Skip to main content

MILOVAN AWATOSA BOBAN NA NYOSO





KOCHA Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic amesema hajutii kuwakosa beki Juma Nyoso na mshambuliaji Haruna Moshi 'Boban', ambao wamesimamishwa na uongozi kwa muda usiojulikana.
Kocha huyo kutoka Serbia ameelezea msimamo wake huo siku moja baada ya uongozi wa Simba kutangaza kuwasimamisha wachezaji hao kwa makosa ya utovu wa nidhamu.
Milovan alisema wachezaji hao wanastahili adhabu waliyopewa na uongozi kwa vile wamekithiri kwa utovu wa nidhamu na pia ni chanzo cha timu kufanya vibaya katika michuano ya ligi.
Kocha huyo alisema, licha ya wachezaji hao kuwa muhimu kwenye kikosi chake na kusimamishwa kwao ni pengo katika timu, suala la nidhamu ni la muhimu zaidi kuliko mchezaji binafsi.
"Boban na Nyoso ni wachezaji wazuri na wanapokosekana katika timu huwa inapwaya, lakini mambo wanayofanya hayawezi kuvumilika,"alisema.
Hata hivyo, Milovan alisema kikosi chake kinaundwa na wachezaji wengi wazuri, wakiwemo waliopandishwa daraja msimu huu, hivyo anaamini timu itaweza kufanya vizuri bila kuwepo kwao.
"Hata Ulaya wachezaji nyota wanapokosa nidhamu, husimamishwa lakini, wapo wengine ambao huchukua nafasi zao na timu ikafanya vizuri, hivyo kusimamishwa kwao kwa utovu wa nidhamu hata mimi naafiki," alisema Cirkovic.
Alisema kwa sasa, timu yake inaendelea na mazoezi ya kujiwinda na mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Azam utakaofanyika keshokutwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mapema jana, Simba kupitia kwa ofisa wake wa habari, Ezekiel Kamwaga ilitangaza jana kuwa, imemsimamisha Boban kuichezea timu ya wakubwa kutokana na vitendo vyake vya utovu wa nidhamu na pia kutokuwa na heshima kwa mwajiri wake.
Kamwaga alisema uongozi umempa Boban siku 21 kutoa maelezo kuhusu makosa yake na iwapo atashindwa kufanya hivyo, klabu inaweza kumchukulia hatua kali zaidi za kinidhamu.
Ofisa huyo alisema, katika kipindi hicho cha siku 21, Boban atalipwa nusu ya mshahara wake wa kila mwezi na hatapata marupurupu yoyote yanayohusiana na timu ya wakubwa.
Akimzungumzia Nyoso, ofisa huyo alisema uongozi umemwagiza afanye mazoezi na kikosi cha timu ya pili ya Simba B hadi hapo atakapoimarisha kiwango chake cha uchezaji.
Alisema hatua hiyo imetokana na ripoti ya benchi la ufundi kuonyesha kuwa, mchezaji huyo amekuwa akifanya makosa mengi uwanjani yanayoigharimu timu, na ingawa amekuwa akipewa maelekezo na walimu, bado amekuwa akiyarudia mara kwa mara.
Kamwaga alisema, kutokana na kosa hilo, Nyoso atafanya mazoezi na wachezaji wa kikosi cha pili hadi walimu watakaporidhika kwamba amejirekebisha na yuko tayari kukitumikia kikosi cha wakubwa.
Aliongeza kuwa, katika muda wote huo atakaokuwa akifanya mazoezi na timu B, Nyoso atakuwa akipata mshahara wake wa kila mwezi kama kawaida na pia atapata marupurupu wanayopata wachezaji wa timu hiyo.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...