Skip to main content

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad Akutana na Balozi Wa China Nchini Tanzania


 Ujumbe wa ubalozi wa China ukiongozwa na Balozi wake nchini Tanzania Lou You Qing (kulia), uliofika nyumbani kwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad huko Mbweni kwa ajili ya kujitambulisha na kubadilishana mawazo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na balozi wa China nchini Tanzania Lou You Qing, wakati ujumbe wa ubalozi huo ulipofika nyumbani kwake Mbweni kwa ajili ya kujitambulisha na kubadilishana mawazo. Katikati ni mkalimani wa lugha ya Kichina na Kiingereza Fang Wang.Picha na Salmin Said-Ofisi Ya Makamu Wa Kwanza Wa Rais Zanzibar 
---
China imesema itaendelea kushirikiana na Zanzibar katika sekta mbali mbali za maendeleo zikiwemo elimu, afya, kilimo na utafiti.

Balozi wa China nchini Tanzania Bw. Lou You Qing ambaye aliongoza ujumbe wa ubalozi huo, ameeleza hayo alipokuwa na mazungumzo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.

Balozi Qing na ujumbe wake walifika nyumbani kwa Makamu wa Kwanza wa Rais huko Mbweni, nje kidogo ya mji wa Zanzibar, kwa ajili ya kujitambulisha rasmi na kubadilishana mawazo juu ya maeneo tofauti ambayo China na Zanzibar zinaweza kushirikiana.

Amesema China iko tayari kushirikiana na Zanzibar katika kuendeleza kilimo cha mpunga pamoja na ujenzi wa miundombinu ya maendeleo, ikiwa ni pamoja kuyaalika makampuni ya kichina kwa ajili ya kuangalia namna yanavyoweza kusaidia katika ujenzi wa bandari mpya ya kibiashara Zanzibar.

Balozi Qing amesema China na Zanzibar zina historia ya muda mrefu katika nyanja mbali mbali zikiwemo siasa na uchumi, na kutaka mashirikiano hayo yaendelezwe kwa maslahi ya pande hizo mbili.

Amefahamisha kuwa uhusiano huo wa kunufaishana, sana unaonekana kukua kwa kasi kubwa kutokana na kuwepo na mawasiliano ya karibu miongoni mwa wananchi wa pande hizo mbili, na kwamba hali hiyo itahamasisha kasi ya maendeleo hapa Zanzibar.

Amesifu juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha miundominu ya kiuchumi, sambamba na kudumisha hali ya amani, mambo ambayo ni muhimu katika kuchochea maendeleo.

Amesema hatua hizo muhimu, zinaweza kuisadia Zanzibar kupiga hatua kubwa za maendeleo ikizingatiwa kuwa inazo rasilimali muhimu zikiwemo historia, utamaduni, bahari na jiografia ya visiwa vya Zanzibar ambavyo ni muhimu katika kukuza sekta ya utalii.

Amebainisha kuwa kihistoria China ilikuwa nchi maskini, lakini imeweza kupiga hatua kubwa za maendeleo kutokana na mipango na mikakati imara iliyojiwekea ambapo Zanzibar inaweza kujifunza na kukuza uchumi wake.

Nae Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amesema Zanzibar inayo mengi ya kujifunza kutoka kwa marifiki zao wa China katika jitihada zake za kujikwamua kiuchumi.

Amesema hatua ya Serikali ya China kukubali kuwapeleka mawaziri na maofisa wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenda kujifunza nchini China ni muhimu katika kufikia malengo yake iliyojiwekea.

Maalim Seif amepongeza mchango wa Serikali ya China katika kukuza maendeleo ya Zanzibar ambapo nchi hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya sekta mbali mbali zikiwemo elimu, afya na Michezo.

Amesema msisitizo wa mashirikiano kwa sasa unapaswa kuekezwa katika sekta za viwanda vidogovidogo, kilimo, utafiti na utalii, ambapo China ina uzoefu mkubwa katika nyanja hizo.

Amesema Zanzibar ambayo inakabiliwa na tatizo la uhaba wa ardhi, inajipanga kuendeleza sekta hizo za kiuchumi hasa kilimo cha umwagiliaji ambacho kinaweza kuinufaisha Zanzibar na hatimaye kupunguza utegemezi wa chakula kutoka nchi nyengine.

Sambamba na hilo Maalim Seif amesema serikali inajipanga kutekeleza mpango wake wa kujenga bandari kubwa ya kibiashara katika eneo la Mpigaduri, na kuiomba China kuangalia uwezekano wa kusaidia utekelezaji wa mpango huo.

Amesema kufanikiwa kwa mpango huo, kutairejeshea Zanzibar hadhi yake ya kuwa kituo kikuu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki ambapo meli kubwa za mizigo na kitalii zitaweza kufunga gati na kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao bila usumbufu.

Amefahamisha kuwa inawezekana kwa Zanzibar kujikwamua kiuchumi, kwa kutumia uzoefu wa China ambayo katika kipindi cha miaka 40 iliyopita ilikuwa nchi maskini na sasa uchumi wake unaendelea kukua kwa kasi kubwa kuelekea kutawala uchumi wa dunia.
 
Na
Na Hassan Hamad
Ofisi Ya Makamu Wa Kwanza Wa Rais Zanzibar

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...