Skip to main content

SIPO TAYARI KULA NA MAFISADI WANAOHAMIA CHADEMA TOKA CCM - DR SLAA


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk Wilbrod Slaa, amesema hayupo tayari kula sahani moja na watuhumiwa wa ufisadi watakaojiunga na chama hicho.
Amesema Chadema ipo makini katika kuwapokea wanachama na viongozi wanaotoka CCM, lakini haitakuwa rahisi kukigeuza chama hicho kuwa pango la mafisadi.
Alisema hayo wakati akimpokea aliyekuwa diwani wa kata ya Lugata katika wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza (CCM), Adrian Tizeba.
Tizeda alikihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Baada ya kutangaza kujiengua CCM, Tizeba alikabidhiwa kadi ya Chadema na Dk.Slaa ambaye alisema kwamba hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu baada ya kuwa wamemvua uanachama diwani wa Katoro kupitia chama hicho, aliyemtaja kwa jina moja la Gervas.
Akihutubia mkutano huo wa hadhara, Dk.Slaa alisema kwamba Chadema kiko makini katika kupokea wanachama kutoka CCM na kamwe hakitakubali kupokea mafisadi.
“Yapo maneno yanasemwa kuhusu wanaCCM kuhamia Chadema, lakini nataka niwaambie kwamba tuko makini, mimi Dk.Slaa siwezi kula sahani moja na mafisadi lazima tunajiridhisha kwanza kabla ya kumpokea mtu”alisema.
Tizeba anakuwa diwani wa tatu katika kipindi cha siku tatu kujiengua kutoka CCM na kujiunga na Chadema.
Siku tatu zilizopita aliyekuwa Diwani wa Kata ya Sombetini mkoani Arusha, Alphonce Mawazo alitangaza kukihama CCM, na juzi diwani wa kata ya Nyampulukano wilaya ya Sengerema, Hamisi Magwao alifuata nyayo hizo.
Tizeba ambaye ni kaka mkubwa wa Mbunge wa Buchosa, Dk.Charles Tizeba, alitangaza uamuzi wa kujiengua CCM jana jioni katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapa na kuhutubiwa na Katibu Mkuu wa Chadema Dk.Wilbroad Slaa na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.
Akitangaza kukihama CCM, Tizeba alisema amechoshwa na tabia za viongozi wa chama hicho, kushindwa kushughulikia matatizo ya msingi yanayowakabili wananchi.
Katika hatua nyingine, Dk.Slaa alitangaza azma ya chama chake kumshughulikia kisheria Mkuu wa Mkoa mpya wa Geita, Said Magalula, ambaye anadaiwa kushirikiana na wawekezaji wa mgodi wa GGM kuwanyanyasa wananchi ikiwa ni pamoja na kuwafyatulia risasi.
Alisema kwamba kama Mkuu huyo wa mkoa anataka kuwa salama katika mkoa wa Geita, hana budi kuwalinda wananchi dhidi ya wawekezaji wanaonyanyasa raia bila sababu za msingi.
Naye Lema alitumia mkutano huo kuzungumzia hukumu iliyotengua ushindi wake wa ubunge katika jimbo la Arusha Mjini akisema kuwa alihukumiwa kihuni.
Hata hivyo alidai kuwa kimsingi hukumu hiyo haijampunguzia chochote kwa sababu anaamini yeye bado ni Mbunge, isipokuwa amepumzishwa kwa muda tu na baadaye atarejea katika nafasi yake hiyo.
Kwa upande mwingine, wanachama 83 wa CCM tawi la Igalagalilo kata ya Kasungamile wilayani Sengerema walijiengua kutoka chama hicho na kujiunga Chadema.
Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya diwani wa kata ya Nyampulukano Hamis Mwagao, kukihama CCM na kutangaza kujiunga Chadema.
Katibu wa Chadema jimbo la Sengerema ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana (Taifa), Rafiki Rufunga alisema jinamizi la watu kujiunga na Chadema linatokana na serikali kushindwa kutatua kero zinazowakabili wananchi na ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo.
Alisema wananchama wa CCM tawi la Igalagalilo walijiunga Chadema April 13, mwaka huu wakati wa kurudisha fomu ya mgombea wa chama hicho katika uchaguzi mdogo wa mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho.
Miongoni mwa wanachama hao yumo Katibu wa Shina (balozi) Kusekwa Masheku na kamanda wa sungusungu Hamisi Nteminyanda.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.