Skip to main content

MILOVAN AWATOSA BOBAN NA NYOSO





KOCHA Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic amesema hajutii kuwakosa beki Juma Nyoso na mshambuliaji Haruna Moshi 'Boban', ambao wamesimamishwa na uongozi kwa muda usiojulikana.
Kocha huyo kutoka Serbia ameelezea msimamo wake huo siku moja baada ya uongozi wa Simba kutangaza kuwasimamisha wachezaji hao kwa makosa ya utovu wa nidhamu.
Milovan alisema wachezaji hao wanastahili adhabu waliyopewa na uongozi kwa vile wamekithiri kwa utovu wa nidhamu na pia ni chanzo cha timu kufanya vibaya katika michuano ya ligi.
Kocha huyo alisema, licha ya wachezaji hao kuwa muhimu kwenye kikosi chake na kusimamishwa kwao ni pengo katika timu, suala la nidhamu ni la muhimu zaidi kuliko mchezaji binafsi.
"Boban na Nyoso ni wachezaji wazuri na wanapokosekana katika timu huwa inapwaya, lakini mambo wanayofanya hayawezi kuvumilika,"alisema.
Hata hivyo, Milovan alisema kikosi chake kinaundwa na wachezaji wengi wazuri, wakiwemo waliopandishwa daraja msimu huu, hivyo anaamini timu itaweza kufanya vizuri bila kuwepo kwao.
"Hata Ulaya wachezaji nyota wanapokosa nidhamu, husimamishwa lakini, wapo wengine ambao huchukua nafasi zao na timu ikafanya vizuri, hivyo kusimamishwa kwao kwa utovu wa nidhamu hata mimi naafiki," alisema Cirkovic.
Alisema kwa sasa, timu yake inaendelea na mazoezi ya kujiwinda na mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Azam utakaofanyika keshokutwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mapema jana, Simba kupitia kwa ofisa wake wa habari, Ezekiel Kamwaga ilitangaza jana kuwa, imemsimamisha Boban kuichezea timu ya wakubwa kutokana na vitendo vyake vya utovu wa nidhamu na pia kutokuwa na heshima kwa mwajiri wake.
Kamwaga alisema uongozi umempa Boban siku 21 kutoa maelezo kuhusu makosa yake na iwapo atashindwa kufanya hivyo, klabu inaweza kumchukulia hatua kali zaidi za kinidhamu.
Ofisa huyo alisema, katika kipindi hicho cha siku 21, Boban atalipwa nusu ya mshahara wake wa kila mwezi na hatapata marupurupu yoyote yanayohusiana na timu ya wakubwa.
Akimzungumzia Nyoso, ofisa huyo alisema uongozi umemwagiza afanye mazoezi na kikosi cha timu ya pili ya Simba B hadi hapo atakapoimarisha kiwango chake cha uchezaji.
Alisema hatua hiyo imetokana na ripoti ya benchi la ufundi kuonyesha kuwa, mchezaji huyo amekuwa akifanya makosa mengi uwanjani yanayoigharimu timu, na ingawa amekuwa akipewa maelekezo na walimu, bado amekuwa akiyarudia mara kwa mara.
Kamwaga alisema, kutokana na kosa hilo, Nyoso atafanya mazoezi na wachezaji wa kikosi cha pili hadi walimu watakaporidhika kwamba amejirekebisha na yuko tayari kukitumikia kikosi cha wakubwa.
Aliongeza kuwa, katika muda wote huo atakaokuwa akifanya mazoezi na timu B, Nyoso atakuwa akipata mshahara wake wa kila mwezi kama kawaida na pia atapata marupurupu wanayopata wachezaji wa timu hiyo.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.