Skip to main content

Dk: Nchimbi Akabidhiwa Ripoti Ya Mauaji Ya Mwangosi



Na: Ibrahim Yamola 

 KAMATI iliyokuwa ikichunguza vurugu zilizotokea mkoani Iringa na kusababisha kifo cha aliyekuwa Mwandishi wa Kituo Cha Televisheni cha Channel Ten, David Mwangosi imekabidhi ripoti yake kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Dk Emaanuel Nchimbi. Katika vurugu hizo ambazo zilizotokea Kijiji cha Nyololo wilayani Mufindi Septemba 2 mwaka huu, kati ya Polisi na wafuasi wa Chadema waliokuwa wakifungua tawi la Chama hicho baadhi ya watu walijeruhiwa akiwemo askari wa jeshi hilo. 

Taarifa iliyotolewa jana na Msemaji wa Wizara hiyo Isaac Nantanga ilisema kamati hiyo imekamilisha kazi iliyopewa na hivyo kusubibili kikao cha kamati hiyo na waziri wiki ijayo. “Waziri ameishukuru kamati hiyo kwa kazi walioifanya na Jumanne (kesho kutwa) atafanya kikao na waandishi wa habari” alisema Nantanga. Wakati akiitangaza kamati hiyo Dk Nchimbi aliitaka kujibu maswali sita ambayo yalikuwa hanaya majibu kutokana na tukio hilo.

 “Tuna maswali sita ambayo mimi sina majibu yake. Swali la kwanza tunataka kujua nini chanzo cha kifo cha Daudi? 
Pili tujue ni kweli kwamba kuna uhasama kati ya polisi na waandishi Iringa?” alisema Dk Nchimbi Aliongeza:

 “Tatu tujue kama ni kweli kuna orodha ya waandishi watatu wa kushughulikiwa Iringa? Nne kama nguvu zilizotumika zilistahili? Tano kama kuna utaratibu wa vyama vya siasa kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa polisi? 

Mwisho kujua uhusiano wa Jeshi la Polisi na vyama vya siasa ukoje?” Dk Nchimbi alisema, sheria lazima zifuatwe kwani nchi ikiingia kwenye matatizo, Serikali haitaweza kuwaeleza wananchi kwamba ndicho kitu kinachotakiwa...

 “Hatutaki tuwe na vita vya wenyewe kwa wenyewe.” Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Theophil Makunga alisema kamati yake ilifanya ziara katika mikoa ya Iringa na Dar es Salaam na kufanya mahojiano na wadau mbalimbali. 

 Alisema wakati wa zoezi hilo walizingatia yale waliyoelezwa na Dk Nchimbi ikiwa ni kufanya kazi kwa kuweka mbele maslahi ya taifa.

 “Alitutaka kufanya kazi bila kuegemea upande mmoja wa Serikali ama chama na tumejibu maswali yote yaliyokuwa katika habibu za rejea alizotupa bila kuacha hata moja,” alisema Makunga. Aliongeza licha ya kujibu habibu hizo za rejea pia tumetoa mapendekezo ambayo kama yatatekelezwa hakutatokea tukio kama hilo. Alipotakiwa kueleza kilichomo ndani ya ripoti hiyo alisema hawezi na kutaka kusubiri Jumanne ambapo Waziri na Kamati nzima itazungumza na waandishi wa habari. 

Kamati hiyo ilikuwa watu watano ambayo ilikukuwa chini ya Mwenyekiti , Jaji mstaafu Steven Ihema, mwakilishi wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga, Wajumbe wengine walikuwa ni mwakilishi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Pili Mtambalike, mtaalamu wa milipuko kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Kanali Wema Wapo na Naibu Kamishina wa Polisi (DCP), Isaya Mngulu.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...