Skip to main content

Tino Katika Harakati za Kipelelezi


MCHEZA filamu machachari wa Tanzania, Hissan Muya 'Tino' ameibuka na movi mpya kali inayokwenda kwa jina la CID.
Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Tino alisema filamu hiyo inahusu mambo ya upepelezi dhidi ya mtandao wa majambazi na wauaji.
Tino alisema filamu hiyo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho katika onyesho litakalofanyika kwenye ukumbi wa Business Park, ulioko Mikocheni, Dar es Salaam.
Alisema uzinduzi wa filamu hiyo utapambwa na burudani mbali mbali, zikiwemo muziki wa dansi na kizazi kipya.
Mcheza filamu huyo mwenye mvuto alisema, kwa sasa ameamua kuachana na filamu za mapenzi, badala yake atakuwa akicheza filamu za mapigano.
Alisema uamuzi wake huo umelenga kupiga hatua kubwa zaidi kimaendeleo katika fani hiyo baada ya kubaini kwamba, filamu za mapenzi hazina mvuto mkubwa kwa mashabiki.
Tino, ambaye amecheza filamu zaidi ya 20 alisema, mbali na filamu za mapigano, atakuwa akicheza filamu zenye mwelekeo wa kuielimisha jamii juu ya masuala mbali mbali.
"Kwa sasa watu wengi wamejikita kutengeneza na kucheza filamu za mapenzi na kusuahau mambo mengine muhimu yanayoigusa jamii, hasa ujambazi, magonjwa kama vile ukimwi na mengineyo,"alisema msanii huyo.
Aliitaja sababu nyingine iliyomfanya azitose filamu za mapenzi kuwa, ni baada ya kupata matatizo alipotengeneza filamu ya shoga.
Filamu hiyo ilikuwa ikielezea tabia ya ushoga katika jamii, lakini mamlaka zinazohusika ziliamua kuipiga marufuku kwa madai kwamba, ilikuwa inakiuka maadili ya kitanzania.
Hata hivyo, baada ya filamu hiyo kufanyiwa marekebisho, ilibadilishwa jina na kuitwa Shoga yangu. Tino hakufurahishwa na uamuzi huo kwa madai kuwa, ulipoteza maana halisi ya filamu hiyo.
“Filamu za mapenzi sasa kwangu basi, nataka kugeukia kwenye filamu za mapigano na zile zinazogusa maisha ya binadamu wa kawaida,” alisema Tino.
Tino amewashauri wasanii wengine kutojikita sana katika filamu za mapenzi kwa vile yapo matukio mengi yanayotokea katika jamii, ambayo yanapaswa kuandikiwa filamu.
Katika hatua nyingine, Tino ameanzisha shindano la Bongo Movie Star Search, linalotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Tino amesema ameamua kuanzisha shindano hilo kwa lengo la kuibua na kuviendeleza vipaji vya vijana, hasa wanaoishi mikoani.
Alisema wazo la kuanzisha shindano hilo lilitoka kwa marehemu Steven Kanumba na walikuwa wamepanga kulifanyiakazi kwa pamoja kabla ya mauti kumkuta.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...