Skip to main content

Jamii yatakiwa kuonesha upendo kwa watoto



Image result for Dkt, Faustine Ndugulile

Naibu waziri wa afya, jinsia wazee na watoto Dkt, Faustin Ndugulile ameitaka jamii kuonyeshwa upendo na mapenzi mema watoto walio na ugonjwa wa usonji kwani no wana haki ya kupatiwa malezi bora kama watoto wengine.
Ameyasema hayo  wakati akizungumza na kituo kimoja cha redio Mkoani Dodoma  ambapo amedai kuwa ugonjwa huo unawapata watoto wadogo na ni ugonjwa unaohitaji watoto kuonyeshwa upendo pamoja na kuwajengea uwezo ili waweze kuwa raia wazuri wa baadae.
Akizungumzia ugonjwa huo DKT Ndugulile amesema ugonjwa huo hauna tiba huku akidai kuwa dalili za ugonjwa huo hubainika pale mtoto anapokuwa na mwaka mmoja au zaidi na moja ya dalili hizo ni pamoja na kushindwa kuongea.
Hata hivyo  Ndugulile amesema serikali inatambua uwepo wa ugonjwa huo na tayari hatua zimeanza kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa walimu ili kuyafahamu makundi ya watoto hao hali itakayosaidia kuyatambua mahitaji maalum yanayopaswa kutolewa kwa watoto hao.
Sanjari na hayo amesema serikali inaendelea kuhamasisha jamii kuutambua na kuuelewa zaidi ugonjwa wa usonji pamoja na kuchukua hatua kwa watu wenye mahitaji maalumu kwenye jamii za kuhakikisha wanapata mahitaji muhimu kama elimu na afya
Aidha Dkt Ndugulile ameyasema hayo mapema leo ikiwa ni siku chache tu zimepita tangu kuadhimishwa kwa siku ya ugonjwa wa usonji nchini ambapo maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka ifikapo april 2.

Comments