Skip to main content

Tino Katika Harakati za Kipelelezi


MCHEZA filamu machachari wa Tanzania, Hissan Muya 'Tino' ameibuka na movi mpya kali inayokwenda kwa jina la CID.
Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Tino alisema filamu hiyo inahusu mambo ya upepelezi dhidi ya mtandao wa majambazi na wauaji.
Tino alisema filamu hiyo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho katika onyesho litakalofanyika kwenye ukumbi wa Business Park, ulioko Mikocheni, Dar es Salaam.
Alisema uzinduzi wa filamu hiyo utapambwa na burudani mbali mbali, zikiwemo muziki wa dansi na kizazi kipya.
Mcheza filamu huyo mwenye mvuto alisema, kwa sasa ameamua kuachana na filamu za mapenzi, badala yake atakuwa akicheza filamu za mapigano.
Alisema uamuzi wake huo umelenga kupiga hatua kubwa zaidi kimaendeleo katika fani hiyo baada ya kubaini kwamba, filamu za mapenzi hazina mvuto mkubwa kwa mashabiki.
Tino, ambaye amecheza filamu zaidi ya 20 alisema, mbali na filamu za mapigano, atakuwa akicheza filamu zenye mwelekeo wa kuielimisha jamii juu ya masuala mbali mbali.
"Kwa sasa watu wengi wamejikita kutengeneza na kucheza filamu za mapenzi na kusuahau mambo mengine muhimu yanayoigusa jamii, hasa ujambazi, magonjwa kama vile ukimwi na mengineyo,"alisema msanii huyo.
Aliitaja sababu nyingine iliyomfanya azitose filamu za mapenzi kuwa, ni baada ya kupata matatizo alipotengeneza filamu ya shoga.
Filamu hiyo ilikuwa ikielezea tabia ya ushoga katika jamii, lakini mamlaka zinazohusika ziliamua kuipiga marufuku kwa madai kwamba, ilikuwa inakiuka maadili ya kitanzania.
Hata hivyo, baada ya filamu hiyo kufanyiwa marekebisho, ilibadilishwa jina na kuitwa Shoga yangu. Tino hakufurahishwa na uamuzi huo kwa madai kuwa, ulipoteza maana halisi ya filamu hiyo.
“Filamu za mapenzi sasa kwangu basi, nataka kugeukia kwenye filamu za mapigano na zile zinazogusa maisha ya binadamu wa kawaida,” alisema Tino.
Tino amewashauri wasanii wengine kutojikita sana katika filamu za mapenzi kwa vile yapo matukio mengi yanayotokea katika jamii, ambayo yanapaswa kuandikiwa filamu.
Katika hatua nyingine, Tino ameanzisha shindano la Bongo Movie Star Search, linalotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Tino amesema ameamua kuanzisha shindano hilo kwa lengo la kuibua na kuviendeleza vipaji vya vijana, hasa wanaoishi mikoani.
Alisema wazo la kuanzisha shindano hilo lilitoka kwa marehemu Steven Kanumba na walikuwa wamepanga kulifanyiakazi kwa pamoja kabla ya mauti kumkuta.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.