Skip to main content

Nyota wa Kibao cha CALL BOX Ajutia wimbo wake huo!



MWANAMUZIKI nyota nchini, Muumin Mwinjuma amesema hakuna kitu anachokijutia katika maisha yake kimuziki kama kutunga wimbo wa Call Box.

Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Muumin alisema wimbo huo ulipoteza heshima yake kimuziki na kumfanya achukiwe na wanawake wengi kwa kuhisi alimtungia mkewe wa pili.

Muumin alisema hadi sasa bado anakuna kichwa ili kurejesha heshima yake kimuziki, hasa kwa wanawake, ambao alikiri kuwa ndiyo mashabiki wake wakubwa.

Alikanusha madai kuwa, alitunga wimbo huo kwa lengo la kusimulia mkasa uliomfanya aachane na mkewe wa pili baada ya kumfumania mara mbili.

"Huu wimbo nilipewa na rafiki yangu mmoja, ambaye ni mganga wa kienyeji, aliniomba niuimbe. Bahati mbaya sana, nilirekodi wimbo huu muda mfupi baada ya kuachana na mke wangu, ndio sababu mashabiki wengi walidhani nimemwimbia yeye,"alisema.

Muumin alisema mashabiki wake wengi ni wanawake kutokana na kuzipokea vizuri nyimbo zake za Mgumba namba moja na namba mbili pamoja na Kilio cha Yatima, hivyo kumchukulia kama mtetezi wao.

Mwimbaji huyo mkongwe alisema amekuwa akitunga nyimbo zake nyingi kutokana na hisia, lakini wakati mwingine hufanya hivyo kutokana na kushuhudia ama kusikia mikasa mbalimbali.

Akisimulia mkasa uliosababisha atengane na mkewe wa pili, Muumin alisema aliwahi kumfumania mara mbili akifanya mapenzi na rafiki zake wawili.

"Ni matukio yaliyonisikitisha na kuhuzunisha sana kwa sababu watu niliomkuta nao ni rafiki zangu wa karibu wa kufa na kuzikana. Ni watu, ambao wamekuwa wakinisaidia na hadi leo ni rafiki zangu,"alisema mwanamuziki huyo.

Aliongeza kuwa, hakutaka kugombana na rafiki zake hao kwa sababu alichobaini ni kwamba, mkosaji mkubwa alikuwa mkewe.

"Alikuwa akiwafahamu vizuri watu hawa kwamba ni rafiki zangu, hivyo hakuwa na sababu ya kuhusiana nao kimapenzi. Hiyo ndiyo sababu kubwa iliyonifanya niachane naye,"alisema.

Muumin alikiri kuwa, kwa sasa amefunga ndoa na mwanamke mwingine, ikiwa ni ndoa yake ya tatu, lakini hapendi ijulikane kwa hofu ya kusukamwa kwa maneno.

Mwimbaji huyo mwenye sauti yenye mvuto alisema, mara nyingi baadhi ya watu wamekuwa wakimsakama kila anapofanya jambo fulani, hivyo ameona ni vyema afanye mambo yake kimya kimya.

Kwa sasa, Muumin ni kiongozi wa bendi ya Victoria Sound, aliyoianzisha mwaka jana baada ya kujiengua katika bendi ya Twanga Pepeta International.

Muumin alisema bendi ya Victoria Sound sio mpya kwa sababu ilianzishwa miaka sita iliyopita. Alisema kilichofanyika ni kuisuka upya.

Kwa mujibu wa Muumin, tayari wameshatunga vibao vipya vinne na wameshaanza kuvipiga kwenye kumbi mbalimbali wanazofanya maonyesho.

Alivitaja vibao hivyo kuwa ni Shamba la Bibi na Utafiti wa mapenzi, alivyovitunga yeye mwenyewe. Aliviita vibao hivyo kuwa ni moto wa kuotea mbali.

Vibao vingine ni Mama Bahati, kilichotungwa na mpiga gita la rythim, Yohana Mbatizaji na Mwisho wa siku, kilichotungwa na Waziri Sonyo.

Muumin alitamba kuwa, baada ya kuisuka upya bendi hiyo, wapinzani wao wakubwa kwa sasa watakuwa Twanga Pepeta na FM Academia.

Mbali na Muumin, Sonyo na Yohana, wanamuziki wengine wanaounda bendi hiyo ni Selemani Mumba, anayepiga gita la solo na Moshi Hamisi, anayepiga kinanda.

Wengine ni George Gama, anayepiga magita yote matatu, Januari Joseph, Ciana Jordan, Ramso Bushoke, Jonas Mlembuka na Mussa Kalenga, ambao ni waimbaji.

Wanamuziki wengine wanaounda bendi hiyo ni Kassim Mumba, anayepiga gita la besi, Abdalla Hussein anayepiga kinanda na Vaninga Swalehe,anayepiga tumba.

Bendi hiyo inakamilishwa na wacheza shoo, Omari Mussa 'Bokilo', Joha Juma, Mariam Othaman, Farida Omari, Lilian Wayanga, Nadia Benjamin na Sophia Ramadhani.Chanzo kimocha kimeeleza.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...