Skip to main content

Mnyika: Watendaji hawaelezi ukweli tatizo la umeme


WAZIRI Kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika, ameeleza kusikitishwa na kauli za viongozi na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kuhusu hali ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini sanjari na uboreshaji wa utendaji TANESCO.
Amesema kauli hizo zinatoa matumaini potofu kwa wananchi na kuwasihi kuzipokea kwa tahadhari kwa kuwa hazielezi ukweli kuhusu tatizo la umeme nchini.
Mnyika ambaye pia ni mbunge wa Ubungo, alitoa kauli hiyo jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari na kusema kulingana na nyaraka alizonazo za ndani ya wizara hiyo na TANESCO kuanzia Septemba hadi Oktoba mwaka huu, hali ya uzalishaji na usafirishaji na usambazaji wa umeme imekuwa tete kwa sababu mbalimbali ikiwemo upungufu wa upatikanaji wa mafuta na gesi asili kwa ajili ya uendeshaji wa mitambo ya kufua umeme na kasi ndogo ya uwekezaji kwa ajili ya kupata ufumbuzi wa kudumu.
Mnyika pia alisema amemwandikia barua Spika wa Bunge, Anne Makinda, ili Wizara ya Nishati na Madini iwajibike kueleza hali halisi katika mikutano ya kamati za Bunge inayoendelea.
“Katika barua hiyo nimependekeza pamoja na mambo mengine suala la kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme na utekelezaji wa mpango wa uboreshaji wa utendaji wa TANESCO lishughulikiwe na kamati nyingine kwa haraka kwa kuzingatia maelezo na maelekezo ya Spika aliyoyatoa bungeni wakati wa kuahirisha mkutano wa nane wa Bunge,” alisema.
Aidha alisema mapitio ya utekelezaji wa mpango wa uboreshaji wa utendaji wa shirika hilo yahusishe kamati ya kudumu ya Bunge na itakayoeleza hatua iliyofikiwa katika uchunguzi wa tuhuma za ufisadi kwa kuzingatia kuwa siku 60 za uchunguzi zimepita.
Chanzo Tanzania Daima

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.