Skip to main content

Mkataba mabadiliko ya tabia nchi nchi itanufaika kwa kupata fedha za kukabili athari za mabadiliko ya tabia nchi





BUNGE limeridhia makubaliano ya Paris kuhusu kuboresha utekelezaji wa mkataba wa makubaliano ya tabia nchi ambayo pamoja na masuala mengine, nchi itanufaika kwa kupata fedha za kukabili athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Kupitia azimio la bunge la kuridhia makubaliano lililowasilishwa jana bungeni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba, fedha hizo kwa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania, zitapatikana kupitia ufadhili wa mifuko ya mabadiliko ya tabia nchi na wadau wengine. “Nchi zilizoendelea zitatakiwa kutoa taarifa kila baada ya miaka miwili kuhusu kiwango cha fedha walizotoa au wanatarajia kutoa kama msaada kwa nchi ambazo ziko hatarini kuathirika na mabadiliko ya tabia nchi,” alisema Makamba.


Waziri Makamba alisema, kwa kuwa Tanzania inaingia kwenye uchumi wa viwanda, makubaliano hayo ya Paris yatasaidia kuchochea matumizi ya gesi asilia, upatikanaji wa teknolojia safi, kufunza wataalamu na kuendelea kuwa na vyanzo vya nishati endelevu kukabiliana na uchafuzi wa mazingira. Wakati huo huo, serikali imesisitiza taasisi za serikali ikiwemo shule, magereza na hospitali kuhakikisha wanaondokana na matumizi ya kuni na mkaa badala yake wanajikita katika nishati ya kupikia isiyo na athari kwa mazingira.
Kwa mujibu wa Waziri Makamba, taasisi zote zimepewa mwaka mmoja na kuagiza kuwa mtu yeyote anayetaka zabuni ya kupika chakula katika taasisi yoyote, ajipange kutotumia mkaa na kuni. Aidha waziri alisema upandaji miti utapewa msukumo mpya na wanatarajia kufanya sensa kubaini miti iliyopandwa. Katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Ally Saleh Ally, kabla ya azimio hilo kupitishwa na wabunge, alishauri serikali kutenga fedha kutoka vyanzo vya ndani kukabili athari za mabadiliko ya tabia nchi. Kwa upande wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Makamu Mwenyekiti, Innocent Bashungwa alitaja faida zitakazopatikana kutokana na kuridhiwa kwa makubaliano hayo kuwa ni kuwezesha kupambana na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo ukame na mafuriko.
Athari nyingine ni kuenea kwa magonjwa ya kuambukiza, kumezwa kwa visiwa vidogo kwenye bahari na maziwa, kuongezeka kwa ujazo wa maji, kuyeyuka kwa barafu katika kilele cha mlima Kilimanjaro na uharibifu wa miundombinu ya barabara na makazi kutokana na mafuriko. Licha ya kipengele cha upatikanaji wa fedha za utekelezaji, vipengele vingine muhimu vya makubaliano hayo ya Paris yaliyopitishwa katika bunge hili la 11 ni pamoja na vinavyotaka kila nchi mwanachama kutunza misitu inayonyonya gesijoto na kila nchi mwanachama kuwajibika kuandaa na kutekeleza mipango ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi. Vile vile umewekwa mfumo wa nchi zinazoendelea kupata teknolojia, kujengewa uwezo na uelewa katika kushughulikia mabadiliko ya tabia nchi, hali ambayo itaongeza uelewa wa jamii kuhusu hatua za kuchukua kupunguza athari.Source Habarileo.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. SÅ‚awomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...