Skip to main content

Katika miezi tisa ya mwaka wa fedha TRA imekusanya jumla ya shilingi Trilioni 11.78

Tokeo la picha la Richard Kayombo


Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa 
kodi  kutoka TRA,  Richardi Kayombo.


 Mamlaka ya mapato Nchini Tanzania (TRA), imesema katika miezi tisa ya mwaka wa fedha 2018/17  imekusanya jumla ya shilingi Trilioni 11.78 ikilinganishwa na shilingi Trilioni 10.86 ambazo zilikusanywa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2016/17.
 Kiasi hicho  ni sawa na ukuaji wa asilimia 8.46 ikilingasnisha na trilioni 10.8 zizokusanywa katika kipindi kama hicho katika mwaka uliopita.

Hayo  yamesemmwa leo jijini dar es salaam na Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi  kutoka TRA,  Richardi Kayombo wakati akizungumza na wandishi  wa habari amabapo amesema kuwa katika mwezi machi 2018 wamekusanya jumla ya shilingi trilioni 1.54 ikilinganishwa na  makusanyo ya mwezi  machi 2017  ambapo ilikusanywa shilingi Trilioni 1.34 ambayo ni sawa na ukuaji wa asilimia 14.49.

Aidha amesema kuwa  bado usajili wa walipa kodi wapya unaendelea wakiwemo wamachinga ambapo kwa wiki hii wako katika mkoa wa geita

Katika hatua nyingine  kayombo amesema kuwa kwa sasa wanacnhi wanaweza kulipa kodi ya majengo kwa  njia ya mtandao kwa kumia simu ya mkononi  kwa kupiga *152*00# na kufuatiwa na maelezo

Comments