Mwimbaji Nyota wa Bongo Fleva Nassib
Abdul a.k.a Diamond usiku wa Aprili 14,2012 ameibuka kidedea baada ya
kujinyakulia tuzo tatu katika tamasha la Utoaji Tuzo za Kili Music
Award 2012.
Diamond
ambaye mwaka 2010 aliibuka pia kidedea kwa kuzoa tuzo nyingi na mwaka
2011 kumpa nafasi 20% kwa kuzoa tuzo nyingi mwaka huu amenyakua tuzo ya
MTUNZI BORA WA MWAKA, MTUMBWIZAJI BORA WA KIUME na Video yake ya Mawazo
ikinyakua tuzo ya VIDEO BORA YA MWAKA.
Mbali na Diamond aliyebahatika kunyakua Tuzo mbili katika tuzo hizo ni msanii mwingine wa Bongo Fleva Suma Lee aliyenyakua tuzo za WIMBO BORA WA AFRO POP ambao alipata kupitia wimbo wa HAKUNAGA na Tuzo ya pili ni ya WIMBO BORA WA MWAKA.
Ambao pia ni HAKUNAGA.
Aidha msanii Chiopukizi wa Bongo Fleva, Omy Dimpoz nae ametamba baada ya kunyakua tuzo ya WIMBO BORA WA KUSHIRIKISHWA wa NAI NAI aliomshirikisha ALI KIBA na pia alitwaa tuzo ya MSANII BORA ANAECHIPUKIA kupitia wimbo wake huo huo wa NAI NAI.
Nae Roma Mkatoliki a.k.a Mpare wa milimani alikuwa katika kundi hilo la wasanii wenye tuzo mbili baada ya kupata tuzo ya WIMBO BORA WA HIP HOP wa MATHEMATICS na Tuzo ya MSANII BORA WA HIP HOP.
Mbali na Diamond aliyebahatika kunyakua Tuzo mbili katika tuzo hizo ni msanii mwingine wa Bongo Fleva Suma Lee aliyenyakua tuzo za WIMBO BORA WA AFRO POP ambao alipata kupitia wimbo wa HAKUNAGA na Tuzo ya pili ni ya WIMBO BORA WA MWAKA.
Ambao pia ni HAKUNAGA.
Aidha msanii Chiopukizi wa Bongo Fleva, Omy Dimpoz nae ametamba baada ya kunyakua tuzo ya WIMBO BORA WA KUSHIRIKISHWA wa NAI NAI aliomshirikisha ALI KIBA na pia alitwaa tuzo ya MSANII BORA ANAECHIPUKIA kupitia wimbo wake huo huo wa NAI NAI.
Nae Roma Mkatoliki a.k.a Mpare wa milimani alikuwa katika kundi hilo la wasanii wenye tuzo mbili baada ya kupata tuzo ya WIMBO BORA WA HIP HOP wa MATHEMATICS na Tuzo ya MSANII BORA WA HIP HOP.
Comments