakosekana. Je, uwajibikaji utaletwa na maandiko tu; au kwa dhamira na utashi wa wenye nchi? Je, utaondoa dhambi katika jamii kwa kujenga makanisa au misikiti mingi? Au utapunguza dhambi kwa kuwabadili waumini kiroho? Unaweza kuwa na makanisa na misikiti mizuri sana, lakini bila kuvitumia kwa maudhui yake, itakuwa kazi bure. Yapo mataifa yasiyokuwa na Katiba iliyoandikwa, lakini yapo mbele kimaendeleo. Nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa Katiba mpya ndiyo suluhu ya madhila yote yanayotufika sasa.

manyerere@hotmail.com
0759488 955
CHANZO: GAZETI LA JAMHURI

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.