Skip to main content

Mkataba mabadiliko ya tabia nchi nchi itanufaika kwa kupata fedha za kukabili athari za mabadiliko ya tabia nchi





BUNGE limeridhia makubaliano ya Paris kuhusu kuboresha utekelezaji wa mkataba wa makubaliano ya tabia nchi ambayo pamoja na masuala mengine, nchi itanufaika kwa kupata fedha za kukabili athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Kupitia azimio la bunge la kuridhia makubaliano lililowasilishwa jana bungeni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba, fedha hizo kwa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania, zitapatikana kupitia ufadhili wa mifuko ya mabadiliko ya tabia nchi na wadau wengine. “Nchi zilizoendelea zitatakiwa kutoa taarifa kila baada ya miaka miwili kuhusu kiwango cha fedha walizotoa au wanatarajia kutoa kama msaada kwa nchi ambazo ziko hatarini kuathirika na mabadiliko ya tabia nchi,” alisema Makamba.


Waziri Makamba alisema, kwa kuwa Tanzania inaingia kwenye uchumi wa viwanda, makubaliano hayo ya Paris yatasaidia kuchochea matumizi ya gesi asilia, upatikanaji wa teknolojia safi, kufunza wataalamu na kuendelea kuwa na vyanzo vya nishati endelevu kukabiliana na uchafuzi wa mazingira. Wakati huo huo, serikali imesisitiza taasisi za serikali ikiwemo shule, magereza na hospitali kuhakikisha wanaondokana na matumizi ya kuni na mkaa badala yake wanajikita katika nishati ya kupikia isiyo na athari kwa mazingira.
Kwa mujibu wa Waziri Makamba, taasisi zote zimepewa mwaka mmoja na kuagiza kuwa mtu yeyote anayetaka zabuni ya kupika chakula katika taasisi yoyote, ajipange kutotumia mkaa na kuni. Aidha waziri alisema upandaji miti utapewa msukumo mpya na wanatarajia kufanya sensa kubaini miti iliyopandwa. Katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Ally Saleh Ally, kabla ya azimio hilo kupitishwa na wabunge, alishauri serikali kutenga fedha kutoka vyanzo vya ndani kukabili athari za mabadiliko ya tabia nchi. Kwa upande wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Makamu Mwenyekiti, Innocent Bashungwa alitaja faida zitakazopatikana kutokana na kuridhiwa kwa makubaliano hayo kuwa ni kuwezesha kupambana na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo ukame na mafuriko.
Athari nyingine ni kuenea kwa magonjwa ya kuambukiza, kumezwa kwa visiwa vidogo kwenye bahari na maziwa, kuongezeka kwa ujazo wa maji, kuyeyuka kwa barafu katika kilele cha mlima Kilimanjaro na uharibifu wa miundombinu ya barabara na makazi kutokana na mafuriko. Licha ya kipengele cha upatikanaji wa fedha za utekelezaji, vipengele vingine muhimu vya makubaliano hayo ya Paris yaliyopitishwa katika bunge hili la 11 ni pamoja na vinavyotaka kila nchi mwanachama kutunza misitu inayonyonya gesijoto na kila nchi mwanachama kuwajibika kuandaa na kutekeleza mipango ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi. Vile vile umewekwa mfumo wa nchi zinazoendelea kupata teknolojia, kujengewa uwezo na uelewa katika kushughulikia mabadiliko ya tabia nchi, hali ambayo itaongeza uelewa wa jamii kuhusu hatua za kuchukua kupunguza athari.Source Habarileo.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.