Skip to main content

HASSANALI KUIWAKILISHA TANZANIA MAONYESHO YA MAVAZI AFRIKA KUSINI



Mbunifu maarufu wa mavazi kutoka Tanzania, Mustafa Hassanali ndiye Mtanzania pekee katika fani ya mitindo aliyepewa mualiko wa kushiriki katika maonyesho ya Wiki ya Mitindo Afrika chini ya African Fashion International (AFI) yatakayofanyika kwa siku nne kuanzia tarehe 24-28 Oktoba, 2012 katika ukumbi wa Melrose Arch, jijini Johannesburg, Afrika ya Kusini.
Mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya kutengeneza Magari ya Mercedes-Benz yanatarajiwa kuwashirikisha wabunifu wa mavazi zaidi ya 35 kutoka sehemu mbalimbali barani Afrika, baadhi ya nchi hizo ni wenyeji Afrika ya Kusini, Ivory Coast, Morocco, Msumbiji, Cameroon, Rwanda, Angola, DRC, Nigeria, Ghana na Tanzania.
“Ni maonyesho ya pekee na yenye heshima yake barani Afrika na hata duniani kwa ujumla kwani wabunifu walioalikwa ni wazoefu na bora katika fani ya Mitindo barani Afrika. Hivyo mwaliko wangu si tu utaweza kutangaza kazi ni nazofanya bali pia utasaidia kutangaza nchi yetu ya Tanzania kupitia maonyesho haya” Alisema, Mustafa Hassanali.
“Watakapotaja jina langu pale katika maonyesho, hawatasema tu huyu ni Mustafa Hassanali, bali watasema huyu ni Mustafa Hassanali kutoka Tanzania, hivyo itakuwa ni mchango mkubwa kwa nchi yetu kuweza kuonyesha fursa zilizopo kupitia Ubunifu wa Mitindo. Nimejiandaa vizuri katika haya maonyesho, nataka kuonyesha nini Tanzania tunacho katika tasnia ya ubunifu kwa ulimwengu mzima ni imani yangu kufanya vizuri” aliongeza Hassanali.
AFI inaandaa mashindano haya ili kuweza kutangaza kazi za wabunifu wa mavazi kutoka barani Afrika katika soko la dunia kwani Afrika ina wabunifu wazuri na imara hivyo kujitokeza kwao katika maonyesho haya kutafungua milango zaidi katika soko la kimataifa na kuongeza fursa nyingi zitakazoinua uchumi wa bara hili kupitia sanaa ya ubunifu wa mitindo.
Licha ya kushiriki katika maonyesha haya, Mustafa Hassanali pia anawaomba Watanzania wote kwa ujumla kuweza kumpigia kura ya kuwa mwanamitindo bora barani Afrika kupitia tovuti ya www.awardnomination.afi.za.com na kuweza kuiletea sifa tasnia ya mitindo nchini Tanzania.
Huu ni mwaka wa tisa kwa Mustafa Hassanali kupata mwaliko wa kuonyesha ubunifu wake katika maonyesho haya. Ameshashiriki katika maonyesho zaidi ya nchi 16 katika miji 25 tofauti duniani, amekuwepo katika kilinge cha sanaa ya mitindo kwa muda mrefu hapa nchini, amechangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko na maendeleo ya kazi za ubunifu wa mavazi hapa Tanzania.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.