Skip to main content

Viongozi wa chama cha Upinzani Chadema watarajiwa kuachiliwa kutoka kizimbani leo



Mwenyekiti wa chama cha upinzani Chadema, Freeman Mbowe katika mahakama ya KisutuHaki miliki ya pichaCHADEMA MEDIA
Image captionMwenyekiti wa chama cha upinzani Chadema, Freeman Mbowe katika mahakama ya Kisutu
Viongozi sita wa Upinzani nchini Tanzania wamefikishwa mahakamani kusaini hati za dhamana zao na ili kuachiwa huru.
Viongozi hao wa chama cha CHADEMA, akiwemo mwenyekiti Freeman Mbowe, walishtakiwa kwa uchochezi ,kuleta vurugu na kuandamana mwezi wa Februari mwaka huu.
Mjumbe mwingine , Halima Mdee, ameongezewa kwenye mashtaka na kufanya jumla ya washtakiwa kuwa saba.
Halima MdeeHaki miliki ya pichaCHADEMA MEDIA
Image captionHalima Mdee
Hapo awali,mjumbe wa Chadema, Halima Mdee alikamatwa alfajiri jana, Aprili Mosi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere akitokea nchini Afrika Kusini inakoeelezwa alilalzwa kwa matibabu.
Kwa mujibu wa ukurasa wa Facebook wa Chadema Media imesema kwamba "Tunatoa mwito kwa Jeshi la Polisi limpatie dhamana ili aweze kuendelea na matibabu yake, Kwani dhamana ni haki yake na zaidi ni kuwa huyu bado ni mtuhumiwa na ni Mgonjwa ambaye ametoka hospitalini."
Eagan Salla, mwandishi wa BBC aliyopo katika mahakama ya Kisutu anasema, 'hali ya ulinzi mahakamani imeimarishwa ijapokuwa wafuasi wa chadema nao wanaonekana nje ya mahakama wakisubiri hatima ya viongozi wao'
Ulinzi umeimarishwa katika mahakama ya Kisutu Dar es salaam
Image captionUlinzi umeimarishwa katika mahakama ya Kisutu Dar es salaam
Alhamisi iliopita, mahakama ya hakimu mkazi Kisutu iliwapatia dhamana viongozi hao sita lakini kusema kuwa watasalia rumande hadi kesi leo tarehe 3 Aprili ambapo wataletwa mahakamani kukamilisha masharti ya dhamana.
Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa akisubiri nje ya chumba cha mahakama
Image captionWaziri mkuu wa zamani Edward Lowassa akisubiri nje ya chumba cha mahakama
Wanasiasa hao hawakuletwa mahakamani katika uamuzi wa dhamana yao huku afisa wa magereza akiiambia mahakama ni kutokana na gari lililotakiwa kuwasafirisha kuja mahakamani hapo kuwa bovu.
Miongoni mwa mashtaka waliyosomewa ni pamoja na maandamano yaliyosababisha kifo cha mwanafunzi wa chuo cha NIT Akwilina Akwiline.
Wanashtakiwa pia kuendelea kufanya mkusanyiko usio halali wilayani Kinondoni shtaka linalowakabili washtakiwa wote.
Hatua hii ya viongozi hawa kuendelea kusota rumande wakisubiria dhamana inaleta picha gani?
Akizungumza na BBC, mchambuzi wa maswala ya siasa Rashid Chilumba anaelezea kwamba kampeni ya kuwelenga upinzani katika awamu iliopo imevuka "mstari mwekundu"
"Viongozi wa upinzani wanapowekwa ndani haitoi taswira nzuri katika mwenendo wa siasa ya ushindani, hasa ukizingatia kwamba kume kuwa tayari na wasiwasi kuwa utawala unebana zaidi upinzani" alielezea Chilumba.
Kesi gani zinazowaandama wanasiasa wa upinzani hasa Chadema?
Kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo, kuna wabunge 13 wa chama hicho wanaokabiliwa na kesi katika mahakama mbalimbali.Chama kikuu cha upinzani Chadema ndicho kinachoonekana kuwa na idadi kubwa ya wanasiasa wake wanaozongwa na kesi mbali mbali.
Mbunge wa Singida, kupitia chama cha chadema Tundu Lissu ambaye kwa sasa yuko nchini Ubelgiji kwa matibabu,anakabiliwa na kesi sita. Kesi zote zinahusiana na uchochezi.
Lissu anasemekana kuwa ndiye mwanasiasa aliyekamatwa mara nyingi zaidi ya wengine. Miongoni mwa kesi zake zilizoibua mjadala mkubwa ndani na nje ya nchi ni ile aliyoshutumiwa kutoa matamko ya uchochezi na kumuita Rais John Magufuli 'dikteta uchwara'.
Joseph Mbilinyi, maarufu kwa jina la kazi zake za usanii Sugu, ambaye ni mbunge wa Mbeya mjini, sasa yuko gerezani kwa kipindi cha miezi mitano baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kutumia lugha za matusi dhidi ya Rais Magufuli.
Kwa upande wake Halima Mdee, mbunge wa jimbo la Kawe jijini Dar es salaam, yeye anazo kesi nne zote zikiwa za uchochezi ikiwemo ile aliyotuhumiwa kutumia lugha mbaya kumpinga Rais Magufuli baada ya kutangazwa kwa marufuku ya kuwaruhusu wanafunzi wa kike kurudi shuleni mara wapatapo ujauzito.
Mbunge wa Arusha Godbless Lema yeye anakabiliwa na kesi nne pia huku zote zikiwa za uchochezi. Siku za nyuma Lema aliwahi kukaa mahabusu kwa muda wa miezi minne kwa kosa la uchochezi. Hivi sasa Lema amekuwa akihudhuria mahakamani mara kwa mara.
Mwenyekiti wa Chadema taifa na kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Freeman Mbowe yeye ana kesi 3 ikiwemo kesi ya wiki hii. Kwa sasa anahitajika kuhudhuria polisi kila siku.
John Mnyika mbunge wa jimbo la ubungo jijini Dar es salaam kwa upande wake anahitajika kuhudhuria polisi kila wiki tangu jaribio la kufanyika kwa maandamano ya chama hicho mwezi uliopita. Huyu kesi yake yeye bado haijawekwa wazi
Mbunge wa Mara, Esther Bulaya, aliwahi kushikiliwa na polisi kwa kosa la kutaka kuandaa mkutano wa hadhara nje ya jimbo lake, jambo ambalo polisi walidai kuwa lilikuwa ni uvunjifu wa sheria.Source BBC

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.