Skip to main content

MAJAMBAZI WALIONIPORA NI MASHABIKI WANGU-JULIET





ACCRA, Ghana
MCHEZA filamu Juliet Ibrahim wa Ghana amesema majambazi
yaliyompora vitu vyenye thamani mbali mbali nyumbani kwake, ni
mashabiki wake wakubwa.
Juliet amewaelezea majambazi hao kuwa ni mashabiki wake
kutokana na kutomdhuru yeye na familia yake.
Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti hivi karibuni kuwa, Juliet
alikutwa na mkasa huo kwenye uwanja wa ndege wa Accra wakati
alipokuwa akirejea kutoka safarini Marekani.
Hata hivyo, Juliet alisema si kweli kwamba tukio hilo lilitokea
uwanja wa ndege. Alisema majambazi hao walimpora baada ya
kufika nyumbani kwake.
Alisema katika tukio hilo, majambazi hao walipora simu zao za
mkononi na pesa taslim, lakini hakuwa tayari kutaja thamani yake.
"Napenda kila mmoja afahamu kwamba, nipo katika hali nzuri mimi
na familia yangu na tukio la kuporwa lilitokea nyumbani, si uwanja
wa ndege,"alisema.
Kwa mujibu wa Juliet, tukio hilo lilitokea saa tatu usiku wakati
umeme ulipokuwa umekatika katika maeneo mengi ya Jiji la Accra.
"Kama kungekuwa na mwangaza, tungeweza kuwaona majambazi
hao walipoegesha gari lao jeusi. Nadhani katika kipindi hiki, kuna
matukio mengi yatakayotokea kwa sababu ya tatizo la kukatika kwa
umeme nchi nzima,"aliongeza.
Aliongeza kuwa, anachoshukuru ni kwamba yeye na familia yake
hawakupata madhara yoyote wakati wa tukio hilo.
"Natumaini majambazi hawa watakuwa wakisoma ujumbe huu.
Napenda kusema asante kwao kwa kutimiza maneno yao ya
kutoidhuru familia yangu. Ni mashabiki wazuri kwangu,"alisema
Juliet.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.