Skip to main content

SIPO TAYARI KULA NA MAFISADI WANAOHAMIA CHADEMA TOKA CCM - DR SLAA


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk Wilbrod Slaa, amesema hayupo tayari kula sahani moja na watuhumiwa wa ufisadi watakaojiunga na chama hicho.
Amesema Chadema ipo makini katika kuwapokea wanachama na viongozi wanaotoka CCM, lakini haitakuwa rahisi kukigeuza chama hicho kuwa pango la mafisadi.
Alisema hayo wakati akimpokea aliyekuwa diwani wa kata ya Lugata katika wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza (CCM), Adrian Tizeba.
Tizeda alikihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Baada ya kutangaza kujiengua CCM, Tizeba alikabidhiwa kadi ya Chadema na Dk.Slaa ambaye alisema kwamba hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu baada ya kuwa wamemvua uanachama diwani wa Katoro kupitia chama hicho, aliyemtaja kwa jina moja la Gervas.
Akihutubia mkutano huo wa hadhara, Dk.Slaa alisema kwamba Chadema kiko makini katika kupokea wanachama kutoka CCM na kamwe hakitakubali kupokea mafisadi.
“Yapo maneno yanasemwa kuhusu wanaCCM kuhamia Chadema, lakini nataka niwaambie kwamba tuko makini, mimi Dk.Slaa siwezi kula sahani moja na mafisadi lazima tunajiridhisha kwanza kabla ya kumpokea mtu”alisema.
Tizeba anakuwa diwani wa tatu katika kipindi cha siku tatu kujiengua kutoka CCM na kujiunga na Chadema.
Siku tatu zilizopita aliyekuwa Diwani wa Kata ya Sombetini mkoani Arusha, Alphonce Mawazo alitangaza kukihama CCM, na juzi diwani wa kata ya Nyampulukano wilaya ya Sengerema, Hamisi Magwao alifuata nyayo hizo.
Tizeba ambaye ni kaka mkubwa wa Mbunge wa Buchosa, Dk.Charles Tizeba, alitangaza uamuzi wa kujiengua CCM jana jioni katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapa na kuhutubiwa na Katibu Mkuu wa Chadema Dk.Wilbroad Slaa na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.
Akitangaza kukihama CCM, Tizeba alisema amechoshwa na tabia za viongozi wa chama hicho, kushindwa kushughulikia matatizo ya msingi yanayowakabili wananchi.
Katika hatua nyingine, Dk.Slaa alitangaza azma ya chama chake kumshughulikia kisheria Mkuu wa Mkoa mpya wa Geita, Said Magalula, ambaye anadaiwa kushirikiana na wawekezaji wa mgodi wa GGM kuwanyanyasa wananchi ikiwa ni pamoja na kuwafyatulia risasi.
Alisema kwamba kama Mkuu huyo wa mkoa anataka kuwa salama katika mkoa wa Geita, hana budi kuwalinda wananchi dhidi ya wawekezaji wanaonyanyasa raia bila sababu za msingi.
Naye Lema alitumia mkutano huo kuzungumzia hukumu iliyotengua ushindi wake wa ubunge katika jimbo la Arusha Mjini akisema kuwa alihukumiwa kihuni.
Hata hivyo alidai kuwa kimsingi hukumu hiyo haijampunguzia chochote kwa sababu anaamini yeye bado ni Mbunge, isipokuwa amepumzishwa kwa muda tu na baadaye atarejea katika nafasi yake hiyo.
Kwa upande mwingine, wanachama 83 wa CCM tawi la Igalagalilo kata ya Kasungamile wilayani Sengerema walijiengua kutoka chama hicho na kujiunga Chadema.
Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya diwani wa kata ya Nyampulukano Hamis Mwagao, kukihama CCM na kutangaza kujiunga Chadema.
Katibu wa Chadema jimbo la Sengerema ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana (Taifa), Rafiki Rufunga alisema jinamizi la watu kujiunga na Chadema linatokana na serikali kushindwa kutatua kero zinazowakabili wananchi na ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo.
Alisema wananchama wa CCM tawi la Igalagalilo walijiunga Chadema April 13, mwaka huu wakati wa kurudisha fomu ya mgombea wa chama hicho katika uchaguzi mdogo wa mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho.
Miongoni mwa wanachama hao yumo Katibu wa Shina (balozi) Kusekwa Masheku na kamanda wa sungusungu Hamisi Nteminyanda.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. SÅ‚awomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...