![]() |
| Warembo Miss Utalii Kinondoni msimu uliopita |
Shindano
la kumpata Binti wa Utalii Kinondoni 2011/2012(Miss Utalii Kinondoni
2011/2012 ngazi ya wilaya limepangwa kufanyika katika ukumbi wa kisasa
na Club ya kimataifa ya San Siro, iliyoko Shekilango Sinza.Shindano
hilo limepangwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 25 Mei 2012 na
kushirikisha mabinti 25 kutoka katika majimbo yote ya wilaya ya
Kinondoni.
Kwa
mujibu wa Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na mkurugenzi wa
Miss Tourism Tanzania Organisation wilaya ya Kinondoni Pius
Yalula,ambao ndio waratibu na waandaaji wa shindano hilo, washiriki
wote wanatarajia kuanza kambi ya mazoezi katika ukumbi huo siku ya
Jumatatu Mei 1,2012. Miss Utalii Kinondoni 2010/2011 Sophia Dioa ambaye
pia ni Miss Utalii Dar es Salaam 2010/2011 na Miss Utalii Tanzania
2010/2011.
Piusi
Yalula alibainisha kuwa ni mpango mkakati wa Miss Tourism Tanzania
organisation mwaka huu, wa kuwafuata watanzania hususani vijana katika
maeneo yao ya burudani,ili kuwahamasisha juu ya utalii wa ndani. Ndio
maana fainali za mwaka za Miss Utalii Kinondoni ,tumeamua kuzifanyia
katika Club ya Sunciro, ambako tunaamini kuwa vijana na watu wa rika
mbalimbali wanapenda kwenda katika kumbi na club za aina hiyo kwa ajili
ya burudani na mapumziko ya wikendi. Utafitin uliofanywa na kitengo
chetu cha masoko umebaini kuwa ili dhana ya utalii wa ndani iweze
kufanikiwa ni lazima tuanze na watu hususani vijana ambao tayali ni
wapenzi wa burudani na wako tayali kutumia sehemu ya pato lao kwaajili
ya burudani na mapumziko ya mwishoni mwa wiki. Tutatumia shindano hili
la Miss Utalii Kinondoni 2010/2012 kuwahamasisha wapenzi wa burudani,
vijana na watu wa rika zote kujenga tabia ya kwenda
kuembelea vivutio vya utalii nchini ,hususani vya wilaya ya kinondoni
na pia kuwaelimisha wao na jamii kuwa Utalii na Burudani kama zilivyo
burudani nyingine na ni fulsa nzuri ya mapumziko ya mwishoni mwa wiki,
tena wakati mwingine kwa garama ndogo,kwani Serikali na mamlaka ya
Hifadhi za Taifa (TANAPA) wameweka bei isiyo zidi shilingi 1500 kwa mtu
mzima na shilingi 500 kwa watoto.
Fomu
kwaajili ya kushiriki shindano hilo zinapatikana katika maeneo
mbalimbali jijini Dar es Salaam ikiwemo Sunsiro Club Shekilango, Zizzu
Fashion Victori,Sea Boys Magomeni,BM Saloon Kinondoni, Dar es Salaam
City Collage Kimara,Chicken Hut mlimani City, Angel Saoon Sinza,Coco
Beach OyterBay na katika ofisi za Miss Tourism Tanzania Organisation zilozoko Ilala Bungini na Kimara Dar es Salaam.
Pous
aliongeza kuwa fainali za mwaka huu za Binti/Miss Utalii kinondoni
2011/12 zitakuwa ni za kipekee kutikana na kamati ya maandalizi
kujipanga vilivyo ,ili kuhakikisha huwa taji la Miss/Binti Utalii Dar
es Salaam linabaki kinondoni na pia kuhakikisha tunachukua taji la
taifa la Miss /Binti Utalii Tanzania 2011/12 mwaka huu. Sifa za
kushiriki shindano la Miss /Binti utalii Tanzania ni pamoja na Elimu
isiyo pungua kidato cha sita au yenye kulingana nayo, uwezo wa
kuzungumza kiswahili fasaha,urefu wa angalau setimita 160 au zaidi,
raia wa tanzania, ngozi na rangi asili,jinsia halosi ya kike, umri usio
pungua miaka 18 wala kuzidi miaka 27 na awe ni mwenye tabia na mwenendo
,tabia njeama na mfano wa kuigwa katika jamii.
Asante,
Pius Yalula
Mkurugenzi Miss Utalii Kinondoni

Comments