Skip to main content

Akina mama na Vijana Manispaa ya Ubungo kupatiwa bilioni 1.9 kwaajili ya mikopo

Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es Salaam
imetangaza kutoa kiasi cha shilingi bilioni 1.9 kwa ajili
mikopo kwa kinamama na vijana na walemavu kuanzia leo .




Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
serikali za mitaa TAMISEMI Joseph Kakunda aliye katikati  na upande 
wa kulia ni Meyawa Manispaa ya Ubungo Boniface Jacob, na upande wa
 kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Kisare Makori.

Hayo yamesemwa na mgeni rasmi Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Joseph Kakunda katika
uzinduzi wa mikopo hiyo viwanja vya Barafu Mburahati.
Vviongozi wa CCM Ubungo wakiongozwa na Katibu wao Lucas Magonja wakifurahia wimbo wa kulipongeza Manispaa ya Ubungo ulioimbwa na kikundi cha kwaya cha Wilaya hiyo

Alisema ameishukuru Manispaa ya Ubungo kwa kutekeleza vyema Ilani
ya CCM  kwa kutenga fedha kwa ajili ya makundi ya  Wanawake,
vijana na walemavu, na kumuagiza Katibu Mkuu wa TAMISEMI 
kuiandikia  Barua ya pongezi Manispaa hiyo kwa kutekeleza
agizo la serikali.






"Ningependa Manispaa hii kutenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara
wa dogo ili kuondoa usumbufu wanao upata katika maeneo ya barabara
ambapo mara nyingi huondolewa,"alisema Kakunda.

Baadhi ya wajasiriamalimali waliofika katika maonyesho ya Biashara 
katika uwanja wa Barafu
Kakunda aliwataka  vijana kujitokeza zaidi kushiriki katika
mikopo hiyo  uzinduzi  vijana wajitokeze kuomba mikopout
kwa sababu hadi sasa idadi ya waliojitokeza kuomba mikopo
ni ndogo.



Nae kaimu Mkurugenzi wa CRDB alikuja katika hafla hii kwa
niaba ya Mkurugenzi wa CRDB ndg.Charles Kimei amesema wanayo
furaha kubwa kuona wamekuwa benki iliyochaguliwa kufanya
kazi na Manispaa ya Ubungo.

Aidha alisema kuwa  wameahidi kutoa ushirikiano na kutimiza yale yote
 waliyokubaliana katika mkataba,na wanajisikia fahari kufanya kazi na 
Manispaa hii kwani wameonyesha wako makini katika masuala mbalimbali.


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo, Mhe Boniface Jacob
alisema walisaini mkataba wa makubaliano na benki yaCRDB
ambapo mikopo hiyo itatolewa kupitia benki hiyo.


Naye Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Halmashauri ya Manispaa
imetenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani ya mwaka mmoja
nanusu waliyoitunza kwa uaminifu mkubwa ndio zikapatikana shilingi
1.9 Bilioni kwa ajili ya mikopo kwa kinamama na vijana.


"Uzinduzi huo ulianza sikumbili zilizopita ambapo leo ni siku ya tatu
katika viwanja hivi na jumla ya kata 14 vikundi vyote vilisha
pata semina  kuelimishwa na kuwa mradi huo upochini ya CRDB
ambao ni wadau wakubwa wa sera ya maendeleo ya viwanda,"alisema
                                                                                Kayombo




Comments