Skip to main content

Tanzania Kuunadi utamaduni wetu katika tamasha la Mabara

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dk.Hamisi Kigwangala jana alishiriki
katika mkutano wa  kamati ya maandalizi ya tamasha la mabara litakalo
fanyika nchini Ufaransa Julai mwaka huu.

Hayo yalisema na wazili Kigwangala katika mkutano huo uliofanyika 
Jjini Dar es Salaam jana ambapo alisema kuwa tanzania itakuwa ni
moja wapo katika ushiriki wa tamasha hilo ambapo jumla ya nchi 54
zitashiriki kuonesha urithi wake.

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dk.Hamisi Kigwangala


Alisema tamasha hilo litakuwa na utamaduni  wa urithi wa asili na
kuwa kamati hiyo imehusisha nchi 7 zikiwemo Kenya ,Tanzania ,Ivery 
Coast.


Hivi karibuni Kigwangala alisema kuwa sekta ya utalii imekuwa 
mhimili muhimu katika ukuaji wa uchumi  wa Tanzania ambapo kwa 
mwaka 2017 sekta ya  utalii imechangia dola za kimarekani Bilioni
2.1 takriban asilimia 25  ya  fedha za kigeni .

"Kupitia tamasha hilo la Mabara Urithi wa Taifa la Tanzania tutaweza
kuutangaza vema mambo kama urithi wa lugha , ngoma zetu za asili
tutaweza kuvitangaza vema,"alisema Kigwangala.


Kigwangala alisema kuwa kuelekea mwezi septemba 
tayari amezindua kamati ya kitaifa ya kuandaa Mwezi 
maalumu wa maadhimisho ya Urithi wa Taifa la Tanzania
ambapo kuppitia tamasha la mabala wataweza kujifunza
mambo zaidi.

Pia  miji ya kihistoria kama vile Bagamoyo na Kilwa, 
michoro ya miambani, Kondoa na mapango ya Amboni.

Aliongeza  Tanzania ikiwa na zaidi ya makabila 120 imejaliwa kuwa 
na anuaia za mila, desturi, vyakula, misemo, imani, mavazi, 
nyimbo, ngoma za aina mbali mbali na matumizi ya lugha ya 
Kiswahili katika  kuunganisha Watazania. 

Comments