Mahojiano na Mawassi Lahcen, Casablanca
Katika eneo la wazi lililoandaliwa na mapinduzi wa chemuchemu za
Uarabuni (Arab Spring), Waislamu wenye siasa kali wanaunda vikundi vipya
kadhaa kusukuma mbele ajenda yao.
Wanaounga mkono brigedi ya Libya inyojiita
Ansar al-Sharia wakipiga kaulimbiu za kidini wakiwa wameshikilia
bendera ya washirika wa al-Qaida kupinga maandamano ya umma dhidi ya
wanamgambo huko Benghazi tarehe 21 Septemba. Wakaazi wa Benghazi
wanalaumu Ansar al-Sharia kwa shambulio la tarehe 11 Septemba katika
ubalozi wa Marekani, [Abdullah Doma/ AFP]
Kwenye mstari wa mbele wa wimbi kubwa la Wasalafi huko Tunisia, Libya na
Yemen ni vikundi vinavyokusanyika chini ya kivuli cha "Ansar
al-Sharia". Kwa mara ya kwanza, wachambuzi wengi waliamini kuwa vikundi
hivi vilikuwa ni jaribio la Wasalafi wa sasa kufuata hali mpya na kwamba
mwishoni wataachana na itikadi ya vurugu za jihadi.
Hata hivyo, kwa kadri mtafiti wa Morocco Abdellah Rami anavyoelezea,
vikundi vya Ansar al-Sharia kwa sasa vinafanya kazi kama "taswira ya
itikadi, hazina ya ubinadamu na watoaji wa fedha kwa wapiganaji wa
al-Qaida." Sabahi ilikaa chini na Rami, mchambuzi wa masuala ya kisiasa
aliyebobea katika vikundi vya Kiislamu katika Kituo cha Sayansi Jamii
cha Morocco, kujadili tukio hili jipya na matarajio yake.
Sabahi: Unachukuliaje kutokea kwa vikundi kadhaa vipya vya Wasalafi
vinavyojiita Ansar al-Sharia kuwa ni kutokea tu kwa bahati au ni sehemu
ya mpango mkubwa?
Abdellah Rami: Mimi silifikirii hili kama tukio la bahati tu. Hili kwa
hakika ni matokeo na mipango inayodhamiria kujizoesha tena mazingira
mageni ya jihadi ya Wasalafi wa sasa kwenda kwenye hali mpya ambayo
imetengenezwa na mapinduzi ya Chemuchemu ya Uarabuni (Arab Spring)
katika kanda hiyo.
Comments