Skip to main content

JK: Nilitaka Kunyonga Wauaji Wa Albino



Suzy Butondo, Shinyanga, MWANANCHI 

 RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa kuna wakati aliwahi kufikiria kuwanyonga watu waliokuwa wakikamatwa kwa kuhusika na mauaji ya albino yalipokuwa yamepamba moto kwa kuwa jambo hilo lilikuwa likimtia hasira. 

Rais Kikwete alisema hayo jana katika kilele cha kumuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga. Rais alisema hayo alipokuwa akizungumzia tukio la uchomwaji wa moto makanisa lililotokea Mbagala, Dar es Salaam akieleza athari za mtu mwenye jazba kuchukua hatua. Juzi, Rais Kikwete alitembelea eneo la hilo la tukio na kushuhudia makanisa matatu yalivyoharibiwa pamoja na magari.

 “Kwenye lile la maalbino nilishaandika kwenye hotuba yangu nitanyonga watu kwa kuwa nilikuwa nina hasira, lakini washauri wangu waliniambia hiyo itakuwa ni kinyume cha sheria kwa kuwa kuna watu walikuwa wamepelekwa mahakamani na hata uamuzi haujatolewa,” alisema Rais Kikwete na kuongeza: “Nilifuta baada ya kushauriwa, lakini hadi sasa nina hasira. Ninajitolea mfano wangu mwenyewe ili muone kwamba kujichukulia uamuzi kusivyokuwa vizuri wakati una hasira.” 

Alirejea kauli yake kwamba kitendo cha mtoto kukojolea kitabu kitukufu cha Waislamu kilikuwa ni kosa kubwa na Waislamu walikuwa na haki ya kukasirika, lakini haikuwa sawa kwao kuvamia makanisa. Rais Kikwete alisema kitendo cha wao kuvamia makanisa na kuyachoma na kuvamia kituo cha polisi ni kinyume cha sheria za nchi.

 “Mtoto mwenyewe kwanza hakutumwa na kanisa pia alikuwa mikononi mwa polisi. Sasa kitendo cha kwenda kituo cha polisi kutaka wapewe mhalifu wao ni kinyume cha sheria pia kuvamia makanisa ilikuwa si sawa.” 

Akerwa na rushwa Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amesema anakerwa na jinsi vitendo vya rushwa vinavyozidi kushamiri nchini na kutoa wito kwa Watanzania wote kushiriki kwa pamoja kuwafichua na kuwataja hadharani wale wote wanaojihusisha na tabia hiyo. 

Alisema anachukizwa kuona vitendo vya rushwa vikizidi kushamiri, huku jamii ikikaa kimya bila kukemea kwa kuwafichua watu wanaojihusisha na vitendo hivyo ambavyo vinachangia kwa kiasi kikubwa kuwanyima haki Watanzania walio wanyonge. 

 “Nawaombeni ndugu zangu tushirikiane kwa pamoja kupiga vita suala hili la rushwa, maana linaelekea kuota mizizi, ni wajibu wa kila mmoja wetu kujitoa muhanga kupiga vita ugonjwa huu wa rushwa. 

Tuikemee sisi sote raia na wasio raia, watumishi wa umma na wasiokuwa watumishi wa umma, wafanyabiashara binafsi na wasiokuwa wafanyabiashara na kila mmoja awe ni balozi wa kupambana na vitendo vya rushwa.” 

Mbio za Mwenge zilizinduliwa Mei 11, mwaka huu huko Mbeya na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Waumini wasali nje Siku tatu baada ya makanisa kuchomwa moto na kuharibiwa vibaya, baadhi ya waumini wamelazimika kusali wakiwa nje, huku viongozi wao wakiwataka kutolipiza kisasi kama mafundisho ya dini zao yanavyoelekeza. 

Hata hivyo, viongozi hao wameitaka Serikali kutekeleza ahadi yake ya kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika na uharibifu huo ili liwe fundisho kwa wengine. Juzi, Rais Kikwete alitembelea makanisa hayo na kuagiza polisi kuwasaka na kuwakamata wote waliohusika ili wafikishwe kwenye vyombo vya sheria. Jana, Mkuu wa Jimbo la Kusini la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Mchungaji Aman Lyimo alisema kwamba katika Usharika wa Mbagala, kamwe hawatalipiza kisasi dhidi ya waovu hao.

 “Waliofanya kitendo hicho si Waislamu, bali ni wahuni wanaotumia dini kama kichaka cha kuficha uovu wao, tuliosomea dini mbalimbali tunafahamu kwamba hakuna dini yoyote inayoruhusu kufanya uovu kama huu uliofanywa katika makanisa.”

 “Hatutawalaani wala kuwahukumu kwa sababu hawajui walitendalo, tutakachokifanya ni kuendelea kuwaelimisha bila kuchoka kwamba wanatakiwa kutubu kwa sababu wamemkosea Mungu.” Kiongozi wa Kanisa la Anglikana, Usharika wa Mbagala Kizuiani, Emmanuel Mng’ong’o alisema waumini wa kanisa hilo wamefanya ibada yao katika mazingira magumu baada ya vurugu hizo. Alisema madirisha 36 ya vioo vya kanisa hilo yalivunjwa, huku madhabahu ikiwa imeharibiwa... 

“Tuna imani na ahadi ya Rais Jakaya Kikwete kwamba waliofanya uhalifu huo watachukuliwa hatua za kisheria.” Kamanda wa Mkoa wa Temeke, David Misime alisema jana kwamba hadi sasa jeshi hilo linawashikilia watu 122 kuhusiana na vurugu hizo. 

CCM walaani Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimelaani kitendo cha kukojolea Kitabu cha Quran na uchomaji wa makanisa. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema, “Vitendo hivi havifanani na utamaduni wetu Watanzania, wanaosifika kwa amani na utulivu.” Aliwataka wananchi kuwa na subira yanapojitokeza matukio kama hayo na kwamba vyombo vya dola vitachukua hatua stahiki kwa wote waliohusika.

Chanzo, MWANANCHI

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...